picha

Malengo kwa Akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, ni malengo ambayo yametolewa ili kuweza kusaidia mtoto azaliwe vizuri na mambo mengine kama tutakavyoona.

Malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba.

1.Lengo la kwanza kabisa ni kuhakikisha kuwa Magonjwa hatarishi kwa Mtoto na Mama yanajulikana mapema na yanadhibitiwa mapema, kwa mfano Magonjwa kama vile Magonjwa ya zinaa na Maambukizi ya virus vya ukimwi, Magonjwa kama yanatibika watayatibu kama hayatibiki dawa maalum zitatolewa ili kumkinga Mama na mtoto.

 

2.Kuhakikisha kwamba Mama anakuwa na vitu vyote muhimu ki afya kwa ajili ya yeye na mtoto kwa mfano kuwa na damu ya kutosha, vitamini za kutosha,kubwa na madini ya kutosha, mwili kuwa na kinga ya kutosha na kutokuwepo kwa magonjwa hatarishi ya kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.

 

3.Tunafanya hivyo ili kumpa Mama elimu kama vile kuepuka mambo hatarishi kabla ya kubeba mimba kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi ya vileo vikali, matumizi ya madawa ya kienyeji, kuishi kwenye sehemu za viwanda vyenye kemikali kali, kutumia vitu vyote vyenye mionzi, kuwa na mazoezi yanayozidi mipaka kwa kufanya hivyo tutamwandaa mama ili aweze kupata mtoto asiye na Magonjwa.

 

4.Kwa hiyo basi tunapaswa kuwaelimisha wachumba wote na akina Mama wanaoendelea kuzaa wajiandae mapema ili kuweza kuepuka matatizo ya kupata watoto wenye ulemavu na Magonjwa ambayo yatawatesa katika maisha pale wazazi wanapoangaika ili kumtibisha mtoto na hatimaye kusababisha uchumi wa familia kushuka kwa hiyo tuendelee kutafakari msemo huu ambao unasema usipoziba ufa utajenga ukuta kwa hiyo wapendwa maandalizi ni ya muhimu sana na tunaokoa mambo mengi sana.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1482

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...
Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano

Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.

Soma Zaidi...
Yajue mazoezi ya kegel

Posti inahusu zaidi mazoezi ya kegel, ni mazoezi ambayo ufanywa na watu wengi na sehemu yoyote yanaweza kufanywa kama vile chumbani, sebuleni, uwanjani na sehemu yoyote ile na kwa watu tofauti.

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.

Soma Zaidi...
Mama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?

Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?

Soma Zaidi...
Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha.

Soma Zaidi...