Menu



Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka



KUTOKA KWA UJAUZITO, DALILI ZAKE NA SABABU ZAKE.




Kutoka kwa ujauzito mara nyimgi hutokea katika hiki kipindi cha kwanza yaani ndani ya wiki 12 za mwanzo. Inakadiriwa kuwa robo ya mimba hutoka. Mwanamke anaweza akatokwa na mimba kwa kujuwa ana bila ya kujuwa. Inaweza kutokea pia mwanamke akabeba ujauzito na ukatoka bila kuwa na habari yeyote kama alikuwa na miba na imetoka. Ni kuwa mimba inaweza kutoka bila ya kuwa na dalili za wazi kama kutoka na damu.



Dalili za kutoka kwa mimba:
A.Maumivu ya mgongo
B.Kuharisha
C.Kichefuchefu
D.Maumivu ya maeneo ya nyonga na kiuno kama unahisi unataka kuingia kwenye siku zako
E.Maumivu makali ya tumbo
F.Kutokwa na majimaji kwenye uke.
G.Kutokwa na vitu kama vijioande vya nyama vijidogo kwenye uke
H.Uchovu mkali sana usio na sababu
I.Kupotea kwa dalili nyingine za ujauzito
J.Kutokwa na damu mabonge manonge ama damu nyingi



Kumbuka hizi ni dalili tu, unaweza kuwa nazo na ujauzito ukawa salama kabisa. Ukiona unahisi dalili hizo muone daktari atathibitisha vyema kwa vipimo ikiwemo utrasound ama kuangalia kiwango cha homoni ya ujjauzito kwneye damu yako.



Ni zipi sababu za kutoka kwa mimba?
Mara nyingi kutoka kwa ujauzito kunaweza kusababishwa na chromosomal abnormalities. Hili ni tatizo la kigenetics. Hapa seli za mtoto zinashindwa kugawanyika vyema na kukuza mtoto. Sababu nyingine za kutoka ujauzito ni:-
A.Matatizo katika homoni kuwa nyingi sana ama kidogo sana
B.Kama mama mjamzito ana kisukari na hafuati masharti vyema
C.Mazingira yanaweza kuchangia kama kuna mionzi hatari kama ya madini ya uranium
D.Maambukizi na mashambulizi ya vijidudu kama bakteria kwenye via vya uzazi.
E.Shida katika mlango wa uzazi (cevix)
F.Kutumia madawa kiholela ama kutumia madawa kusudi kwa lengo la kutoa ujauzito
G.Ugonjwa wa endometriosis (kuvimba kwa kuta za mji wa mimba β€œuterus”)
H.Magonjwa ya ngono kama gonoria



Sababu nyingine za kutoka kwa mimba
A.Utapia mlo
B.Kuwa na kitambi
C.Matumizi ya vilevi na sigara
D.Maradhi ya tezi ya thyroid
E.Shinikizo la damu la juu sana




NITAZUIAJE MIMBA KUTOKA?
Mimba nyingi zinazotoka husababishwa na genetics ama mambo ya kiafya ambayo si rahisi kuzuilika. Hivyo kwa mimba hizi ni ngumu sana kuzuia kutoka kwake. Hata hivypo kitu ambacho unaweza kukifanya ni kuhakikisha kuwa unabakia katika afya salama kabla na baada ya kubeba ujauzito. Fafya mabo yafuatayo yatasaidia katika kuboresha afya yako na kuzuia kiutoka kwa ujauzito:-



A.Kula mlo kamili wenye virutubisho (balanced diet)
B.Fanya mazoezi mara kwa mara. Si lazima eti mazoezi ya kukutoa mijasho, unaweza kufanya mazoezi ya viungo pia hata ukiwa kitandani.
C.Wacha ama punguza kutumia pombe, sigara ama dawa za kulevya.
D.Punguza unywaji wa chai kama unakunywa kwa wingi kupitiliza. Hapa ninazungumzia chai ya majani ya chai ambayo ina caffein.
E.Fanya uchunguzi wa afya yako mara kwa mara.
F.Wacha kutumia dawa kiholela
G.Jiepushe na mambo ambayo yataweza kuwa ni hatari kwa ujauzito kama kupigana ama miereka.
H.Fuata maelekezo vyema kutoka kwa wahudumu wa afya.



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1190

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Umuhimu wa kunyonyesha mtoto

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka

Soma Zaidi...
Ni ili sababu ya kutokea kwa tezi dume

Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.

Soma Zaidi...
Uzazi wa mpango

Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUITAMBUA SIKU HATARI YA KUPATA MIMBA (UJAUZITO)

SIKU YA KUPATA UJAUZITO Mimba hutokea pindi mbegu ya kiume (sperm) inapokutana na yai la mwanamke (ova) na kuungana kwa pamoja kutengeneza selli moja iitwayo zygote.

Soma Zaidi...
Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.

Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada

Soma Zaidi...
Napenda kuuliza mke wangu anamuda wa wiki moja . tumbo na maziwa vinauma je dalili hizo zinawekuwa ni ujauzito...?

Maumivu ya tumbo kwa mjamzito huweza kuanaa kuonekana mwanzoni kabisa mwaujauzito, ndani ya mwezi mmoja. Ikabidi si dalili pekee ya kuwa ni mjamzito.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

Njoo ujifunze vyakula vya kuboresha mbegu za kiume na nguvu za kiume.

Soma Zaidi...