Nitakujiza dawa ya chango na maumivu ya tumbo lahedhi, dalili zake na njia za kukabiliana na maumivu ya tumbo la chango.
Dawa ya chango na dawa maumivu ya tumbo la hedhi.
Ni hali ya kawaida kwa mwanmke kupatwa na maumivu akikaribia hedhi ama anapokuwa kwenye hedhi. Hali hii haihitaji hata uangalizi wa daktari. Maumivu haya yanaweza kutofautiana kulingana na umri na maumbile. Kwa wanaoanza sasa wanaweza kupatwa na maumivu makali hata kuliko ambao ni wakubwa. Ambao wana matatizo ya homoni mau,ivu yanaweza kuw ani makali pia. Ukali hii ni wenye kuvumilika, lakini inatokea baadhi ya nyakati kwa baadhi ya wanawake maumivu hayawezi kuvumilika ni makali sana, mpaka anapelekwa hospitali.
Basi makala hii ni kwa ajili yako, tutaona sababu za maumivu haya makali yasiyoweza kuvumilika na pia tatuaona dawa za chango na maumivi ya tumbo la hedhi. Usichoke endelea nayo makala hii mpaka mwisho. Ukipenda tuwachie maoni yako hapo chini.
Ni zipio sababu za maumivu makali ya chango na tumbo la hedhi?
1.Kuota kwa vinyama maeneo mengine ndani ya mwili lakini nje ya tumbo la mimba. Hali hii inaweza kuwa na dalili kama kupata hedhi yenye damu nyingi sana na za mabonge, hedhi kuwa zaidi ya siku 7, maumivu makali ya tumb, maumivu makali wajati wa kushiriki tendo la ndoa.
2.Kama mfumo wa homoni haupo sawa yaani hormone imbalance. Tatizo la homoni ni sugu sana kwa wanawake wengi. Inakadiriwa kuwa katika kila wanawake 10 basi mmoja wao atakuwa na tatizo hili. Shida ya homoni inaweza kuwa na dalili kama:- maumivu makali ya chango, kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, kutokwa na chunusi nyingi usoni, mwanamke kuwa mzito sana, nywele zake zinakuwa dhaifa na kunyonyoka kwa haraka, na ngozi kuwa na madod madoa.
3.Kuwa na uvimbe kwenye mfumo wa uzazi. Mwnamke anaweza kuwa na dalili kama maummivu ya miguu, maumivu ya mgongo kwa chhini, kukosa choo kikubwa, kupata hedhio yenye damu nyingi, maumivu mkakli ya chango, kukojoa mara kwa mara na kushindwa kumaliza mkojo wote anapokojoa.
4.Kuwa na maambukizi au mashambulizi ya bakteria, fangasi na virusi kwenye mfumo wa uzazi. Mwanamke anaweza kupatwa na dalili kama kutokwa na damu kablya ya kuinia hedhi na baada, kutokwa na majimaji yanayotoa harufu ukeni, maumivu makali wakati wa kukojoa, kupata homa.
Sababu nyingine ni:
1.Kukaza kwa tisu za kwenye tumbo la kizazi
2.Matumizi ya baadhi ya njia za uzazi wa mpango
3.Maumbile ya mwanamke.
Dawa ya chango na dawa maumivu ya tumbo la hedhi.
A.Ibuprofen (Advil, Motrin IB)
B.Naproxen sodium (Aleve na Anaprox)
C.Ketoprofen (Actron na Orudis KT)
D.Mefenamic acid
Namna ya kukabiliana na tumbo la chango na maumivu ya tumbo la hedhi
1.Fanya mazoezi ya mrakwa mara
2.Hakikisha huna misongo ya mawazo
3.Punguza kula vyakula vyenye chumvi sana pia punguza kula vitu vya sukari sana
4.Punguza unywaji wa chai ya majani ya chai (caffein)
5.Punguza vyakula vyenye mafuta ya wanyama kwa wingi kama nyama.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba tu mimba, Mama anapobeba mimba Kuna mabadiliko Katika uke wa Mama kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o
Soma Zaidi...Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.
Soma Zaidi...Post yetu imebeba mada inayohusiana na wanaume wanaowashwa Uume embu tuone dalili zinazopelekea kuwashwa kwa penis. Uume(penis) ni party ya mwanaume ya sehemu za siri.pia wanaume ambao hawajatahiriwa(unsircumside) kwasababu Ile ngozi ya juu husababishwa k
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kujiepusha na maradhi ya ini
Soma Zaidi...Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14
Soma Zaidi...