Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.w)katika ardhi takatifu. Lakini ubaya wa bahati, Bani Israil walikhini amana hii na kuwa wezi wa fadhila. Hebu turejee Qur'an tuone baadhi ya neema za Allah juu ya Bani Israil na jinsi walivyofanya ukaidi.
"Enyi kizazi cha Israili! Kumbukeni neema zangu nilizokuneemesheni na nikakutukuzeni kuliko viumbe wengine (wakati huo)" (2:47).
Na (kumbukeni) tulipokuokoeni kwa watu wa Firauni waliokupeni adhabu mbaya; wakiwachinja watoto wenu wanaume na kuwawacha hai wanawake; na katika hayo (kuokolewa huko) ilipatikana neema kubwa iliyotoka kwa Mola wenu. Na (kumbukeni) tulipoitenga bahari kwa ajili yenu na tukakuokoeni, na tukawazamisha watu wa Firauni na hali mkitazama" (2:49-50).
Na (kumbukeni habari hii pia): Mliposema: "Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mwenyezi Mungu waziwazi". Yakakunyakueni mauti ghafla na hali mnaona. Kisha tukakufufueni baada ya kufa kwenu, ili mpate kushukuru. Na tukakutilieni kivuli kwa mawingu (mlipokuwa mnakata jangwa kutoka Misri kwenda Palestina) na tukakuteremshieni Manna na Salwa: (Tukakwambieni) "Kuleni katika vitu vizuri hivi tulivyokuruzukuni." Nao hawakutudhulumu sisi (walipokhalifu amri yetu) lakini walikuwa wamejidhulumu nafsi zao." (2:55-57).
Na (kumbukeni khabari hii nayo): Musa aliomba maji kwa ajili ya watu wake, tukasema: "Lipige jiwe kwa fimbo yako" mara zikabubujika humo chem.-chem kumi na mbili; kila kabila likajua mahali pake pa kunywea. (Tutawaambia) kuleni na kunyweni katika riziki ya Mwenyezi Mungu, wala msiasi katika ardhi mkafanya uharibifu. Na (kumbukeni) mliposema: "Ewe Musa! Hatuwezi kusubiri kwa chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi, kama mboga zake na matango yake na ngano yake na adesi zake na vitunguu vyake". Akasema (Mwenyezi Mungu): "Mnabadili vitu duni kwa vile vilivyo bora? Nendeni kwenye mji, huko mtapata mlivyoviomba"; Na ikapigwa juu yao (chapa ya) dhila (unyonge) na umaskini; nawakastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi Mungu na wakiwaua manabii pasipo haki. Basi haya ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupindukia mipaka (ya Mwenyezi Mungu) (2:60-61).
Hizo ni baadhi tu ya aya miongoni mwa aya zibainishazo neema za Allah juu ya Bani Israil na ukaidi wao.
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k
Soma Zaidi...Ukweli ni katika sifa za waumini. Siku zote hakuna hasara katika kusema ukweli. Kinyume chake uongo ni katika madhambi makubwa sana.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.
Soma Zaidi...Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.
Soma Zaidi...Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.
Soma Zaidi...Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri.
Soma Zaidi...Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...