Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

a) Wakati wa Ukhalifa wa Uthman bin Affan (r.a)

- Dola ya Kiislamu ilianza kuporomoka nusu ya pili ya uongozi wa Khalifah, Uthman bin Affan (r.a).
- Wanafiki wakiongozwa na Abdullah bin Sabaa, walizua fitna na kumtuhumu kiongozi wa Dola na kuanzisha imani na itikadi potofu.
- Wapinzani wa Dola ya Kiislamu walijiimarisha na kutuma wajumbe watatu kutoka Misri, Basra na Kufa kwa Khalifa kuwasilisha malalamiko yao.
- Wajumbe hao walirejesha fitina kwao kuwa ujumbe wao umepuuzwa na Khalifa, hivyo wakaandaa jeshi la askari 1000 ili kuangusha utawala wa Uthman (r.a).
- Wakazi wa Madina walipambana na waasi hao lakini walizidiwa nguvu na

hatimaye kuingia hadi Msikitini na kumuua Khalifa akiwa anasoma Qur’an.



b) Wakati wa Khalifa Ali bin Abi Taalib (r.a)

- Baada ya kuuliwa Uthman (r.a), wapinzani walishikilia mji wa Madina kwa siku sita na kuongoza wao na siku ya 6 walimtangaza Ali (r.a) kuwa ndiye Khalifa.
- Uchaguzi huu wa Ali (r.a) haukukubalika kwa Waislamu, na kuwagawa waislamu makundi manne.
i. Vita kati ya Bi Aisha (r.a) na Khalifa Ali (r.a), Vita vya Jamal (Ngamia)

- Bi Aisha (r.a) waliungana na Talha na Zubair (r.a) na kuandaa jeshi la kulipiza kisasi cha kuuliwa Uthman (r.a).
- Ali (r.a) walifanya sulhu na Bi Aisha pamoja na Mua’wiya (r.a) kwa kuafikiana kuwa Khalifa Ali (r.a) atawaadhibu wauaji wa Uthman (r.a) Dola ikiwa na amani.
- Mpinzani mkubwa, Abdullah bin Sabaa na jeshi lake walivuruga sulhu hiyo na vita vikapiganwa mji wa Basra na waislamu 10,000 walikufa.

ii.Vita kati ya Khalifa Ali (r.a) na Mua’wiya; Vita vya Sifin

- Wakati Ali anatawazishwa Ukhalifa, Mua’wiya alikuwa Gavana wa Syria, Khalifa Ali alimvua ugavana Mua’wiya lakini Mua’wiya alikataa.
- Khalifa Ali (r.a) aliandaa jeshi na kupigana na jeshi la Mua’wiya huko

Syria sehemu iitwayo Sifin mnamo mwaka 36 A.H.

- Musa Asha’r (r.a) kwa upande wa Khalifa walifanya sulhu na Amr bin Al- As (r.a) kwa upande wa Mua’wiya (r.a) lakini wauaji wa Uthman hawakutaka sulhu na kuamua kujitenga na kupambana na Khalifa Ali na Mua’wiya (r.a).
- Kundi hili lililojitenga na Khalifa Ali (r.a) liliitwa “Khawaarij”

(waliojitenga).



iii.Kuuliwa Khalifa Ali bin Abi Twalib (r.a)

- Khawaarij walipanga njama za kumuua Mua’wiya, Ali na Amr bin Al-As (r.a) aliyekuwa mshauri wa Mua’wiya (r.a) mwaka 40 A.H.ndani ya swala ya Alfajir.
- Muuaji wa Ali (r.a) alimjeruhi Ali vibaya kwa upanga wa sumu na hatimaye akafa siku ya 3 yake.
- Wauaji wa Mua’wiya na Amr (r.a) hawakufanikiwa kwani Mua’wiya na

Amr (r.a) hawakufika msikitini swala ile.

- Baada ya kuuliwa Ali bin Abi Twalib (r.a), mtoto wake Hassan alichaguliwa kushika nafasi ya Ukhalifa.
- Mua’wiya aliandaa jeshi na akapambana na Hassan (r.a) na mwishowe walikubaliana kuwa, Mua’wiya achukue Ukhalifa na baada ya kufa, uongozi utakuwa chini ya Hussein bin Ali (r.a).
- Kinyume na makubaliano, Mua’wiya kabla hajafa alimteua mtoto wake

Yazid kushika uongozi wa Dola baada yake.

- Dola ya Kiislamu iliyoasisiwa na Mtume (s.a.w) ikaporomoka na ufalme

ulioasisiwa na Mua’wiya ukachukua nafasi.



Mafunzo yatokanayo na kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

i. Ni muhimu na wajibu kwa waislamu kuwa makini katika kuandaa na kuchaguzi viongozi wa Kiislamu kwa mujibu wa malengo yao.


ii. Maadui wa Uislamu hawatarudi nyuma kamwe katika kuupiga vita Uislamu na waislamu.


iii. Mgawanyiko wa kimakundi ndani ya umma wa Kiislamu ndiye ufa pekee unaopelekea kudhoofika Uislamu na waislamu.


iv. Kuwabaini wanafiki na maadui wa Uislamu na mbinu zao ni jambo la msingi mno katika kuendesha harakati za Kiislamu.


v. Waislamu watakapokuwa tayari kikweli kweli kuupigania Uislamu, Uislamu utachukua hatamu yake yak kuongoza maisha ya jamii.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1792

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1

Soma Zaidi...
Mji wa Makkah na kabila la kiqureish

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.

Soma Zaidi...
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Soma Zaidi...