Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil.


Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.w)katika ardhi takatifu. Lakini ubaya wa bahati, Bani Israil walikhini amana hii na kuwa wezi wa fadhila. Hebu turejee Qur'an tuone baadhi ya neema za Allah juu ya Bani Israil na jinsi walivyofanya ukaidi.



"Enyi kizazi cha Israili! Kumbukeni neema zangu nilizokuneemesheni na nikakutukuzeni kuliko viumbe wengine (wakati huo)" (2:47).




Na (kumbukeni) tulipokuokoeni kwa watu wa Firauni waliokupeni adhabu mbaya; wakiwachinja watoto wenu wanaume na kuwawacha hai wanawake; na katika hayo (kuokolewa huko) ilipatikana neema kubwa iliyotoka kwa Mola wenu. Na (kumbukeni) tulipoitenga bahari kwa ajili yenu na tukakuokoeni, na tukawazamisha watu wa Firauni na hali mkitazama" (2:49-50).



Na (kumbukeni habari hii pia): Mliposema: "Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mwenyezi Mungu waziwazi". Yakakunyakueni mauti ghafla na hali mnaona. Kisha tukakufufueni baada ya kufa kwenu, ili mpate kushukuru. Na tukakutilieni kivuli kwa mawingu (mlipokuwa mnakata jangwa kutoka Misri kwenda Palestina) na tukakuteremshieni Manna na Salwa: (Tukakwambieni) "Kuleni katika vitu vizuri hivi tulivyokuruzukuni." Nao hawakutudhulumu sisi (walipokhalifu amri yetu) lakini walikuwa wamejidhulumu nafsi zao." (2:55-57).




Na (kumbukeni khabari hii nayo): Musa aliomba maji kwa ajili ya watu wake, tukasema: "Lipige jiwe kwa fimbo yako" mara zikabubujika humo chem.-chem kumi na mbili; kila kabila likajua mahali pake pa kunywea. (Tutawaambia) kuleni na kunyweni katika riziki ya Mwenyezi Mungu, wala msiasi katika ardhi mkafanya uharibifu. Na (kumbukeni) mliposema: "Ewe Musa! Hatuwezi kusubiri kwa chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi, kama mboga zake na matango yake na ngano yake na adesi zake na vitunguu vyake". Akasema (Mwenyezi Mungu): "Mnabadili vitu duni kwa vile vilivyo bora? Nendeni kwenye mji, huko mtapata mlivyoviomba"; Na ikapigwa juu yao (chapa ya) dhila (unyonge) na umaskini; nawakastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi Mungu na wakiwaua manabii pasipo haki. Basi haya ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupindukia mipaka (ya Mwenyezi Mungu) (2:60-61).



Hizo ni baadhi tu ya aya miongoni mwa aya zibainishazo neema za Allah juu ya Bani Israil na ukaidi wao.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 687

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
Mambo muhimu anayofanyiwa muislamu kabla ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah

Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).

Soma Zaidi...
Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji

Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.

Soma Zaidi...