picha

Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona

Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi saba na nane.

1.sababu ya kwanza ni kuwepo kwa presha.

Kuna kipindi akina mama wanakuwa na presha wakati wakiwa na mimba hali inayosababisha kuzaliwa kwa watoto ndebile kwa hiyo akina mama wanapaswa kupima presha wakati wakiwa na mimba tangia mwanzoni ili kuweza kuepuka tatizo la kuwepo kwa presha wakati wa ujauzito.

 

2. Mtoto kukosa maji akiwa tumboni.

Kwa kawaida mtoto akiwa tumboni huwa na maji yake ambayo kwa kawaida maji hayo huitwa amniotic fluid ambapo maji hayo umsaidia mtoto kufanya vitu mbalimbali akiwa tumboni kwa hiyo kuna kipindi maji hayo  upungua au kuisha  kwa sababu mbalimbali na kupelekea mtoto kuzaliwa ndebile.

 

3. Kuwepo kwa Maambukizi kwenye mji wa mimba.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na Maambukizi mbalimbali kwenye mji wa mimba ambayo Usababisha mimba kutoka.

 

4. Kuwepo kwa kisukari wakati wa ujauzito.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kisukari wakati wa ujauzito ambacho usababisha matatizo mbalimbali kwa mtoto na kusababisha mimba kutoka au kuzaliwa kwa mtoto ndebile.

 

5. Kuwepo kwa kifafa cha mimba.

Hali hii uwapata sana akina mama wengi wenye presha wakati wa mimba na kufuatia degedege wakati wa mimba hali hii ikizidi usababisha mama kujifungua mtoto ndebile.

 

6. Mfuko wa uzazi kuwa dhaifu na kushindwa kubeba mtoto.

Kuna wakati mwingine mfuko wa uzazi unakuwa dhaifu na kusababisha kushindwa kubeba mtoto akiwa tumboni hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile.

 

7. Kulegea kwa mlango wa kizazi kabla ya wakati.

Kuna kipindi mlango wa kizazi unalegea kabisa kabisa kabla ya wakati hali inayosababisha kuzaliwa kwa mtoto ndebile kwa sababu mlango wa kizazi ukifungukaa na umpatia  mtoto kupita kwa urahisi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/07/21/Thursday - 10:25:42 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 9027

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 ai web app    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Faida za uzazi wa mpango kwa jamii

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii.

Soma Zaidi...
Mimi Nina tatizo kila nkishika mimba huwa zinatoka tu ni mara 5 Sasa nifanyaje?

Mimba inaweza kutoka kutokana na maradhi, majeraha ama misukosuko mimgine. Kutoka kwa mimva haimaanishi ndio mwisho wa kizazi.

Soma Zaidi...
Sababu za kupata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.

Soma Zaidi...
maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba

Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi?

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa

Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye

Soma Zaidi...
Changamoto kubwa za tendo la ndoa kwa wanaume

Posti hii inahusu zaidi changamoto ya tendo la ndoa kwa wanaume,wanaume wamekuwa wakipata changamoto ya tendo la ndoa na kuwafanya kushindwa kujiamini na kukosa kabisa raha kwenye maisha yao

Soma Zaidi...
Nini husababisha korodani moja kuwa kubwa kuliko nyingine

kama pumbu moja ni kubwa uliko jingine post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakwend akuangalia vinavyoweza kusababisha korodani moja kuw akubwa zaidi ya lingine

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Soma Zaidi...