Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

a) Wakati wa Ukhalifa wa Uthman bin Affan (r.a)

- Dola ya Kiislamu ilianza kuporomoka nusu ya pili ya uongozi wa Khalifah, Uthman bin Affan (r.a).
- Wanafiki wakiongozwa na Abdullah bin Sabaa, walizua fitna na kumtuhumu kiongozi wa Dola na kuanzisha imani na itikadi potofu.
- Wapinzani wa Dola ya Kiislamu walijiimarisha na kutuma wajumbe watatu kutoka Misri, Basra na Kufa kwa Khalifa kuwasilisha malalamiko yao.
- Wajumbe hao walirejesha fitina kwao kuwa ujumbe wao umepuuzwa na Khalifa, hivyo wakaandaa jeshi la askari 1000 ili kuangusha utawala wa Uthman (r.a).
- Wakazi wa Madina walipambana na waasi hao lakini walizidiwa nguvu na

hatimaye kuingia hadi Msikitini na kumuua Khalifa akiwa anasoma Qur'an.



b) Wakati wa Khalifa Ali bin Abi Taalib (r.a)

- Baada ya kuuliwa Uthman (r.a), wapinzani walishikilia mji wa Madina kwa siku sita na kuongoza wao na siku ya 6 walimtangaza Ali (r.a) kuwa ndiye Khalifa.
- Uchaguzi huu wa Ali (r.a) haukukubalika kwa Waislamu, na kuwagawa waislamu makundi manne.
i. Vita kati ya Bi Aisha (r.a) na Khalifa Ali (r.a), Vita vya Jamal (Ngamia)

- Bi Aisha (r.a) waliungana na Talha na Zubair (r.a) na kuandaa jeshi la kulipiza kisasi cha kuuliwa Uthman (r.a).
- Ali (r.a) walifanya sulhu na Bi Aisha pamoja na Mua'wiya (r.a) kwa kuafikiana kuwa Khalifa Ali (r.a) atawaadhibu wauaji wa Uthman (r.a) Dola ikiwa na amani.
- Mpinzani mkubwa, Abdullah bin Sabaa na jeshi lake walivuruga sulhu hiyo na vita vikapiganwa mji wa Basra na waislamu 10,000 walikufa.

ii.Vita kati ya Khalifa Ali (r.a) na Mua'wiya; Vita vya Sifin

- Wakati Ali anatawazishwa Ukhalifa, Mua'wiya alikuwa Gavana wa Syria, Khalifa Ali alimvua ugavana Mua'wiya lakini Mua'wiya alikataa.
- Khalifa Ali (r.a) aliandaa jeshi na kupigana na jeshi la Mua'wiya huko

Syria sehemu iitwayo Sifin mnamo mwaka 36 A.H.

- Musa Asha'r (r.a) kwa upande wa Khalifa walifanya sulhu na Amr bin Al- As (r.a) kwa upande wa Mua'wiya (r.a) lakini wauaji wa Uthman hawakutaka sulhu na kuamua kujitenga na kupambana na Khalifa Ali na Mua'wiya (r.a).
- Kundi hili lililojitenga na Khalifa Ali (r.a) liliitwa 'Khawaarij'

(waliojitenga).



iii.Kuuliwa Khalifa Ali bin Abi Twalib (r.a)

- Khawaarij walipanga njama za kumuua Mua'wiya, Ali na Amr bin Al-As (r.a) aliyekuwa mshauri wa Mua'wiya (r.a) mwaka 40 A.H.ndani ya swala ya Alfajir.
- Muuaji wa Ali (r.a) alimjeruhi Ali vibaya kwa upanga wa sumu na hatimaye akafa siku ya 3 yake.
- Wauaji wa Mua'wiya na Amr (r.a) hawakufanikiwa kwani Mua'wiya na

Amr (r.a) hawakufika msikitini swala ile.

- Baada ya kuuliwa Ali bin Abi Twalib (r.a), mtoto wake Hassan alichaguliwa kushika nafasi ya Ukhalifa.
- Mua'wiya aliandaa jeshi na akapambana na Hassan (r.a) na mwishowe walikubaliana kuwa, Mua'wiya achukue Ukhalifa na baada ya kufa, uongozi utakuwa chini ya Hussein bin Ali (r.a).
- Kinyume na makubaliano, Mua'wiya kabla hajafa alimteua mtoto wake

Yazid kushika uongozi wa Dola baada yake.

- Dola ya Kiislamu iliyoasisiwa na Mtume (s.a.w) ikaporomoka na ufalme

ulioasisiwa na Mua'wiya ukachukua nafasi.



Mafunzo yatokanayo na kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu

i. Ni muhimu na wajibu kwa waislamu kuwa makini katika kuandaa na kuchaguzi viongozi wa Kiislamu kwa mujibu wa malengo yao.


ii. Maadui wa Uislamu hawatarudi nyuma kamwe katika kuupiga vita Uislamu na waislamu.


iii. Mgawanyiko wa kimakundi ndani ya umma wa Kiislamu ndiye ufa pekee unaopelekea kudhoofika Uislamu na waislamu.


iv. Kuwabaini wanafiki na maadui wa Uislamu na mbinu zao ni jambo la msingi mno katika kuendesha harakati za Kiislamu.


v. Waislamu watakapokuwa tayari kikweli kweli kuupigania Uislamu, Uislamu utachukua hatamu yake yak kuongoza maisha ya jamii.



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 199

Post zifazofanana:-

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

swala ya tarawehe na namna ya kuiswali, rakaa zake na suna zake.
5. Soma Zaidi...

kwa nini riba ni haramu?
Soma Zaidi...

DUA 51 - 60
51. Soma Zaidi...

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA BAMIA (OKRA)
Makala hii inakwenda kukuonyesha faida za kula bamia kwa afya afya Soma Zaidi...

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Dua sehemu 03
Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa. Soma Zaidi...

Dalili za gonorrhea - gonoria
Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume Soma Zaidi...

GEOGRAPHY NECTA PAST PAPERS REVIEW PAPERR 04
116. Soma Zaidi...

Namna ya kumuosha maiti hatua kwa hatua, nguzo na sunnah za josho la maiti
1. Soma Zaidi...

Hadithi aliyoisimulia Kijakazi kwa sultan
Soma Zaidi...

AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...