Utajuwaje kama kidonda kupona
Posti hii inahusu zaidi juu ya kuhakiki kama kidonda kimepona kwa mgonjwa mwenye vidonda, kwanza kabisa tunajua kuwa vidonda uwanyima Watu raha na pengine kuwafanya wakate tamaa kama wapo hospitalini kwa hiyo tunapaswa kutumia njia zifuatazo ili kuweza ku
Uhakiki wa kidonda kupona.
1.Tunapaswa kuangalia kama mishipa ya damu inaweza kupita na kusafirisha damu kutoka upande mmoja kwenda mwingine. Kwa sababu sehemu yenye kila kidonda damu huwa haipiti ila kwa kadiri kinavyoendelea kupona hivyo hivyo ndiyo na mishipa ya damu inaanza kupita.
2 Kitu kingine ni kuangalia kiasi cha Maumivu kilichopo kwa kawaida kidonda kama ni kipya na maumivu yanakiwepo mengi na kadiri kinavyoendelea kupona na maumivu upungua kwa hiyo ukija kumruhusu Mgonjwa kwenda nyumbani akidai amepona kwanza kabisa jaribisha kama kuna maumivu au maumivu ni machache ambayo hata akiwa nyumbani anaweza kuyamudu na kupona vizuri.
3. Na pia tunapaswa kuangalia kama kidonda kinatoa maji maji, kama kinatoa maji hiyo ni Dalili kwamba matibabu bado yanahitajika na mgonjwa anapaswa kuendelea kupata matibabu au kupewa dawa za kutumia ili aweze kuendelea kuzitumia.
4.Kwa hiyo katika kutibu vidonda tunapaswa kuangalia na hali ya wagonjwa wetu ikoje kwa sababu pengine vidonda vknadhindwa kupona kwa sababu ya Maambukizi au kuwepo kwa madawa yanayopunguza kinga mwilini kwa kufanya hivyo Mgonjwa anaweza kutibiwa kwanza chanzo na mengine yanaendelea baadae.
5. Kwa hiyo pale ruhusa inapotolewa ili mgonjwa aendelee na tiba ni vizuri kumpa mashariti akiwa nyumbani namna ya kutunza kidonda chake na kama ana Maambukizi awe makini ili asiwambukize wengine na wale wanaomzunguka
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 web hosting 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Njia za kuzuia damu isiendelee kuvuja
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia damu isiendelee kuvuja, ni njia ambazo utumika ikiwa kuna damu inavuja kwenye sehemu yoyote ya mwili,kwa hiyo tunaweza kutumia njia hizi ili kuepuka kuendelea kuvuja kwa damu.
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.
Soma Zaidi...Faida za chanjo
Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Namna ya kutoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma anayopewa mgonjwa au mtu yeyote aliyepata ajali kabla ya kumpeleka hospitalini
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini
Soma Zaidi...