Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.
Zifuatazo Ni Dalili za Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID.
Mwanamke atakundulika kuwa na PID Kama akiwa na Dalili zifuatazo;
1.maumivu makali ya tumbo hasa chini ya kitovu. Kutokana na Maambukizi yaliyoenda kuathiri via vya Uzazi .
2.kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu ya rangi ya maziwa mgando. Uchafu huu hutokana na bacteria ambao hushambulia sehemu za shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi na ndio maana hupelekea kutoa uchafu.
3.kupata homa za Mara kwa Mara. Kwasababu ya Maambukizi hayo yaliyoenda kuathiri kwenye Uzazi wa mwanamke pamoja na maumivu hupelekea kupata homa za Mara kwa mara.
4.kupata Hali ya kichefuchefu au kutapika. Hii Ni kwasababu mwanamke anaweza kukosa hedhi au hedhi kujirudia kwa mwezi pamoja na uchafu unayotengenezwa na hao bacteria hupelekea kupata kichefuchefu au kutapika.
5.kupata maumivu wakati wa kukojoa. Maambukizi haya hufanya sehemu hizo kuwa na michubuko hivyo husababisha mtu akikojoa kupata maumivu.
6.kutokwa na Damu wakati wa kujamiina. Damu hizi hutoka pia kwa sababu ya michubuko iliyotokea Ndani na ndio maana akijamiina anaweza Kutokwa na Damu.
7.kupata maumivu ya mgongo. Ni kwasababu ya Maambukizi yanayoathiri via vya Uzazi Kama shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi ndio hupelekea kupata maumivu ya mgongo.
8.kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa au kujamiina.hii pia Ni kwasababu ya michubuko iliyotokea Ndani na iliyosababisha na Mashambulizi ya bacteria hao.
9.wakati mwingine Kutokwa na usaha ukeni. Uchafu ukizid na Hali hii hupelekea kutoa usaha kwa sababu ya kukosa matibabu na kukaa na Ugonjwa huu kwa muda mrefu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 web hosting 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Je mwanamke anaweza kujijuwa ni mjamzito baada ya muda gani.
Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Soma Zaidi...Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...Jinsi ya kupata mtoto wa kiume
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.
Soma Zaidi...Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa
Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.
Soma Zaidi...Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...