picha

JITIBU KWA TANGAIZI: faida za kiafya za tangaizi

Tangaizi ni katika mimea yenye asili na bara la asia hususan nchi ya China.

JITIBU KWA TANGAIZI: faida za kiafya za tangaizi

FAIDA ZA TANGAIZI

Tangaizi ni katika mimea yenye asili na bara la asia hususan nchi ya China. Mmea huu hutambulika kwa faida zake za kitiba toka zamani sana. Na karibia dunia nzima hutumia tangaizi kama tiba na kama kinywaji. Ndani ya tangaizi kuna chembechembe ziitwazo gingerol, hizi ndizo huipa tangaizi uwezo wake wa kitiba.

 

Unaweza kutumia tangaizi kwa kutafuna vipande vidogovidogo au kwa kutia kwenye  mboga. Pia unaweza kuweka kwenye chai ikiwa vipande vidogo au ikiwa imekauchwa na kusagwa kama ungaunga. Zipo njia nyingi za kutumia tangaizi. Zifuatazo ni katika baadhi ya faida za tangaizi iafya:-

 

  1. Tangaizi ni mujarabu sana katika kutibu kichefuchefu. Hususani kichefuchefu cha mimba. Kwa ujumla kichefuchefu huwapata sana wajawazito, na watu walofanyiwa upasuaji wa ndani. Lakini kinaweza kumpata mtu yeyote. Unaweza kutumia tangaizi kwenye chai, ama kutafuna vipande vidogo. Hakikisha unakula japo gram moja.
  2. Hupunguza maumivu ya misuli
  3. Hupunguza maumivu ya viungo
  4. Husaidia katika kushusha kiwango cha sukari. Hususan kwa wenye kisukari type 2. kwa kufanya hivi pia hupunguza athari ya kupata maradhi ya moyo
  5. Husaidia kwa wenye tatizo la kutokupata choo na kukosa hamu ya kula.
  6. Hupunguza maumivu ya tumbo la chango kwa wanawake.
  7. Hupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani (cancer)
  8. Huimarisha afya ya ubongo
  9. Husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga za mwili.


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 1902

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 web hosting     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia, sababu zake na dalili zzake

Hapa utajifunza sababu za kupatwa na maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia

Soma Zaidi...
Faida za kula apple (tufaha)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha

Soma Zaidi...
Faida za pilipili

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za pilipili

Soma Zaidi...
FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA

Pera ni tunda bora lakini pia ni dawa, tambua umuhimu wa tunda hili kiafya

Soma Zaidi...
Faida za karoti

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za karoti na umuhimu wake kiafya

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Soma Zaidi...