picha

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir



Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu. Na kama mkipigwa vita lazima tutakusaidieni." Na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa wao ni waongo. Kama wakifukuzwa hawatatoka pamoja nao, na kama wakipigwa hawatawasaidia; na kama wakiwasaidia kwa yakini watageuza migongo (wende mbio); kisha hawatanusuriwa. (59:11-1 2)


Hakika nyinyi (Waislamu) mnaogopwa zaidi katika nyoyo zao kuliko wanavyomuogopa Mwenyezi Mungu; maana wao ni watu wasiofahamu (lolote). (59:13)



Hawatapigana nanyi kwa mkusanyiko isipokuwa katika vijiji vyao vilivyohifadhiwa, au nyuma ya kuta. Vita vyao baina yao vikubwa. Utawadhani kuwa wako pamoja; kumbe nyoyo zao ni mbali mbali. Hayo ni kwa sababu wao ni watu wasio na akili. Hali yao (hawa Mayahudi wa Kibanu Nadir) ni kama ya wale (Mayahudi wa Bani Qaynuqai) waliowatangulia (kufikwa na baa) hivi karibuni; walionja ubaya wa mambo yao; na watapata adhabu (nyingine) iumizayo (vile vile). Ni kama Shetani anapomwambia mtu: "Kufuru;" na anapokufuru akamwambia: "Mimi si pamoja nawe, hakika namuogopa Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu. "(59:14-16)


Basi mwisho wa wote wawili hao ukawa waingie Motoni kukaa humo daima; na hiyo ndiyo jaza ya madhalimu. (59:17)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i)Hushirikiana na kusaidiana na makafiri katika kuuhujumu Uislamu na Waislamu.
(ii)Wanawaogopa watu kuliko wanavyo muogopa Allah (s.w)
(iii)Wanaonekana kuwa wamoja lakini kiutendaji kila mmoja yuko na lake. Umoja wao ni kama ule wa inzi, likitupwa jiwe kila mmoja hutawanyika kikwake tofauti na mshikamano ule wa kundi la nyuki ambao wakichozwa hushambulia kwa pamoja mpaka kumkibiza adai




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1638

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 web hosting    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu

Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu (EDK form 1: mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu

Soma Zaidi...
Maana ya muislamu.

Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu.

Soma Zaidi...
(c)Vipawa vya Mwanaadamu

Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu katika mtazamo wa Uislamu

Katika Uislamu elimu imegawanyika katika Elimu ya muongozo na elimu ya mazingira.

Soma Zaidi...