image

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa

Ulinzi na Usalama


Wakati wa Ukhalifa wa Makhalifa wanne ulinzi uliimarishwa kwa kiwango kikubwa. Wakati wa Mtume(s.a.w) hakukua na jeshi maalum. Kila mtu alikuwa askari na vita ilipofika Waislamu walijitokeza wakapewa mafunzo na kwenda vitani. Ni kweli pia kuwa katika Dola ya Kiislamu kila Muumin ni askari wa Allah(s.w) na wakati wowote anapotakiwa ni lazima awe tayari kupigania dini ya Mwenyezi Mungu.



β€œEnyi mlioamini Je! Nikujulisheni biashara itayokuokoeni na adhabu iumizayo(61:10).


Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na piganieni dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu.......” (61:11)


Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waislamu nafsi zao na mali zao ili nae awape Pepo. Wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu wanauwa na wanauwawa.............” (9:111)


Ni dhahiri Waislamu ni askari wa Mwenyezi Mungu. Pamoja na hivi tangu wakati wa Khalifa wa pili Umar, liliundwa jeshi kama yalivyo majeshi ya kileo. Khalifa ndie aliyekuwa mkuu wa majeshi, aliteua kamanda wa jeshi na makamanda wa mikoa na wilaya.


Idara ya ulinzi ilianzishwa na askari wote waliorodheshwa na utaratibu wa mshahara na posho ulianza kutumika kwa askari wa kudumu, wakujitolea na wale waliopigana vita vya awali kama Badr, Uhud, n.k.


Nchi iligawanywa kwenye maeneo ya kiulinzi, makao makuu ya maeneo haya yakawa Madina, Kufa, Basra, Mosul, Fustat, Damaskas, Hems, Jordan na Palestine. Katika sehemu zote hizi kambi zilijengwa kwa ajili ya askari. Mashamba ya mifugo yalipanuliwa kwa matumizi ya farasi na ngamia wa vita.


Pamoja na askari wa farasi na wa miguu jeshi la maji lilianza katika Ukhalifa wa Uthman. Vita vya kwanza vya majini vilipiganwa na Muawiya alipovamia Cyprus mnamo mwaka wa 28 A.H. Makao makuu ya Jeshi la maji yalikuwa Alexandria Misri.



Usalama wa Taifa



Idara ya usalama ilikuzwa. Ilianza tangu wakati wa Mtume(s.a.w) na kuendelezwa wakati wa Makhalifa wanne. Walitumika wanajeshi na wasio wanajeshi katika kazi ya kupata habari ndani na nje ya Dola na hasa kujua mwenendo wa adui. Wapo Machief, kwa mfano Syria, waliochaguliwa kuwa wanausalama, kuchunguza mwenendo wa Warumi. Palestine lilikuwepo kundi la Wayahudi lililojulikana kwa jina la Samara lilijizatiti katika upelelezi. Khalifa Umar(r.a) aliweka wapelelezi ndani ya jeshi (military intelligence) ili apate habari zote. Hivyo idara hii nayo ilisaidia sana katika ulinzi na usalama wa Dola ya Kiislamu.


Hivi ndivyo Serikali ya Kiislamu ilivyoendeshwa kwa muda wa miaka 40 kuanzia kwa Mtume(s.a.w) hadi Makhalifa wake wanne na imekuwa ndio msingi wa uendeshaji wa Serikali zote za leo Duniani.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 230


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...

Hstora ya Nabii Ilyasa
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya Nabii Ilyasa Soma Zaidi...

Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake. Soma Zaidi...

Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.
Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume. Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

Historia ya Nabii Ya'qub
Katika somo hili utawenda ujfunz ahstoraya Nabii Ya'qub na familia yake Soma Zaidi...

Mtume kumuoa bi khadija
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija. Soma Zaidi...

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta
Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta Soma Zaidi...

Shukurani za Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Allah(s.w)
Kwa neema hii ya kuruzukiwa watoto wawili - Ismail na Is- haqa(a. Soma Zaidi...

fadhila za kusoma quran
Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s. Soma Zaidi...

Jifunze historia ya uislamu toka mitume na manabii, kuja kwa makhalifa na maimamu hadi leo
Soma Zaidi...