picha

Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.

Zifuatazo Ni Dalili za Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID.

Mwanamke atakundulika kuwa na PID Kama akiwa na Dalili zifuatazo;

1.maumivu makali ya tumbo hasa chini ya kitovu. Kutokana na Maambukizi yaliyoenda kuathiri via vya Uzazi .

 

2.kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu ya rangi ya maziwa mgando. Uchafu huu hutokana na bacteria ambao hushambulia sehemu za shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi na ndio maana hupelekea kutoa uchafu.

 

3.kupata homa za Mara kwa Mara. Kwasababu ya Maambukizi hayo yaliyoenda kuathiri kwenye Uzazi wa mwanamke pamoja na maumivu hupelekea kupata homa za Mara kwa mara.

 

4.kupata Hali ya kichefuchefu au kutapika. Hii Ni kwasababu mwanamke anaweza kukosa hedhi au hedhi kujirudia kwa mwezi pamoja na uchafu unayotengenezwa na hao bacteria hupelekea kupata kichefuchefu au kutapika.

 

5.kupata maumivu wakati wa kukojoa. Maambukizi haya hufanya sehemu hizo kuwa na michubuko hivyo husababisha mtu akikojoa kupata maumivu.

 

6.kutokwa na Damu wakati wa kujamiina. Damu hizi hutoka pia kwa sababu ya michubuko iliyotokea Ndani na ndio maana akijamiina anaweza Kutokwa na Damu.

 

7.kupata maumivu ya mgongo. Ni kwasababu ya Maambukizi yanayoathiri via vya Uzazi Kama shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi ndio hupelekea kupata maumivu ya mgongo.

 

8.kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa au kujamiina.hii pia Ni kwasababu ya michubuko iliyotokea Ndani na iliyosababisha na Mashambulizi ya bacteria hao.

 

9.wakati mwingine Kutokwa na usaha ukeni. Uchafu ukizid na Hali hii hupelekea kutoa usaha kwa sababu ya kukosa matibabu na kukaa na Ugonjwa huu kwa muda mrefu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2050

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 ai web app     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Huduma kwa wasioona hedhi

Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.

Soma Zaidi...
Siku za kupata mimba

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba

Soma Zaidi...
je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini?

Je kutokwa na maji ukeni ambayo hayana harufu na meupe Hadi kuroanisha chupi, na je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini?

Soma Zaidi...
Mabaka yanayowasha chini ya matiti.

Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mwanamke kukosa tendo la ndoa, ni sababu ambazo uwakuta wanawake wengi unakuta mama yuko kwenye ndoa ila hana hata hamu ya lile tendo la ndoa hali ambayo umfanya mwanamke kuona kitendo cha tendo la ndoa ni unyanyasaji au

Soma Zaidi...
Sababu za kutoona hedhi kwa wakati

Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...