Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona
1.sababu ya kwanza ni kuwepo kwa presha.
Kuna kipindi akina mama wanakuwa na presha wakati wakiwa na mimba hali inayosababisha kuzaliwa kwa watoto ndebile kwa hiyo akina mama wanapaswa kupima presha wakati wakiwa na mimba tangia mwanzoni ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa presha wakati wa ujauzito.
2. Mtoto kukosa maji akiwa tumboni.
Kwa kawaida mtoto akiwa tumboni huwa na maji yake ambayo kwa kawaida maji hayo huitwa amniotic fluid ambapo maji hayo umsaidia mtoto kufanya vitu mbalimbali akiwa tumboni kwa hiyo kuna kipindi maji hayo upungua au kuisha kwa sababu mbalimbali na kupelekea mtoto kuzaliwa ndebile.
3. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mji wa mimba.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na Maambukizi mbalimbali kwenye mji wa mimba ambayo Usababisha mimba kutoka.
4. Kuwepo kwa kisukari wakati wa ujauzito.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kisukari wakati wa ujauzito ambacho usababisha matatizo mbalimbali kwa mtoto na kusababisha mimba kutoka au kuzaliwa kwa mtoto ndebile.
5. Kuwepo kwa kifafa cha mimba.
Hali hii uwapata sana akina mama wengi wenye presha wakati wa mimba na kufuatia degedege wakati wa mimba hali hii ikizidi usababisha mama kujifungua mtoto ndebile.
6. Mfuko wa uzazi kuwa dhaifu na kushindwa kubeba mtoto.
Kuna wakati mwingine mfuko wa uzazi unakuwa dhaifu na kusababisha kushindwa kubeba mtoto akiwa tumboni hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile.
7. Kulegea kwa mlango wa kizazi kabla ya wakati.
Kuna kipindi mlango wa kizazi unalegea kabisa kabisa kabla ya wakati hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile kwa sababu mlango wa kizazi ukifungukaa na umpatia mtoto kupita kwa urahisi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 6910
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Madrasa kiganjani
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa Soma Zaidi...
Dalili 10 za kukaribia kujifungua pamoja na uchungu wa kujifungua
Download Kitabu cha elimu ya Ujauzito na malezi ya mimba. Soma Zaidi...
Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake
Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu. Soma Zaidi...
Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.
posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot Soma Zaidi...
Siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba Soma Zaidi...
Dalili za kuharibika kwa mimba
Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka. Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo. Soma Zaidi...
Mabadiliko ya ngozi wakati wa ujauzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye ngozi wakati wa ujauzito, ni mabadiliko yanayotokea kwenye ngozi ya Mama wakati wa ujauzito. Soma Zaidi...
Chanzo cha tatizo la mvurugiko wa hedhi.
Posti hii inahusu zaidi chanzo cha mvurugiko wa hedhi, Kuna kipindi hedhi uvurugika kabisa, pengine unaweza kupata hedhi mara mbili kwa mwezi au kukosa au pengine siku kuwa zaidi ya tano mpaka Saba au kuwa chache, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali tut Soma Zaidi...