image

Rangi za matunda

Fida za matunda huanzia kwenye rangi zake, je unajuwa kama rangi ya matunda inaeleza jambo?

Rangi za matunda

RANGI ZA MATUNDA
Unaweza kujiuliza ni kwa nini matunda yana rangi mbalimbali? Hili swali Mwenyezi mungu aliyeumba kila kitu ndiye anajuwa saidi. Ila kwa ufupi utambuwe kuwa rangi katika matunda ni dalili ya ishara flani. Katika post hii tutaona baadhi ya rangi katika matunda. Mwisho wa post hii utaweza kutambua nini kimo katika tunda utakaloliona kwa kuangalia rang.

1.rangi nyekundu Rangi nyekundu kwenye matunda hutokana na nyembenchembe ziitwazo lycopene. Hizi ni antoxidant ambazo husaidia katika kulinda mwili dhidi ya sumu za vyakula. Sumu hizi mara nyingi huweza kuharibu seli ndani ya miili yetu. Pia sumu hizi husababisha mtu kuzeeka haraka. Chembechembe hizi pia husaidia katika kuzuia uharibifu wa seli mwilini. Huimarisha mfumo mzima wa kinga mwilini. Na pia husaidi akatika kulinda au kupunguza adhari za magonjwa ya moyo na saratani.matunda yenye rangi hii ni pamoja na tomato, matikiti, pilipili n.k

2.rangi ya njano. Rangi ya njano kwenye matunda husababishwa na chembechembe ziitwazo beta-carotene, hizi pia ni antoxidant. Chembechembe hizi husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini. Mwili huweza kubadili beta-carotene, kuwa vitamini A. Itambulike kuwa vitamini hivi ni muhimu sana katika afya ya mtu. Kupamabana mna maradhi mablimbali nna kuimarisha afya ya macho. Kupambana na wadudu wanaosababisha vidonda vya tumbo. Huimarisha afya ya ngizi na maeneo mengune yenye utando laini.miongoni mwa matunda yenye rangi hii ni viazi, karoti, maembe n.k

3.rangi ya kijani. Rangi ya kijani husaidia kutambuwa uwepe wa vitamini Ana C. Kama inavyotambulika mboga za majani zina rangi hii. Vitamini A na C huweza kupatikana kwa wingi kwenye rangi hii. Itambulike kuwa vitamini hivi ni muhimi katika kudhibiti mfumo mzima wa kinga mwilini. Upungufu wowote wa vitamini hivi viwili uanaweza kusababisha madhara makubwa mwilini.

4.rangi ya bluu na violet Rangi hii hutambulisha uwepo wa anthocyanin ambayo ni antioxidat. Itambulike kuwa antioxidant zina uwezo mkubwa wa kupambana na sumu mbalimbali ndani ya mwili. Sumu hizi zinasababishwa ba vyakula tunavyokula kwa kiasi kikubwa. Vyakula hivi vyenye rangi hii huwa vina vitamini C kwa kiasi kikubwa. Pia vyakula hivi vina kambakamba ambazo ni muhimu sana katika afya ya mtu.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 554


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Yafahamu magonjwa nyemelezi kwa watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano,. Ni magonjwa yanayowapata watoto wadogo kwa sababu kinga Yao bado ni ndogo. Soma Zaidi...

Faida za kula stafeli/soursop
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za stafel/soursop Soma Zaidi...

Vyakula vya madini kwa wingi, na kazi za madini mwilini
Utajifunza vyakula vyenye madini kwa wingi, kazi za madini mwilini na athari za upungufu wake Soma Zaidi...

Aina za vyakula ambayo huongeza damu kwa wajawazito na watoto
Hizi ni aina za vyakula ambavyo husaidia katika kuongeza damu kwa wajawazito na watoto. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula kabichi
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kabichi Soma Zaidi...

Faida za kula karoti
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kula karoti Soma Zaidi...

Faida 5 za asali na matumizi yake.
Katika post hii utakwenda kujifunza faida na matumizi ya asali mwilini. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula ndimu na limao
Soma Zaidi...

Matunda yenye vitamini C kwa wingi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matunda yenye vitamin C kwa wingi Soma Zaidi...

VINYWAJI SALAMA KWA MWENYE KISUKARI
Kuchaguwa vinywaji si jambo rahisi, lakini inabidi iwe hivyo kama una tatizo la kisukari. Je unasumbuka kujuwa vinywaji salama? makala hii ni kwa ajili yako, hapa tutaona vinywaji ambavyo ni salama kwa mwenye kisukari. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula kunazi/ lote tree
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula kunazi/ lotetree Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Ukwaju
Soma Zaidi...