Uyoga (mushrooms)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga

Uyoga (mushroom)

Uyoga pia ni katika vyakula vya asili, ijapokuwa upatikanaji wake umekuwa mchache siku hizi. Shukrani ziwaendee wataalamu wa kilimo, kwa sasa tunaweza kuzipata mbegu za uyoga kutoka maabara na kulima uyoga popote pale. Wataalamu wa mimea wanaamini kuwa uyoga si katika mimiea kwani uyoga upo katika kundi la viumbe liitwalo fungi (kingdom fungi). ila tunapozungumzia vyakula uyoga tunauweka kwenye kundi la mbogamboga. Uyoga una virutubisho vingi na vizuri kwa afya.

 

Kulinda mwili zidi ya cancer, Kama ilivyokuwa kwenye matunda na mboga zingine kuwa kuna antioxidant ambayo hii ni chembechembe inayopambana na sumu na kemikali ambazo zinaweza kuathiri seli za mwili wako. Basi kwenye uyoga pia kuna antioxidant kama iliyo karoti na matunda mengine tuloona hapo juu. Hii husaidia kwa kiwango kikubwa kupambana na kuuwa seli za kansa au saratani ambazo zinatengenezwa mwilini.

 

Mna kwenye uyoga madini yanayoitwa selenium, madini haya huwezi kuyapata kwenye matunda mngi sana na mbogamboga nyingi lakini haya utayapata kwa urahisi kwenye uyoga. Madini haya husaidia katika kuuwa seli sa saratani, pia kuzuia kuota kwa uvimbe unaosababishwa na saratani na aina zingine za vimbe.

 

Uyoga una vitamin D, ambavyo hivi pia husaidia katika kupambana na kuthibiti kukuwa kwa seli za saratani mwilini. Vitamin D husaidia katika utendaji mwema wa kazi za DNA. Itambulike kuwa saratani huanza kuathiri DNA ndio baadae huendelea kukuwa ndani ya mwili na baadae kuathiri sehemu za mwili. Hivyo uyoga una chembechembe hizi ambazo husaidia katika kupamba na nsa saratani.

 

Uyoga husaidia katika kuthibiti na kupamabana na kisukari hususan type 2 diabetes. Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa ulaji wa vyakula vyenye kambakamba (fiber) husaidia katika kushusha kiwango cha sukari kwenye damu. Hivyo husaidia katika kuimarisha afya ya itengenezwaji wa insulin.

 

Husaidia katika kuimarisha afya ya moyo, uwepo wa lkambakamba, madini ya potassium pamoja na vitamin C husaidia kwa kiwango kikubwa katika kuimarisha afya ya moyo (cardiovascular health). ulaji wa vyakula vyenye madini ya potassium kwa wingi pamoja na sodium kwa kiwango kidogo husaidia katika kupunguza shinikizo la damu hivyo husaidia kwa wale wenye presha ya kupanda ya damu.

 

Husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga mwilini (immune system). madini ya selenium yaliyomo kwenye uyoga kusaidia katika kushawishi na kustimulate mfumo wa afya mwilini katika kupambana na wadudu wavamizi. Madini haya husaidia katika kusahwishi T-cell au CD4 katika kupambana na wadudu wavamizi kama bakteria, virus na fangas. Beta-glucan inayopatikana kwenye ukuta wa seli za uyoga husaidia katika kuufanya mwili upambane vyema na wavamisi na kupamba nna na vijidudu vya maradhi.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1966

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Faida za kula papai

Posti hii inaonyesha Faida za kula papai.papai Ni tunda na Lina leta afya,nguvu na kuujenga mwili.

Soma Zaidi...
Boga (pumpkin)

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula kabichi

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kabichi

Soma Zaidi...
Vyakula vya vitamin D

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin D

Soma Zaidi...
Faida za kula Tufaha (epo)

Tufaha ni katika matunda adimu na matamu, je unazijuwa faida zake kkiafya?

Soma Zaidi...
Tufaha (apple)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza damu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya kuongeza damu

Soma Zaidi...
Yajuwe magonjwa matano yanayo tokana na utapiamlo

Post hii inakwenda kukutajia mahonjwa matano ambayo hutokana na utapia mlo.

Soma Zaidi...
Matunda yenye Vitamin C kwa wingi

Vitamin C ni katika vitamin vinavyosaidia sana mfumo wa Kinga kulinda mwili dhidi ya vimelea vya maradhi. Hapa nitakuletea orodha ya matunda ambayo yana vitamini C kwa wingi.

Soma Zaidi...