Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii
Kutoka kwa ujauzito mara nyimgi hutokea katika hiki kipindi cha kwanza yaani ndani ya wiki 12 za mwanzo. Inakadiriwa kuwa robo ya mimba hutoka. Mwanamke anaweza akatokwa na mimba kwa kujuwa ana bila ya kujuwa. Inaweza kutokea pia mwanamke akabeba ujauzito na ukatoka bila kuwa na habari yeyote kama alikuwa na miba na imetoka. Ni kuwa mimba inaweza kutoka bila ya kuwa na dalili za wazi kama kutoka na damu.
Dalili za kutoka kwa mimba:
A.Maumivu ya mgongo
B.Kuharisha
C.Kichefuchefu
D.Maumivu ya maeneo ya nyonga na kiuno kama unahisi unataka kuingia kwenye siku zako
E.Maumivu makali ya tumbo
F.Kutokwa na majimaji kwenye uke.
G.Kutokwa na vitu kama vijioande vya nyama vijidogo kwenye uke
H.Uchovu mkali sana usio na sababu
I.Kupotea kwa dalili nyingine za ujauzito
J.Kutokwa na damu mabonge manonge ama damu nyingi
Kumbuka hizi ni dalili tu, unaweza kuwa nazo na ujauzito ukawa salama kabisa. Ukiona unahisi dalili hizo muone daktari atathibitisha vyema kwa vipimo ikiwemo utrasound ama kuangalia kiwango cha homoni ya ujjauzito kwneye damu yako.
Ni zipi sababu za kutoka kwa mimba?
Mara nyingi kutoka kwa ujauzito kunaweza kusababishwa na chromosomal abnormalities. Hili ni tatizo la kigenetics. Hapa seli za mtoto zinashindwa kugawanyika vyema na kukuza mtoto. Sababu nyingine za kutoka ujauzito ni:-
A.Matatizo katika homoni kuwa nyingi sana ama kidogo sana
B.Kama mama mjamzito ana kisukari na hafuati masharti vyema
C.Mazingira yanaweza kuchangia kama kuna mionzi hatari kama ya madini ya uranium
D.Maambukizi na mashambulizi ya vijidudu kama bakteria kwenye via vya uzazi.
E.Shida katika mlango wa uzazi (cevix)
F.Kutumia madawa kiholela ama kutumia madawa kusudi kwa lengo la kutoa ujauzito
G.Ugonjwa wa endometriosis (kuvimba kwa kuta za mji wa mimba βuterusβ)
H.Magonjwa ya ngono kama gonoria
Sababu nyingine za kutoka kwa mimba
A.Utapia mlo
B.Kuwa na kitambi
C.Matumizi ya vilevi na sigara
D.Maradhi ya tezi ya thyroid
E.Shinikizo la damu la juu sana
NITAZUIAJE MIMBA KUTOKA?
Mimba nyingi zinazotoka husababishwa na genetics ama mambo ya kiafya ambayo si rahisi kuzuilika. Hivyo kwa mimba hizi ni ngumu sana kuzuia kutoka kwake. Hata hivypo kitu ambacho unaweza kukifanya ni kuhakikisha kuwa unabakia katika afya salama kabla na baada ya kubeba ujauzito. Fafya mabo yafuatayo yatasaidia katika kuboresha afya yako na kuzuia kiutoka kwa ujauzito:-
A.Kula mlo kamili wenye virutubisho (balanced diet)
B.Fanya mazoezi mara kwa mara. Si lazima eti mazoezi ya kukutoa mijasho, unaweza kufanya mazoezi ya viungo pia hata ukiwa kitandani.
C.Wacha ama punguza kutumia pombe, sigara ama dawa za kulevya.
D.Punguza unywaji wa chai kama unakunywa kwa wingi kupitiliza. Hapa ninazungumzia chai ya majani ya chai ambayo ina caffein.
E.Fanya uchunguzi wa afya yako mara kwa mara.
F.Wacha kutumia dawa kiholela
G.Jiepushe na mambo ambayo yataweza kuwa ni hatari kwa ujauzito kama kupigana ama miereka.
H.Fuata maelekezo vyema kutoka kwa wahudumu wa afya.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.
Soma Zaidi...Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.
Soma Zaidi...Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoabkunaweza kuashiria kuwa kuna majeraha yametokea huwenda ni michubuko ilitokea ndio ikavujisha damu. Lakini kwa nini hali kama hii itokee. Posti hii itakwwnda mujibu swali hili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.
Soma Zaidi...