Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona
1.sababu ya kwanza ni kuwepo kwa presha.
Kuna kipindi akina mama wanakuwa na presha wakati wakiwa na mimba hali inayosababisha kuzaliwa kwa watoto ndebile kwa hiyo akina mama wanapaswa kupima presha wakati wakiwa na mimba tangia mwanzoni ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa presha wakati wa ujauzito.
2. Mtoto kukosa maji akiwa tumboni.
Kwa kawaida mtoto akiwa tumboni huwa na maji yake ambayo kwa kawaida maji hayo huitwa amniotic fluid ambapo maji hayo umsaidia mtoto kufanya vitu mbalimbali akiwa tumboni kwa hiyo kuna kipindi maji hayo upungua au kuisha kwa sababu mbalimbali na kupelekea mtoto kuzaliwa ndebile.
3. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mji wa mimba.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na Maambukizi mbalimbali kwenye mji wa mimba ambayo Usababisha mimba kutoka.
4. Kuwepo kwa kisukari wakati wa ujauzito.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kisukari wakati wa ujauzito ambacho usababisha matatizo mbalimbali kwa mtoto na kusababisha mimba kutoka au kuzaliwa kwa mtoto ndebile.
5. Kuwepo kwa kifafa cha mimba.
Hali hii uwapata sana akina mama wengi wenye presha wakati wa mimba na kufuatia degedege wakati wa mimba hali hii ikizidi usababisha mama kujifungua mtoto ndebile.
6. Mfuko wa uzazi kuwa dhaifu na kushindwa kubeba mtoto.
Kuna wakati mwingine mfuko wa uzazi unakuwa dhaifu na kusababisha kushindwa kubeba mtoto akiwa tumboni hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile.
7. Kulegea kwa mlango wa kizazi kabla ya wakati.
Kuna kipindi mlango wa kizazi unalegea kabisa kabisa kabla ya wakati hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile kwa sababu mlango wa kizazi ukifungukaa na umpatia mtoto kupita kwa urahisi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.
Soma Zaidi...Unaweza kutaka kujuwa je naweza kupata dalili za mimba baada ya siku nne toka ujauzito kutungwa? ama baada ya siku nne toka kushiriki tendo la ndoa. Makala hii itakwenda kujibu maswali haya na mengineyo.
Soma Zaidi...Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kutibu mbegu dhaifu, ni njia ambazo utumika kutibu mbegu ambazo ni dhaifu ili kuweza kuondoa tatizo hili ambalo limewakumba wanaume wengi na kusababisha madhara makubwa kwenye ndoa au familia.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...