image

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah


Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Wanatafuta kumdanganya Mwenyezi Mungu na wale walioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao; nao hawatambui. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu iumizayo kwa sababu ya kule kusema kwao uwongo. (2:8-10)


Na wanapoambiwa: "Msifanye uharibifu ulimwenguni." Husema "Sisi ni watengenezaji. "Hakika wao ndio waharibuji, laini hawatambui.Na wanapoambiwa: "Aminini kama walivyoamini watu" Husema"Oh! Tuamini kama walivyoamini wale wapumbavu?" Hakika wao ndio wapumbavu lakini hawajui. (2:11-1 3)



Na wanapokutana na walioamini husema: "Tumeamini"; na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema: "Hakika sisi tu pamoja nanyi, tunawacheza shere tu." Mwenyezi Mungu atawalipa shere yao na kuwawacha katika upotofu wao wakitangatanga ovyo. Hao ndio waliokhiari upotofu kuliko uongofu; lakini biashara yao haikupata faida wala hawakuwa wenye kuongoka. (2:14-1 6)


Mfano wao (hawa wanafiki) ni kama mfano wa wale (wasafiri waliokumbwa na kiza) wakakoka moto, (na) ulipowaonyesha yaliyo pembezoni mwao, Mwenyezi Mungu aliiondoa nuru yao hiyo na kuwawacha katika viza; hawaoni. (2:17)


Viziwi, mabubu, vipofu; kwa hivyo hawatarejea. (2:18)


Au (mfano wao pia) ni kama mvua kubwa itokayo mawinguni; ndani yake mkawa mna viza na radi na umeme; wakawa


wakitia vidole vyao masikioni mwao kwa ajili ya mingurumo, kwa kuogopa kufa; (na kufanya hivyo hawakusaidii kitu). Na Mwenyezi Mungu anawajua vyema hao makafiri. (2:19)


Unakaribia umeme huo kunyakua macho yao; kila unapowaangazia huenda ndani yake na unapowafanyia giza husimama. Na Mwenyezi Mungu angependa angaliondoa kusikia kwao na kuona kwao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kuweza juu ya kila kitu. (2:20)



Kutokana na aya hizi tunajifunza sifa za wanafiki zifuatazo:
(i)Kuonesha imani ya uongo. Katika vinywa vyao wanadai kuwa ni waumini lakini katika nafsi zao na matendo yao wanaikanusha imani yao.
(ii)Wanauchukia Uislamu nyoyoni mwao, na wanazidi kuuchukia kila Uislamu unavyosonga mbele.
(iii)Hufanya uharibifu katika nchi huku wakidai kuwa wanatengeneza.
(iv)Huwabeza waumini wa kweli wanaofuata Uislamu vilivyo.
(v)Hawana msimamo. Wanataka wapate maslahi ya Uislamu na wakati huo huo wawe pamoja na makafiri.
(vi)Wanawacheza shere Waislamu.
(vii)Kwa mujibu wa mfano uliopigwa katika aya ya 17 (2:17) wamekhiyari kupotea baada ya kujiwa na mwongozo (nuru).
(viii)Kwa sababu wamedhamiria upotevu badala ya uongofu kwa ajili ya maslahi ya dunia, hata ukiwaita kwenye uongofu hawawezi kuja. Wamefananishwa na watu wenye vilema vitatu kwa pamoja vya uziwi, ububu na upofu. Hivyo hawawezi kusikia neno la mwenye kuadhini wala la mwenye kukimu.


Kwa mujibu wa mfano uliopigwa katika aya ya 19 na 20 (2:19-20), wanafiki wanatamani matunda yatokanayo na kusimama kwa Uislamu katika jamii lakini hawako tayari kukabiliana na changamoto zinazotokana na mchakato mzima wa kusimamisha Uislamu katika jamii. Wanafurahia matunda yanayotokana na mvua nzuri za masika lakini hawako tayari kukabiliana na radi, ngurumo na umeme vinavyoandamana na mvua hizo.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 494


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kutopupia dunia
"Ewe mwanangu! Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu umeipa Elimu nafasi ya kwanza?
Soma Zaidi...

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat ash-Shuura
“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele). Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao
Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s. Soma Zaidi...

Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6). Soma Zaidi...

Kuamini siku ya mwisho
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

Ni Ipi Elimu yenye manufaa
Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa Soma Zaidi...

Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kwanini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini?
Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu) Soma Zaidi...