Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
1. Kwanza kabisa ugumu wa choo ni hali inayotokea kwa wajawazito ambapo choo ushindwa kutoka nje au kwa wakati mwingine utoka nje kwa kutumia nguvu kubwa hii ni kwa sababu kuna mabadiliko kwenye mfumo wa umengenywaji ambapo usababisha maji kuisha kwenye kinyesi na kusababisha ugumu wa kinyesi na pengine hali huu usababishwa na kubadilika kwa homoni za mimba hasa hasa progesterone homoni.
2. Kwa hiyo kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo hili la choo kuwa kigumu, Mama wajawazito wanapaswa kunywa maji mengi ili kurainisha chuo na pia wanapaswa kutumia aina mbalimbali za matunda kama vile mapapai, maparachichi, maembe na matunda mengine mbalimbali ambayo ufanya kinyesi kuwa kiraini, pia wanapaswa kutumia mboga mboga za majani kwa wingi, na chakula chenye mlo kamili ili kuweza kupunguza hali huu ya kinyesi kuwa kigumu.
3. Kuna njia nyingine ambayo ni kunywa maji asubuhi kabla haujala chochote na hali hii pia upunguza ugumu wa choo, na pia akina Mama wajawazito wanapopata tatizo kama hili wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo kwa asili yake ufanya kinyesi kuwa kigumu kama vile vyakula vya mtama na vyakula vingine ambavyo vinaweza kuongeza tatizo zaidi.
4. Na pia wanawake wajawazito wanapaswa kufanya mazoezi mengi hasa hasa kutembea walau kwa dakika thelathini kila siku ili kuweza kulifanya tumbo kubwa laini na kinyesi kupunguza ugumu wake, na baada ya kufanya mazoezi akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha. Na pia wauguzi na wataalam wa afya wanapaswa kuwaeleza wazi wajawazito kubwa huu ni ugonjwa ambao upo na uisha tu baada ya kujifungua.
5. Kwa kawaida kuna jamii nyingine ambazo uwa na imani potovu na kufanya vitendo ambavyo ki afya hairuhusiwi kwa Maana mama mjamzito akipatwa na tatizo la ugumu wa kinyesi wanachukua mti wanamkalisha mama na kuanza kuchokonoa kinyesi ili kitoke taratibu hii ni hatari kwa sababu wanaweza kuharibu na sehemu mbalimbali kwa sababu ya kuchokonoa na mti kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii nzima ili kuepuka udhalilishaji wa kijinsia na kusababisha uharibifu kwa akina Mama.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na WA awake na wasichana Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji na kuepuka mimba zisizotarajiwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...Miongoni mwa dalili zamwanzo za ujauzito ni maumivu ya tumbo ama kupatwa na damu kidogo. Mabadiliko ya ute ute sehemu za siri ni katika baadhi ya dalili. Endelea na makala hii utajifunza zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi saratani zinazowashambulia watoto. Hizi ni aina mbalimbali za saratani ambazo upenda kuwasumbua watoto ambao ni chini ya umri wa miaka mitano na uleta madhara katika kipindi cha makuzi yao.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...