Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.
Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu. Na kama mkipigwa vita lazima tutakusaidieni." Na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa wao ni waongo. Kama wakifukuzwa hawatatoka pamoja nao, na kama wakipigwa hawatawasaidia; na kama wakiwasaidia kwa yakini watageuza migongo (wende mbio); kisha hawatanusuriwa. (59:11-1 2)
Hakika nyinyi (Waislamu) mnaogopwa zaidi katika nyoyo zao kuliko wanavyomuogopa Mwenyezi Mungu; maana wao ni watu wasiofahamu (lolote). (59:13)
Hawatapigana nanyi kwa mkusanyiko isipokuwa katika vijiji vyao vilivyohifadhiwa, au nyuma ya kuta. Vita vyao baina yao vikubwa. Utawadhani kuwa wako pamoja; kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni kwa sababu wao ni watu wasio na akili. Hali yao (hawa Mayahudi wa Kibanu Nadir) ni kama ya wale (Mayahudi wa Bani Qaynuqai) waliowatangulia (kufikwa na baa) hivi karibuni; walionja ubaya wa mambo yao; na watapata adhabu (nyingine) iumizayo (vile vile). Ni kama Shetani anapomwambia mtu: "Kufuru;" na anapokufuru akamwambia: "Mimi si pamoja nawe, hakika namuogopa Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu. "(59:14-16)
Basi mwisho wa wote wawili hao ukawa waingie Motoni kukaa humo daima; na hiyo ndiyo jaza ya madhalimu. (59:17)
Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i)Hushirikiana na kusaidiana na makafiri katika kuuhujumu Uislamu na Waislamu.
(ii)Wanawaogopa watu kuliko wanavyo muogopa Allah (s.w)
(iii)Wanaonekana kuwa wamoja lakini kiutendaji kila mmoja yuko na lake. Umoja wao ni kama ule wa inzi, likitupwa jiwe kila mmoja hutawanyika kikwake tofauti na mshikamano ule wa kundi la nyuki ambao wakichozwa hushambulia kwa pamoja mpaka kumkibiza adai
Umeionaje Makala hii.. ?
Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k
Soma Zaidi...(v)Kuwaombea dua wazazi.
Soma Zaidi...Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?
Soma Zaidi...“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).
Soma Zaidi...