Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu)
Mgawanyo wa Elimu usiokubalika katika Uislamu (usio sahihi).
- Katika Uislamu, HAKUNA mgawanyo wa ‘Elimu Dunia’ na ‘Elimu Akhera’.
- Mgawanyo huu ni potofu wenye dhana ya kikafiri kuwa kuna maisha ya Dini yanayoongozwa na Mwenyezi Mungu na maisha ya Dunia yanayoongozwa na binaadamu.
Mgawanyo huu sio sahihi kwa sababu zifuatazo:
1. Nabii Adam (a.s) aliandaliwa yeye na kizazi chake kuwa Makhalifa (viongozi) na alifundishwa majina (fani zote) ya vitu vyote.
Rejea Qur’an (2:31) na (2:38-39).
2.Amri ya kusoma aliyopewa Mtume (s.a.w) na umma wake haibagui elimu ya dini na dunia.
3.Muasisi wa (chanzo cha) elimu na fani zote ni Mwenyezi Mungu (s.w). Hakuna mwanaadamu aliyeasisi elimu au fani yeyote ila ni mwendelezaji tu.
Rejea Qur’an (96:3-5).
4. Pia Qur’an inatufahamisha kuwa wanaomcha Allah (s.w) ipasavyo ni waumini wataalamu waliozama katika fani mbali mbali za kumjua Allah (s.w), sio tu fani za kidini za Fiqh, Tawhiid, n.k.
Rejea Qur’an (35:27-28)
6. Katika Qur’an Allah (s.w) anatufahamisha kuwa waumini wenye elimu ya fani mbali mbali ndio wenye daraja kubwa zaidi mbele yake.
Rejea Qur’an (58:11), (49:13).
7. Hakuna mgawanyo wa elimu unaooneshwa katika Hadith za Mtume (s.a.w) zinazoelezea fani za elimu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.
Soma Zaidi...Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.
Soma Zaidi...Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia.
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...