Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
1. Kwanza kabisa ugumu wa choo ni hali inayotokea kwa wajawazito ambapo choo ushindwa kutoka nje au kwa wakati mwingine utoka nje kwa kutumia nguvu kubwa hii ni kwa sababu kuna mabadiliko kwenye mfumo wa umengenywaji ambapo usababisha maji kuisha kwenye kinyesi na kusababisha ugumu wa kinyesi na pengine hali huu usababishwa na kubadilika kwa homoni za mimba hasa hasa progesterone homoni.
2. Kwa hiyo kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo hili la choo kuwa kigumu, Mama wajawazito wanapaswa kunywa maji mengi ili kurainisha chuo na pia wanapaswa kutumia aina mbalimbali za matunda kama vile mapapai, maparachichi, maembe na matunda mengine mbalimbali ambayo ufanya kinyesi kuwa kiraini, pia wanapaswa kutumia mboga mboga za majani kwa wingi, na chakula chenye mlo kamili ili kuweza kupunguza hali huu ya kinyesi kuwa kigumu.
3. Kuna njia nyingine ambayo ni kunywa maji asubuhi kabla haujala chochote na hali hii pia upunguza ugumu wa choo, na pia akina Mama wajawazito wanapopata tatizo kama hili wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo kwa asili yake ufanya kinyesi kuwa kigumu kama vile vyakula vya mtama na vyakula vingine ambavyo vinaweza kuongeza tatizo zaidi.
4. Na pia wanawake wajawazito wanapaswa kufanya mazoezi mengi hasa hasa kutembea walau kwa dakika thelathini kila siku ili kuweza kulifanya tumbo kubwa laini na kinyesi kupunguza ugumu wake, na baada ya kufanya mazoezi akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha. Na pia wauguzi na wataalam wa afya wanapaswa kuwaeleza wazi wajawazito kubwa huu ni ugonjwa ambao upo na uisha tu baada ya kujifungua.
5. Kwa kawaida kuna jamii nyingine ambazo uwa na imani potovu na kufanya vitendo ambavyo ki afya hairuhusiwi kwa Maana mama mjamzito akipatwa na tatizo la ugumu wa kinyesi wanachukua mti wanamkalisha mama na kuanza kuchokonoa kinyesi ili kitoke taratibu hii ni hatari kwa sababu wanaweza kuharibu na sehemu mbalimbali kwa sababu ya kuchokonoa na mti kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii nzima ili kuepuka udhalilishaji wa kijinsia na kusababisha uharibifu kwa akina Mama.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto.
Soma Zaidi...Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, mara nyingi tatizo hili uwakumba akina mama mbalimbali ambapo mtoto uzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Soma Zaidi...