Malengo kwa Akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, ni malengo ambayo yametolewa ili kuweza kusaidia mtoto azaliwe vizuri na mambo mengine kama tutakavyoona.
Malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.
1.Lengo la kwanza kabisa ni kuhakikisha kuwa Magonjwa hatarishi kwa Mtoto na Mama yanajulikana mapema na yanadhibitiwa mapema, kwa mfano Magonjwa kama vile Magonjwa ya zinaa na Maambukizi ya virus vya ukimwi, Magonjwa kama yanatibika watayatibu kama hayatibiki dawa maalum zitatolewa ili kumkinga Mama na mtoto.
2.Kuhakikisha kwamba Mama anakuwa na vitu vyote muhimu ki afya kwa ajili ya yeye na mtoto kwa mfano kuwa na damu ya kutosha, vitamini za kutosha,kubwa na madini ya kutosha, mwili kuwa na kinga ya kutosha na kutokuwepo kwa magonjwa hatarishi ya kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.
3.Tunafanya hivyo ili kumpa Mama elimu kama vile kuepuka mambo hatarishi kabla ya kubeba mimba kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi ya vileo vikali, matumizi ya madawa ya kienyeji, kuishi kwenye sehemu za viwanda vyenye kemikali kali, kutumia vitu vyote vyenye mionzi, kuwa na mazoezi yanayozidi mipaka kwa kufanya hivyo tutamwandaa mama ili aweze kupata mtoto asiye na Magonjwa.
4.Kwa hiyo basi tunapaswa kuwaelimisha wachumba wote na akina Mama wanaoendelea kuzaa wajiandae mapema ili kuweza kuepuka matatizo ya kupata watoto wenye ulemavu na Magonjwa ambayo yatawatesa katika maisha pale wazazi wanapoangaika ili kumtibisha mtoto na hatimaye kusababisha uchumi wa familia kushuka kwa hiyo tuendelee kutafakari msemo huu ambao unasema usipoziba ufa utajenga ukuta kwa hiyo wapendwa maandalizi ni ya muhimu sana na tunaokoa mambo mengi sana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 ai web app 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Je endapo mama atafanya tendo la ndoa wiki moja kabla ya kuingia hedhi anaweza kupata ujauzito?
Zipo siku maalumu ambazo mwanamke hupata mimba. Siku hizi huzoeleka kwa jina la siku hatari. Je ungependa kufahamu mengi kuhusu siku hatari, endelea na makala hii.
Soma Zaidi...Mambo ambayo mama anapaswa kujua akiwa mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mambo anyopaswa kujua akiwa mjamzito. Ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa mama akiwa mjamzito.
Soma Zaidi...Ni vipi nitagundua kuwa nina ujauzito?
Hali ya ujauzito huanza kutabirika Mara tu ya kujamiana, pia chemikali (hormon) za mwili huanza mchakato wa kuongeza na kupunguza utendaji kazi wa kemikali hizo mfano.follical stimulating hormon (FSH) na lutenazing hormon kuivisha yai tayari kwa kutengen
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.
Soma Zaidi...Njia za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha kwa sababu kuna familia nyingi zinakosa watoto sio kwa sababu ni tasa ila kuna njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa
Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...