Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.
Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Mambo ya kuzingatia ikiwa mimba imetoka.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu chanzo cha mimba kutoka nini ni nini? Kama ni mimba ya kwanza mama anapaswa kuwa makini na kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya kuhusu ni wakati gani wa kubeba mimba Ili kuweza kuepuka madhara ya kutoka kwa mimba.
2. Pia Mama aliyetoa mimba anapaswa kuhudumiwa kama mama yule aliyejifungua kwa mfano mimba ikitoka na miezi sita maumivu aliyoyapata yule aliyejifungua na aliyetoa mimba ni Yale Yale na pengine kama vyuma vya kutoa mimba vimetumika maumivu ni makubwa zaidi.
3. Pia Mama anapaswa kujua ni wakati gani wa kubeba mimba nyingine, kwa kawaida mama akitoa mimba anapaswa kubeba mimba nyingine baada ya miezi sita kwa sababu mama aliyetoa mimba anaweza kuingia kwenye siku zake za mwezi ndani ya siku ishilini na Moja.
4. Pia Mama anapaswa kufahamu kwamba akibeba mimba kabla ya miezi sita anaweza kupata tatizo hilo hilo kwa sababu via vya uzazi na viungo vya kusaidia kushika mtoto vinakuwa bado havijakomaa kuweza kubeba mimba tena na kusababisha kutoka kwa mimba mara nyingine kama mama amebeba mimba kabla ya mda.
5. Vile vile jamii inapaswa kuelewa kwamba mimba kutoka sio laana kwa jamii Bali ni kwa sababu mbalimbali kama vile maambukizi, na mambo mengine mengi kwa hiyo jamii inapaswa kutoa Mila potofu na kuwepo kwa ushirikiano kwa mama na familia kwa ujumla.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Endapo nina dalili za mimba na nikipima sina mimba, je, tatizo ni nini?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Ujue Ute kwenye uke
Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.
Soma Zaidi...SABABU ZA KUKOSA NGUVU ZA KIUME AMA KUWA NA UWEZO MDOGO WA KUHIMILI TENDO LA NDOA
Hii ni hali inayowapata wanaume kushindwa kuhimili tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki, kliniki nisehemu ambayo mtoto hupelekwa Ili kujua maendeleo ya mtoto akiwa chini ya umri wa miaka mitano
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...Sifa za siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba
Soma Zaidi...