NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE

Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a.

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE


Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a.s)katika Mitume waliotajwa katika Qur-an ni Nabii Nuhu(a.s). Nuhu(a.s) ni miongoni mwa Mitume wa mwanzo mwanzo kabisa. Kutokana na mabaki ya kihistoria tunajifunza kuwa Nabii Nuhu na kaumu yake waliishi katika nchi ya Iraq.



Mazingira ya Jamii Aliyoikuta Nabii Nuhu (a.s)
Nabii Nuhu(a.s) aliwakuta watu wa jamii yake wakimshirikisha Allah(s.w)kwa namna mbali mbali nawalikuwa wakiabudia masanamu waliyoyachonga na kuyapa majina ya W adda , Suwa’a , Y aghuutha , Y a’uuka na Nasraa . Kama tulivyofahamishwa katika Qur-an kuwa viongozi wa jamii ya kishirikina ambao walikuwa ndio wapinzani wakubwa wa ujumbe wa Nabii Nuhu waliwanasihi wafuasi wao:




“Msiache miungu yenu, wala msiwache Wadda wala Suwa’a wala Yaghuutha na Ya’uka na Nasraa.” (71:23).



Mtume(s.a.w) anatufahamisha katika Hadith kuwa Wadda na wale waliotajwa pamoja naye walikuwa ni watu wacha-Mungu katika jamii yao. Walipofariki,watu wakaanza kuyazungukia



makaburi yao na shetani akakichochea kizazi kilichofuata kuunda sanamu za watu hao. Kwa kufanya hivyo walidhani wangeliweza kuwaiga vitendo vyao vyema kwa kuwa na taswira za watu hao daima katika akili zao. Kizazi cha tatu kilishawishika kirahisi sana kuwa watu hao walikuwa ni miungu wanaostahiki kuabudiwa badala au pamoja na Allah(s.w). Masanamu yote yanayoabudiwa yana historia ya namna hii.



Wito wa Nabii Nuhu(a.s) kwa Watu Wake
Nabii Nuhu(a.s) kama walivyofanya Mitume wote, aliwafundisha watu wake Tawhiid kuwa wamuamini Allah (s.w) kwa kuzingatia ishara mbali mbali zilizowazunguka, na kwamba wamuabudu yeye peke yake na wasimshirikishe na chochote. Aliwaonya juu ya adhabu kali itakayowafika iwapo hawatakoma kumshirikisha Allah(s.w) na miungu wengine.Juu ya wito wa Nuhu(a.s) kwa watu wake Qur-an inatufahamisha:




“Tulimpeleka Nuhu kwa watu wake, naye akasema: “Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila yeye. Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya siku (hiyo) iliyo kuu.” (7:59).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2528

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Vita vya badri

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Jitihada alizozifanya Khalifa wa Tatu katika kuilinda Quran

Soma Zaidi...
KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka.

Soma Zaidi...
Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Soma Zaidi...
tarekh

MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).

Soma Zaidi...
Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...