Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa

Kuanzishwa kwa vitenge vya ulinza na Usalama, na usalama wa taifa

Ulinzi na Usalama


Wakati wa Ukhalifa wa Makhalifa wanne ulinzi uliimarishwa kwa kiwango kikubwa. Wakati wa Mtume(s.a.w) hakukua na jeshi maalum. Kila mtu alikuwa askari na vita ilipofika Waislamu walijitokeza wakapewa mafunzo na kwenda vitani. Ni kweli pia kuwa katika Dola ya Kiislamu kila Muumin ni askari wa Allah(s.w) na wakati wowote anapotakiwa ni lazima awe tayari kupigania dini ya Mwenyezi Mungu.



β€œEnyi mlioamini Je! Nikujulisheni biashara itayokuokoeni na adhabu iumizayo(61:10).


Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na piganieni dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu.......” (61:11)


Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waislamu nafsi zao na mali zao ili nae awape Pepo. Wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu wanauwa na wanauwawa.............” (9:111)


Ni dhahiri Waislamu ni askari wa Mwenyezi Mungu. Pamoja na hivi tangu wakati wa Khalifa wa pili Umar, liliundwa jeshi kama yalivyo majeshi ya kileo. Khalifa ndie aliyekuwa mkuu wa majeshi, aliteua kamanda wa jeshi na makamanda wa mikoa na wilaya.


Idara ya ulinzi ilianzishwa na askari wote waliorodheshwa na utaratibu wa mshahara na posho ulianza kutumika kwa askari wa kudumu, wakujitolea na wale waliopigana vita vya awali kama Badr, Uhud, n.k.


Nchi iligawanywa kwenye maeneo ya kiulinzi, makao makuu ya maeneo haya yakawa Madina, Kufa, Basra, Mosul, Fustat, Damaskas, Hems, Jordan na Palestine. Katika sehemu zote hizi kambi zilijengwa kwa ajili ya askari. Mashamba ya mifugo yalipanuliwa kwa matumizi ya farasi na ngamia wa vita.


Pamoja na askari wa farasi na wa miguu jeshi la maji lilianza katika Ukhalifa wa Uthman. Vita vya kwanza vya majini vilipiganwa na Muawiya alipovamia Cyprus mnamo mwaka wa 28 A.H. Makao makuu ya Jeshi la maji yalikuwa Alexandria Misri.



Usalama wa Taifa



Idara ya usalama ilikuzwa. Ilianza tangu wakati wa Mtume(s.a.w) na kuendelezwa wakati wa Makhalifa wanne. Walitumika wanajeshi na wasio wanajeshi katika kazi ya kupata habari ndani na nje ya Dola na hasa kujua mwenendo wa adui. Wapo Machief, kwa mfano Syria, waliochaguliwa kuwa wanausalama, kuchunguza mwenendo wa Warumi. Palestine lilikuwepo kundi la Wayahudi lililojulikana kwa jina la Samara lilijizatiti katika upelelezi. Khalifa Umar(r.a) aliweka wapelelezi ndani ya jeshi (military intelligence) ili apate habari zote. Hivyo idara hii nayo ilisaidia sana katika ulinzi na usalama wa Dola ya Kiislamu.


Hivi ndivyo Serikali ya Kiislamu ilivyoendeshwa kwa muda wa miaka 40 kuanzia kwa Mtume(s.a.w) hadi Makhalifa wake wanne na imekuwa ndio msingi wa uendeshaji wa Serikali zote za leo Duniani.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 513

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao

Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

β€œKwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Soma Zaidi...
Mikataba ya aqabah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...