Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir



Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu. Na kama mkipigwa vita lazima tutakusaidieni." Na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa wao ni waongo. Kama wakifukuzwa hawatatoka pamoja nao, na kama wakipigwa hawatawasaidia; na kama wakiwasaidia kwa yakini watageuza migongo (wende mbio); kisha hawatanusuriwa. (59:11-1 2)


Hakika nyinyi (Waislamu) mnaogopwa zaidi katika nyoyo zao kuliko wanavyomuogopa Mwenyezi Mungu; maana wao ni watu wasiofahamu (lolote). (59:13)



Hawatapigana nanyi kwa mkusanyiko isipokuwa katika vijiji vyao vilivyohifadhiwa, au nyuma ya kuta. Vita vyao baina yao vikubwa. Utawadhani kuwa wako pamoja; kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni kwa sababu wao ni watu wasio na akili. Hali yao (hawa Mayahudi wa Kibanu Nadir) ni kama ya wale (Mayahudi wa Bani Qaynuqai) waliowatangulia (kufikwa na baa) hivi karibuni; walionja ubaya wa mambo yao; na watapata adhabu (nyingine) iumizayo (vile vile). Ni kama Shetani anapomwambia mtu: "Kufuru;" na anapokufuru akamwambia: "Mimi si pamoja nawe, hakika namuogopa Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu. "(59:14-16)


Basi mwisho wa wote wawili hao ukawa waingie Motoni kukaa humo daima; na hiyo ndiyo jaza ya madhalimu. (59:17)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i)Hushirikiana na kusaidiana na makafiri katika kuuhujumu Uislamu na Waislamu.
(ii)Wanawaogopa watu kuliko wanavyo muogopa Allah (s.w)
(iii)Wanaonekana kuwa wamoja lakini kiutendaji kila mmoja yuko na lake. Umoja wao ni kama ule wa inzi, likitupwa jiwe kila mmoja hutawanyika kikwake tofauti na mshikamano ule wa kundi la nyuki ambao wakichozwa hushambulia kwa pamoja mpaka kumkibiza adai




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 838

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...
Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...