Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.
Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Mambo ya kuzingatia ikiwa mimba imetoka.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu chanzo cha mimba kutoka nini ni nini? Kama ni mimba ya kwanza mama anapaswa kuwa makini na kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya kuhusu ni wakati gani wa kubeba mimba Ili kuweza kuepuka madhara ya kutoka kwa mimba.
2. Pia Mama aliyetoa mimba anapaswa kuhudumiwa kama mama yule aliyejifungua kwa mfano mimba ikitoka na miezi sita maumivu aliyoyapata yule aliyejifungua na aliyetoa mimba ni Yale Yale na pengine kama vyuma vya kutoa mimba vimetumika maumivu ni makubwa zaidi.
3. Pia Mama anapaswa kujua ni wakati gani wa kubeba mimba nyingine, kwa kawaida mama akitoa mimba anapaswa kubeba mimba nyingine baada ya miezi sita kwa sababu mama aliyetoa mimba anaweza kuingia kwenye siku zake za mwezi ndani ya siku ishilini na Moja.
4. Pia Mama anapaswa kufahamu kwamba akibeba mimba kabla ya miezi sita anaweza kupata tatizo hilo hilo kwa sababu via vya uzazi na viungo vya kusaidia kushika mtoto vinakuwa bado havijakomaa kuweza kubeba mimba tena na kusababisha kutoka kwa mimba mara nyingine kama mama amebeba mimba kabla ya mda.
5. Vile vile jamii inapaswa kuelewa kwamba mimba kutoka sio laana kwa jamii Bali ni kwa sababu mbalimbali kama vile maambukizi, na mambo mengine mengi kwa hiyo jamii inapaswa kutoa Mila potofu na kuwepo kwa ushirikiano kwa mama na familia kwa ujumla.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Aina mbalimbali za mimba kutoka.
Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.
Soma Zaidi...Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.
Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil
Soma Zaidi...Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri
Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.
Soma Zaidi...Je matiti kujaa na chuchu kuuma inakua ni dalili za hedhi?
Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito.
Soma Zaidi...Huduma kwa wanaopata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wanaoingia kwenye siku zao zaidi ya mara moja kwa mwezi.
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango
Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur
Soma Zaidi...