Vyakula salama na vilivyo hatari kwa mwenye kisukari, na vipi atajikinga na kisukari

Vyakula salama na vilivyo hatari kwa mwenye kisukari, na vipi atajikinga na kisukari

Makala hii inakwenda kukupa elimu juu ya vyakula na vinywaji vilivyo salama kwa mtu mwenye kisukari, na ni vyakula vipi ni hatari kwa mwenye kisukari. Pia utajifunza njia za kujilinda na kupata kisukari.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

VYAKULA SALAMA NA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
Kisuari ni hali ya mwili kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari hivyo kuachia sukari yote kuishia kwenye damu bila ya kuingia kwenye seli ili kutumika maeneo mbalimbali ya mwili. Na hutokea endapo uzalishwaji wa homoni ya insulini utakuwa katika shida. Eidha hutokea kwa sababu homoni ya insulini inayozalishwa si yenye kutosheleza ama mwili wenyewe unashindwa kuitumiahomoni ya insulini. Homoni ya insulin ndio ambayo hudhibiti kiwango cha sukari.

Vipi kisukari hutokea?
Mwili unahitaji sukari kwa ajili ya kuzalisha nishati yaani nguvu. Mwili pia unahifadhi sukari kwa matumizi ya baadaye. Endapo sukari mwilini itakuwa ni nyingi basi homoni ya insulini huzaliwa kwa wingi ili kupunguza sukari iliyozidi n akuihifadhi kwa matumizi yaa baadaye. Na endapo sukari itakuwa ni kidogo mwilili homoni ya insulini huzuiliwa hivyo mwili hutumua sukari iliyohifadhiwa. Kwa kufanya hivi kiwango cha sukari hudhibitiwa.

Sasa endapo kutatokea shida yeyote katika matumizi ya homoni ya insulini mwili utashindwa kuhifadhi sukari pia kuitumia sukari. Hivyo sukari itabakia kwenye damu bila ya kwenda kokote kwa matumizi. Hali hii ikitokea ndipo mtu huambiwa ana kisukari. Kisukari kinaweza kuwa ni kwa muda mfupi kama kwa baadhi ya wajawazito. Pia kinaweza kuwa ni cha kudumu, na hapa tunazungumzia type1 na type 2.

Mtu mwenye kisukari anatakiwa kuwa makini sana katika matumizi ya vyakula na vinywaji. Vinginevyo anaweza kuingia kwenye matatizo makubw aya kiafya. Je unavijuwa vyakula salama kwa nmwemye kisukari? Na je unavijuwa vyakula hatari kwa mwenye kisukari? Endelea na makala hii hadi mwisho:-



VYAKULA SALAMA KWA MWENYE KISUKARI
1.Samaki hasa wale wenye fati kwa wingi kama samlon na sardines
2.Mbogamboga za majani
3.Palachichi
4.Mayai
5.Mbegu za chia
6.Maharagwe
7.Kitunguu thaumu
8.Nyama yandege wafugwao kama kuku
9.Kahawa
10.Vinywaji visivyowekwa sukari
11.Jusi za mbogamboga
12.Usikoboe mahindi, mchele, na mtama
13.Matunda kwa uchache



VYAKULA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
1.Nafaka zilizokobolewa
2.Nafaka zilizoongezwa sukari
3.Mikate yenye sukari
4.Nafaka zisizo na kini
5.Mboga zenye chumvi nyingi
6.Mboga zilizoongezwa maziwa
7.Vinywaji vyote vya sukari usitumie mpaka kiwango chako cha sukari kiwe kipo katika udhibiti hata asali epukana nayo kwanza
8.Juisi zilizowekwa sukari ama zenye utamu kama za matunda
9.Vinywaji vya energy (energy drink)
10.Nyama ya kuoka
11.Nyama zenye mafuta mengi
12.Nyama ya ngurue
13.Maziwa fresh
14.Samaki wa kuoka
15.Soda



Njia za kujikinga na kisukari
1.Dhibiti uzito wako. Hakikisha huna uzito w akupitiliza
2.Fanya mazoezi mara kwa mara
3.Kula mlo kamili
4.Punguza misongo ya mawazo
5.Kunywa maji kwa wingi
6.Wacha kuvuta sigara
7.Punguza ama wacha unywaji wa pombe
8.Punguza ulaji wa sukari kwa wingi
9.Pendelea kunywa kahawa
10.Tumia dawa za asili kiasi uwezavyo

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1019

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kitunguu saumu
Kitunguu saumu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kitunguu saumu

Soma Zaidi...
Vyakula vya madini kwa wingi, na kazi za madini mwilini
Vyakula vya madini kwa wingi, na kazi za madini mwilini

Utajifunza vyakula vyenye madini kwa wingi, kazi za madini mwilini na athari za upungufu wake

Soma Zaidi...
Faida za kula ukwaju
Faida za kula ukwaju

Uchachu wa ukwaju, ndio ubora wake, kuna virutubisho vingi kwa kula ukwaju, soma makala hii

Soma Zaidi...
Vitamini na kazi zake
Vitamini na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi vitamini mbalimbali na kazi zake kwenye mwili,vitamini ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za madini ya chuma mwilini
Zijue kazi za madini ya chuma mwilini

Posti hii inahusu zaidi kazi za madini ya chuma mwilini,Ni madini ambayo ufanya kazi mbalimbali mwilini na pia utokana na vyakula mbalimbali ambavyo upatikana kwenye wanyama na mimea. Zifuatazo ni kazi za madini ya chuma.

Soma Zaidi...
Faida za kungumanga/nutmeg
Faida za kungumanga/nutmeg

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula kungumanga

Soma Zaidi...
Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake
Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za vyakula na kazi zake, hii ni Aina tatu za vyakula na kazi zake jinsi zinavyofanya kazi, hufanya kazi kama ifuatavyo,

Soma Zaidi...
Upungufu wa vitamin C mwilini
Upungufu wa vitamin C mwilini

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu upungufu wa vitamini C mwilini

Soma Zaidi...
Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako
Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako

Post huu inakwenda kukupa orodha ya madini muhimu kwa ajili ya afya yako.

Soma Zaidi...