Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Tofauti kati ya Qur’an na Vitabu vingine vya Mwenyezi Mungu (s.w).
|
Kitabu cha Qur’an |
Vitabu Vingine vya Mwenyezi Mungu |
|
1. Neno la Asili. Qur’an imebakia katika lugha yake ya asili ya kiarabu fasaha pamoja nakutafsiriwa katika lugha tofauti. |
Vitabu vingine lugha zao za asili zilizoshushiwa zimepotea na kutojulikana. |
|
2. Lugha zilizoshushiwa Vitabu. Lugha ya Qur’an ni hai kwani mpaka leo inatumika na kufahamika na walimwengu wengi. |
Lugha za vitabu vilivyotangulia ni mfu, zimefutika zamani na hazijulikani na watu. Rejea Qur’an (14:4). |
|
3. Kuhifadhiwa na Kulindwa Vitabu. Qur’an imebaki katika asili yake kama ilivyoteremsha bila kubadilishwa chochote na wanaadamu ndani yake. Rejea Qur’an (15:9) na (41:42) |
Vitabu vingine vimepotea katika asili yake kwa kupunguzwa, kuongezwa na kupotoshwa asili ya ujumbe wake na mikono ya wanaadamu.. |
|
4. Hitoria ya Kushushwa Vitabu. Historia ya kushushwa Qur’an inajulikana vyema mfano; namna, sehemu, muda/kipindi na sababu ya kuteremshwa kila aya. |
Vitabu vingine historia ya kushushwa kwao haijulikani, mfano; muda, nama, sababu au sehemu. |
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 web hosting 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?
Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.
Soma Zaidi...(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.
Soma Zaidi...Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu
Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...