Vipimo muhimu wakati wa ujauzito
Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito.
1. Upimaji wa damu ili kuangalia kiwango cha damu kilichomo mwilini, kwa kawaida mjamzito kabla ya kujifungua anapaswa kuwa na damu ya kutosha kwa sababu wakati wa kujifungua Mama utoa damu nyingi sana kwa hiyo kila mwezi mama uchukua dawa za follic ili kuweza kuongeza damu na pia akina Mama uambiwa kula vyakula muhimu vya kuongeza damu kwa hiyo wajawazito wote nwanapaswa kupima na kuangalia kiasi cha damu kilichomo mwilini mwa Mama.
2. Upimaji wa damu ili kuangalia group la Mama na baba kama zinaendana, mara nyingi Watu wengi wameoana tu na hawajui magroup yao ya damu hali hii uleta shida kwa mtoto wakati wa kujifungua kwa sababu pengine ya kuwepo kwa RH ambayo usababisha kutokwa kwa mimba na kwa upima magroup yao ya damu kila mtu anaweza kujua watu gani anapaswa kuwapatia na mtu gani atapokea kutoka kwake.
3. Pia Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende kwa sababu ugonjwa huu ni hatari pindi akiwa tumboni kwa hiyo wazazi wote wanapaswa kuudhulia kliniki kwa mara ya kwanza ili waweze kupima maambukizi ya kaswende, kama wote wanayo wanapaswa kutibiwa ili kuepu kujifungua mtoto mwenye ugonjwa huu maana ni hatari.
4. Pia Mama mjamzito anapaswa kupima maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na hatimaye kumwepusha mtoto kuzaliwa akiwa na Maambukizi, na pia kujua afya ya Mama ili kuweza kuwa makini wakati wa kujifungua na kuepusha kuendelea kumpatia huduma na kuendelea vizuri, pia Baba na Mama wote wanapaswa kujua hali zao na kuendelea na matibabu.
5.Mama mjamzito anapaswa kupima Malaria.
Tunajua kubwa Malaria ni tishio kwa Mama wakati wanapaswa kupima ugonjwa wa Malaria, kwa kuwa Mama mara nyingi upewa dawa za SP ili kuweza kuzuia Malaria kwa Mama mjamzito na mtoto kwa hiyo ni jambo la muhimu kupima Malaria na kuepuka shida yake mbalimbali.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 ai web app 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Hatua kwa hatua: Jinsi ya kulea ujauzito katika miezi tisa.
Safari ya ujauzito ni ya kusisimua, yenye mabadiliko mengi ya kimwili na kihisia. Kulea ujauzito kwa usahihi ni uwekezaji wa afya ya mtoto na mama. Mwongozo huu unatoa hatua kwa hatua jinsi ya kulea ujauzito katika kila trimester ili kuhakikisha mtoto anakuwa salama na mama anabaki na afya njema.
Soma Zaidi...Fahamu siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu.
Soma Zaidi...Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom
Soma Zaidi...Huduma kwa wanaotoa damu yenye mabonge
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.
Soma Zaidi...Faida za kula yai lililopikwa kwa mama mjamzito
Yai lililopikwa ni chanzo kizuri cha protini, vitamini, na madini muhimu kwa mama mjamzito. Husaidia katika ukuaji wa mtoto tumboni, afya ya mama, na kuimarisha kinga ya mwili.
Soma Zaidi...Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti
Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti
Soma Zaidi...