image

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil.


Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.w)katika ardhi takatifu. Lakini ubaya wa bahati, Bani Israil walikhini amana hii na kuwa wezi wa fadhila. Hebu turejee Qur'an tuone baadhi ya neema za Allah juu ya Bani Israil na jinsi walivyofanya ukaidi.



"Enyi kizazi cha Israili! Kumbukeni neema zangu nilizokuneemesheni na nikakutukuzeni kuliko viumbe wengine (wakati huo)" (2:47).




Na (kumbukeni) tulipokuokoeni kwa watu wa Firauni waliokupeni adhabu mbaya; wakiwachinja watoto wenu wanaume na kuwawacha hai wanawake; na katika hayo (kuokolewa huko) ilipatikana neema kubwa iliyotoka kwa Mola wenu. Na (kumbukeni) tulipoitenga bahari kwa ajili yenu na tukakuokoeni, na tukawazamisha watu wa Firauni na hali mkitazama" (2:49-50).



Na (kumbukeni habari hii pia): Mliposema: "Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mwenyezi Mungu waziwazi". Yakakunyakueni mauti ghafla na hali mnaona. Kisha tukakufufueni baada ya kufa kwenu, ili mpate kushukuru. Na tukakutilieni kivuli kwa mawingu (mlipokuwa mnakata jangwa kutoka Misri kwenda Palestina) na tukakuteremshieni Manna na Salwa: (Tukakwambieni) "Kuleni katika vitu vizuri hivi tulivyokuruzukuni." Nao hawakutudhulumu sisi (walipokhalifu amri yetu) lakini walikuwa wamejidhulumu nafsi zao." (2:55-57).




Na (kumbukeni khabari hii nayo): Musa aliomba maji kwa ajili ya watu wake, tukasema: "Lipige jiwe kwa fimbo yako" mara zikabubujika humo chem.-chem kumi na mbili; kila kabila likajua mahali pake pa kunywea. (Tutawaambia) kuleni na kunyweni katika riziki ya Mwenyezi Mungu, wala msiasi katika ardhi mkafanya uharibifu. Na (kumbukeni) mliposema: "Ewe Musa! Hatuwezi kusubiri kwa chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi, kama mboga zake na matango yake na ngano yake na adesi zake na vitunguu vyake". Akasema (Mwenyezi Mungu): "Mnabadili vitu duni kwa vile vilivyo bora? Nendeni kwenye mji, huko mtapata mlivyoviomba"; Na ikapigwa juu yao (chapa ya) dhila (unyonge) na umaskini; nawakastahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi Mungu na wakiwaua manabii pasipo haki. Basi haya ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupindukia mipaka (ya Mwenyezi Mungu) (2:60-61).



Hizo ni baadhi tu ya aya miongoni mwa aya zibainishazo neema za Allah juu ya Bani Israil na ukaidi wao.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 265


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Maana ya Kuamini Siku ya Mwisho
Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu? Soma Zaidi...

Maana ya muislamu.
Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu. Soma Zaidi...

DUA WAKATI WA KURUKUU,KUITIDALI, KUSUJUDI NA NAMNA YA KUSOMA TAHIYATU
6. Soma Zaidi...

KAZI ZA MALAIKA
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Soma Zaidi...

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI
β€œKatika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...

Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini
Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s. Soma Zaidi...

Maana ya Kuamini Mitume wa Allah (s.w) katika maisha ya kila s iku.
Waumini wa kweli wa Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji
Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s. Soma Zaidi...

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu) Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...