Malengo kwa Akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, ni malengo ambayo yametolewa ili kuweza kusaidia mtoto azaliwe vizuri na mambo mengine kama tutakavyoona.
Malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.
1.Lengo la kwanza kabisa ni kuhakikisha kuwa Magonjwa hatarishi kwa Mtoto na Mama yanajulikana mapema na yanadhibitiwa mapema, kwa mfano Magonjwa kama vile Magonjwa ya zinaa na Maambukizi ya virus vya ukimwi, Magonjwa kama yanatibika watayatibu kama hayatibiki dawa maalum zitatolewa ili kumkinga Mama na mtoto.
2.Kuhakikisha kwamba Mama anakuwa na vitu vyote muhimu ki afya kwa ajili ya yeye na mtoto kwa mfano kuwa na damu ya kutosha, vitamini za kutosha,kubwa na madini ya kutosha, mwili kuwa na kinga ya kutosha na kutokuwepo kwa magonjwa hatarishi ya kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.
3.Tunafanya hivyo ili kumpa Mama elimu kama vile kuepuka mambo hatarishi kabla ya kubeba mimba kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi ya vileo vikali, matumizi ya madawa ya kienyeji, kuishi kwenye sehemu za viwanda vyenye kemikali kali, kutumia vitu vyote vyenye mionzi, kuwa na mazoezi yanayozidi mipaka kwa kufanya hivyo tutamwandaa mama ili aweze kupata mtoto asiye na Magonjwa.
4.Kwa hiyo basi tunapaswa kuwaelimisha wachumba wote na akina Mama wanaoendelea kuzaa wajiandae mapema ili kuweza kuepuka matatizo ya kupata watoto wenye ulemavu na Magonjwa ambayo yatawatesa katika maisha pale wazazi wanapoangaika ili kumtibisha mtoto na hatimaye kusababisha uchumi wa familia kushuka kwa hiyo tuendelee kutafakari msemo huu ambao unasema usipoziba ufa utajenga ukuta kwa hiyo wapendwa maandalizi ni ya muhimu sana na tunaokoa mambo mengi sana.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Madhara ya kiafya ya kupiga punyeto
Post hii inakwenda kukutania madhara ya kuoiga punyeto kwa afya yako.
Soma Zaidi...Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Aina za uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.
Soma Zaidi...Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua
Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.
Soma Zaidi...Dalili za mimba ya watoto mapacha
Makala hii itakwenda kukupa dalili ambazo zinaonyesha kuwa mimba ni ya mapacha. Dalili hizi zitahitajika kuthibitishwa na kipimo cha daktari ili kujuwa kuwa ni kweli.
Soma Zaidi...Sababu za kuwepo fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa Ugonjwa wa fangasi,ni sababu mbalimbali ambazo zinaweza kusababisha fangasi.
Soma Zaidi...