picha

Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona

Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi saba na nane.

1.sababu ya kwanza ni kuwepo kwa presha.

Kuna kipindi akina mama wanakuwa na presha wakati wakiwa na mimba hali inayosababisha kuzaliwa kwa watoto ndebile kwa hiyo akina mama wanapaswa kupima presha wakati wakiwa na mimba tangia mwanzoni ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa presha wakati wa ujauzito.

 

2. Mtoto kukosa maji akiwa tumboni.

Kwa kawaida mtoto akiwa tumboni huwa na maji yake ambayo kwa kawaida maji hayo huitwa amniotic fluid ambapo maji hayo umsaidia mtoto kufanya vitu mbalimbali akiwa tumboni kwa hiyo kuna kipindi maji hayo  upungua au kuisha  kwa sababu mbalimbali na kupelekea mtoto kuzaliwa ndebile.

 

3. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mji wa mimba.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na Maambukizi mbalimbali kwenye mji wa mimba ambayo Usababisha mimba kutoka.

 

4. Kuwepo kwa kisukari wakati wa ujauzito.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kisukari wakati wa ujauzito ambacho usababisha matatizo mbalimbali kwa mtoto na kusababisha mimba kutoka au kuzaliwa kwa mtoto ndebile.

 

5. Kuwepo kwa kifafa cha mimba.

Hali hii uwapata sana akina mama wengi wenye presha wakati wa mimba na kufuatia degedege wakati wa mimba hali hii ikizidi usababisha mama kujifungua mtoto ndebile.

 

6. Mfuko wa uzazi kuwa dhaifu na kushindwa kubeba mtoto.

Kuna wakati mwingine mfuko wa uzazi unakuwa dhaifu na kusababisha kushindwa kubeba mtoto akiwa tumboni hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile.

 

7. Kulegea kwa mlango wa kizazi kabla ya wakati.

Kuna kipindi mlango wa kizazi unalegea kabisa kabisa kabla ya wakati hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile kwa sababu mlango wa kizazi ukifungukaa na umpatia  mtoto kupita kwa urahisi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 10215

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 ai web app     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Huduma kwa wanaotoa damu yenye mabonge

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?

Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?

Soma Zaidi...
Nini husababisha upungufu wa nguvu za kiume

Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Sababu za mbegu za kiume kuwa dhaifu

Posti hii inahusu zaidi sababu za mbegu za kiume kuwa dhaifu, hali hii uwatokea wanaume wengi kwa sababu mbalimbali za kimaisha ambazo ufanya mbegu za kiume kuwa dhaifu na kusababisha madhara makubwa zaidi kwa sababu wanaume wengi ushindwa kujiamini kwa h

Soma Zaidi...
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito

Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Posti hii inaelezea kiufupi kabisa kuhusiana na Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Soma Zaidi...