Figo ni nini, ni yapi maradhi yake na nitajiepusha vipi na maradhi ya figo

Makala hii itakwenda kukueleza ni nini hasa hizi figo, na ni yapi maradhi yake na ni kwa namna ggani utaweza kujilinda na maradhi ya figo.

Figo ni nini, ni yapi maradhi yake na nitajiepusha vipi na maradhi ya figo

IJUWE FIGO NA MARADHI YAKE NA NAMNA YA KUJIKINGA NA MARADHI YA FIGO:

Figo ni katika viungo muhimu sana katika mwili wa mwanadamu. Ijapokuwa kila kiungo ni muhimu kwenye mwili wa binadamu, lakini katika mfumo wa kutoa mkojo na kuchuja damu figo ni muhimu zaidi. maradhi ya figo yamekuwa yakiongezeka kuliko ilivyokuwa hapo zmani, ijapokuwa kasi yake sio sawa na maradhi mengine. Makala hii itakwenda kukueleza ni nini hasa hizi figo, na ni yapi maradhi yake na ni kwa namna ggani utaweza kujilinda na maradhi ya figo.


Kila mtu ana figo mbili kwenye mwili wake, ukubwa wa figo unakadiriwa kufukia ukubwa wa ngumi yako. Katika mwili wako figo hupatikana karibia na katikati ya mgongo chini kidogo ya mbavu. Ndani ya kila figo kuna mamilioni ya vichujio vya kuchuja damu vinavyojulikana kama nephron. Kazi yake kubwa ni kuchuja damu, kuondoa uchafu kwenye damu na kuondoa maji ya ziada kwenye damu na kupata mkojo ambao ni mchanganyiko wa majina na uchafu uliotoka kwenye damu. Baadaye maji haya ya mchanganyko yanakwenda kwenye kibofu na kuhifadhiwa kama mkojo.



Kati ya maradhi mengi ya figo huanza kuathiri hizi nephone. Na endapo hizi nephrone zikiharibiwa zinapelekea figo kuathirika na kushindwa kufanya kazi vyema na kushindwa kuondoa uchau kwenye damu. Katika sababu za tatizo hili la kuathirika kwa nephone inaweza kuwa matatizo ya kurithi, majeraha, ama matumizi ya madawa ambayo athari yake yanaweza kuathiri figo.



Unaweza kuwa hatarini sana kama una maradhi ya kisukari, ama kama una shinikizo kubwa la damu ama una ukaribu wa kifamilia na watu ambao wana tatizo hili. Maradhi hatari ya figo ni yale ambayo huathiri nephone kipolepole na huwenda hii kuchukuwa miaka kadhaa hadi kuja kuumwa. Matatizo mengine yanayoweza kuathiri figo ni kama saratani ya figo na vijiwe vya kwenye figo.



Katika njia za kulinda figo yako dhidi ya maradhi ni pamoja na kunywa maji mengi angalau glasi 8 kwa siku. Fanya mazoezi na punguza kula vyakula vyenye chumvi sana. Nenda chooni kila unapohisi kukojoa wacha kubana mkojo kwa muda mrefu. Hizi ni baadhi tu ya njia ambazo zitakusaidia kulinda figo zako dhini ya maradhi.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 636

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia Ugonjwa wa ini

Posti hii inaelezea namna na jinsi ya kujikinga au kuzuia Ugonjwa wa ini.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jipu la Jino

Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, ni madhara ambayo yanaweza kutokea iwapo maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo hayatatibiwa kwa wakati.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa moyo.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mambo hatari yanayosababisha ugonjwa wa moyo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuporomoka kwa mapafu (pneumothorax)

Posti hii inazungumzia Ugonjwa wa mapafu ambao hujulikana Kama pafu lililoporomoka (Pneumothorax) hutokea wakati hewa inavuja kwenye nafasi kati ya mapafu yako na ukuta wa kifua. Hewa hii hutoka nje ya pafu lako. Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na jera

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa upele

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa uchovu sugu.

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa uchovu sugu ni ugonjwa tata unaoonyeshwa na uchovu mwingi ambao hauwezi kuelezewa na hali yoyote ya matibabu. Uchovu unaweza kuwa mbaya zaidi kwa shughuli za kimwili au kiakili, lakini haiboresha kwa kupumzika

Soma Zaidi...
Matibabu ya VVU na UKIMWI

Somo Hili linakwenda kukuletea matibabu ya VVU/UKIMWI

Soma Zaidi...
Madhara ya kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kama mtu hajatibiwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi Mdomoni.

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za fangasi Mdomoni kwa watoto, vijana, watu wazima na mama wanaonyonyeshwa.

Soma Zaidi...