Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa pamoja na kitambi
1. Tunapaswa kufahamu kwamba mara nyingi tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa na kitambi ni mtindo wa maisha ambapo kwa walio wengi ujiachiaa kabisa katika maisha na vyakula, kwa mfano unaweza kuona mtu anatoka nyumbani kwenda kazini kwa kutumia gari na akifika kazini ni kukaa tu na jioni akitoka kazini ni kupiga bia na nyama yoyote ile na pengine anaongezea chips akitoka hapo anafika nyumbani ni kuangalia movies na kusubiria chakula, watu wanaishi hivyo hata bila ya mazoezi hatimaye kuota kitambi na unene kupita kiasi.
2. Kwa hiyo watu wanapaswa kubadilika na kufuata yafuatayo ili kuweza kuepuka na tatizo la kuwepo kwa vitambi kwa kubadilisha mtindo wa maisha kwa kupiga mazoezi mara kwa mara walau mara tatu kwa wiki pamoja na kutumia maji ya uvuguvugu ili kupunguza vitambi na unene uliopitiliza.
3. Epuka matumizi ya vyakula vya wanga.
Kwa kawaida kitu kikubwa ambacho kipo kwenye vyakula vya wanga ni starch na ndiyo inayosababisha kuwepo kwa unene uliopitiliza.
4. Epuka matumizi ya vyakula vyenye sukari nyingi.
Kwa kawaida tunajua kazi ya sukari ikiwa nyingi mwilini usababisha kuwepo kwa mwongezeko wa mwili pamoja na uzito kwa hiyo ni vizuri kutumia sukari kidogo kwenye vinywaji.
5. Kufunga ili kuweza kuchoma calories ambazo zimo mwilini ambazo utokana na ulaji wa vyakula vyenye wanga na sukari.
6. Tumia vyakula vyenye wingi wa protini na gari kwa kiasi kidogo na pia tumia uchache wa unga na sukari.
7. Katika kupunguza uzito ni vizuri kabisa kufahamu kwamba matumizi ya vyakula vya wanga mara kwa mara hata kama unafanya mazoezi sio rahisi kupunguza tatizo kwa hiyo punguza matumizi ya vyakula vyenye wanga.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kuwepo kwa kizungu Zungu,ni Dalili ambazo Uweza kujionyesha kwa mtu ambaye ameshawahi kupatwa na tatizo la kizungu Zungu au hajawahi kupata dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi, ni faida ambazo upatikana kwa watu wanaodhani wameambukizwa na virus vya ukimwi na kuweza kujikinga.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari
Soma Zaidi...Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Uvimbe au mashambulizi ya bacteria kwenye utando laini uliopo tumboni ambao kitaalamu hujulikana Kama peritonitis.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto
Soma Zaidi...Posti inahusu huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu.huduma ya kwanza Ni kumsaidia mtu alie pata jeraha au ajali kabla hajamwona dactari au kufika hospitalinia.
Soma Zaidi...