Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.
Zifuatazo Ni Dalili za Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID.
Mwanamke atakundulika kuwa na PID Kama akiwa na Dalili zifuatazo;
1.maumivu makali ya tumbo hasa chini ya kitovu. Kutokana na Maambukizi yaliyoenda kuathiri via vya Uzazi .
2.kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu ya rangi ya maziwa mgando. Uchafu huu hutokana na bacteria ambao hushambulia sehemu za shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi na ndio maana hupelekea kutoa uchafu.
3.kupata homa za Mara kwa Mara. Kwasababu ya Maambukizi hayo yaliyoenda kuathiri kwenye Uzazi wa mwanamke pamoja na maumivu hupelekea kupata homa za Mara kwa mara.
4.kupata Hali ya kichefuchefu au kutapika. Hii Ni kwasababu mwanamke anaweza kukosa hedhi au hedhi kujirudia kwa mwezi pamoja na uchafu unayotengenezwa na hao bacteria hupelekea kupata kichefuchefu au kutapika.
5.kupata maumivu wakati wa kukojoa. Maambukizi haya hufanya sehemu hizo kuwa na michubuko hivyo husababisha mtu akikojoa kupata maumivu.
6.kutokwa na Damu wakati wa kujamiina. Damu hizi hutoka pia kwa sababu ya michubuko iliyotokea Ndani na ndio maana akijamiina anaweza Kutokwa na Damu.
7.kupata maumivu ya mgongo. Ni kwasababu ya Maambukizi yanayoathiri via vya Uzazi Kama shingo ya uzazi, nyuma ya mfuko wa Uzazi, na mirija ya uzazi ndio hupelekea kupata maumivu ya mgongo.
8.kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa au kujamiina.hii pia Ni kwasababu ya michubuko iliyotokea Ndani na iliyosababisha na Mashambulizi ya bacteria hao.
9.wakati mwingine Kutokwa na usaha ukeni. Uchafu ukizid na Hali hii hupelekea kutoa usaha kwa sababu ya kukosa matibabu na kukaa na Ugonjwa huu kwa muda mrefu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Sababu za wajawazito kupata Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.
Soma Zaidi...Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Madhara ya kutumia vidonge kwa akina dada vya uzazi wa mpango
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia vidonge vya uzazi wa mpango kwa akina dada.
Soma Zaidi...Dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Soma Zaidi...