picha

Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

1. Kwanza  kabisa ugumu wa choo ni hali inayotokea kwa wajawazito ambapo choo ushindwa kutoka nje au kwa wakati mwingine utoka nje kwa kutumia nguvu kubwa hii ni kwa sababu kuna mabadiliko kwenye mfumo wa umengenywaji ambapo usababisha maji kuisha kwenye kinyesi na kusababisha ugumu wa kinyesi na pengine hali huu usababishwa na kubadilika kwa homoni za mimba hasa hasa progesterone homoni.

 

2. Kwa hiyo kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo hili la choo kuwa kigumu, Mama wajawazito wanapaswa kunywa maji mengi ili kurainisha chuo na pia wanapaswa kutumia aina mbalimbali za matunda kama vile mapapai, maparachichi, maembe na matunda mengine mbalimbali ambayo ufanya kinyesi kuwa kiraini, pia wanapaswa kutumia mboga mboga za majani kwa wingi, na chakula chenye mlo kamili ili kuweza kupunguza hali huu ya kinyesi kuwa kigumu.

 

3. Kuna njia nyingine ambayo ni  kunywa maji asubuhi kabla haujala chochote na hali hii pia upunguza ugumu wa choo, na pia akina Mama wajawazito wanapopata tatizo kama  hili wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo kwa asili yake ufanya kinyesi kuwa kigumu kama vile vyakula vya mtama na vyakula vingine ambavyo vinaweza kuongeza tatizo zaidi.

 

4. Na pia wanawake wajawazito wanapaswa kufanya mazoezi mengi hasa hasa kutembea walau kwa dakika thelathini kila siku ili kuweza kulifanya tumbo kubwa laini na kinyesi kupunguza ugumu wake, na baada ya kufanya mazoezi akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha. Na pia wauguzi na wataalam wa afya wanapaswa kuwaeleza wazi wajawazito kubwa huu ni ugonjwa ambao upo na uisha tu baada ya kujifungua.

 

5. Kwa kawaida kuna jamii nyingine ambazo uwa na imani potovu na kufanya vitendo ambavyo ki afya hairuhusiwi kwa Maana mama mjamzito akipatwa na tatizo la ugumu wa kinyesi wanachukua mti wanamkalisha mama na kuanza kuchokonoa kinyesi ili kitoke taratibu hii ni hatari kwa sababu wanaweza kuharibu na sehemu mbalimbali kwa sababu ya kuchokonoa na mti kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii nzima ili kuepuka udhalilishaji wa kijinsia na kusababisha uharibifu kwa akina Mama.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/13/Thursday - 07:43:16 am Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 4111

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango

Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali.

Soma Zaidi...
Kwa nini hujapata siku zako za hedhi.

Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.

Soma Zaidi...
dalili za mimba baada ya tendo la ndoa na changa ndani ya wiki moja

Utajifunza dalili za mwanzoni za mimba changa kuanzia wiki moja baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa wanawake.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kufunga kizazi kwa wanawake.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Sababu za Kukoma hedhi (perimenopause)

Kukoma hedhi hufafanuliwa kuwa hutokea miezi 12 baada ya kipindi chako cha mwisho cha hedhi na huashiria mwisho wa mizunguko ya hedhi. Kukoma hedhi kunaweza kutokea katika miaka ya 40 au 50. Kukoma hedhi ni mchakato wa asili wa kibaolojia. Ingawa pia in

Soma Zaidi...
Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.

Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Upungufu wa homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.

Soma Zaidi...