picha

Dalili za ukimwi siku za mwanzo

Makala hii inakwenda kukupa majibu ya maswali mengi kuhusu VVU na UKIMWI. tutakwenda kuona kwa ufupi historian a chanzo cha VVU na UKIMWI. hatuwa za maambukizi ya VVU na ukimwi na dalili zake za kuonekana toka kupata maambukizi. Pia hapa utajifunza namna

Dalili za ukimwi siku za mwanzo

DALILI ZA UKIMWI SIKU ZA MWANZO
Bila shaka umeshawahi kujiuliza kuhusu dalili za mwanzo za VVU na ukimwi. Makala hii itakwenda kujibu baadhi ya maswali yako mengine ambayo ulikuwa ukijiuliza kama, ni zipi dalili za mwanzo za vvu na ukimwi, je ukimwi unaingiaje, ni nini kitatokea baada ya kupata virusi vya ukimwi na mengineyo zaidi. Makala hii ni moja ya makala zetu za kutoa elimu ya afya ili kuendelea kuelimusha jamii.



Je nini maana ya UKIMWI?
UKIMWI ni ufupisho wa maneno Upungufu Wa Kinga Mwilini. Ukimw husababishwa na aina ya virusi inayojulikana kwa jina la VVU yaani Virusi vya ukimwi. Historia ya Ukimwi imeanza zamani sana toka miakaya 1950. Kuna nadharia nyingi sana kuhusu chanzo na asili ya ukimwi. Kisayansi nadharia inayokubalika ni kuwa chanzo cha ukimwi ni masokwe. Miaka ya 1980 ukimwi ndipo ulipoanza kujulikana rasmi.


Hatua za maambukizi ya VVU na UKIMWI
Mara tu baada ya mtu kupata maambukizi mapya, atapitia hatuwa kuu tatu kabla ya kuambiwa ana ukimwi. hatuwa hizi hutofautiana kwa dalili zake. Kutoka kuambukizwa virusi mpaka kuambiwa mtu ana ukimwi inaweza kuchukuwa miaka mitano hadi kumi. Wapo baadhi ya watu wakawa pungufu ya hapo ama Zaidi ya hapo. Hebu saa tuzione hatuwa hizi na dalili zake.



A. Hatuwa ya kwanza baada ya maambukizi mapya:
Hatuwa hii hupatikana mwanzoni mwa wiki za mwanzo kabisa baada tu ya kupata maambukizi mapya. Katika hatuwa hii mtu hawzi kupima akaonekana kuwa ana maambukizi. Katika hatuwa hii virusi vinakuwa ni vingi sana kwenye damu, na huzaliana kwa kasi sana. Na hapa mtu anaweza kuonyesha baadhi ya dalili. Kuonyesha dalili hizi inachukuwa wiki 2 hadi sita. Baada ya hapo hatoweza kuona dalili tena. Dalili za maambukizi ya VVU katika hatuwa hii ni kama:-

1. Kupata mafuwa
2. Vidonda vya koo
3. Uchovu
4. Homa
5. Maumivu ya kichwa
6. Kutokwana upele
7. Kuvimba na kuuma kwa tezi za shingo na mapajani.



B. Hatuwa ya pili baada ya baambukizi mapya
Hatuwa hii ni katika hatuwa hatari sana. Katika kipindi hiki kiwango cha virusi kwenye damu hupunguwa na virusi kuelekea maeneo mengine ya mwili na kuathiri seli hai nyeupe zinazojulikana kama VD4. Katika hatuwa hii mtu akipima ataonekana kama ameathirika, lakini hakuna dalili yeyote itakayoonekana kwa muathirika katika kipindi hiki chote. Hatuwa hii inaweza kudumu kwa muda wa miaka mitano hadi 10. Katika wakati huu wote virusi vitaendelea kuathiri na kuharibu seli za CD4 mabzo ndio mlinzi wa mwili.


Seli za CD4 ni nini na ni zipi kazi zake?
Kabla hatujaona hatuwa ya tatu kwanza tuone kwa ufupi ni nini seli za CD4. Katika damu kuna seli aina kuu tatu ambazo ni seli hai nyeupe, seli hai nyekundu na seli sahani. Kila moja kati ya hizi ina kazi yake maalumu. Kwa mfano:-



1. Kazi za seli hai nyekundu ni kusafirisha hewaa ya oksijeni kutoka kwenye mapafu na kupeleka kwenye moyo ambapo husambazwa kuelekea maeneo mengine ya mwili. Seli hai nyekundu ndizo ambazo nyingi kwenye damu na ndio maana damu ni nyekundu. Pia kazi nyingine ni kusafirisha hewa ya kabonidaiyoksaidi kutoka kwenye seli kupeleka kwenye mapafu kupitia kweye moyo.



2. Kazi za seli sahani ni kusaidia katika kuganda kwa damu na kupona kwa vidonda. Endapo utakuwa umejikata na jeraha likawa linatoa damu, seli sahani hiletwa kwa wing eneolile ili kusaidia damu kutoendelea kutoka na kuganda eneo lile. Uponaji wa vidonda na majeraha pia huhitaji seli hizi.


3. Seli hai nyeupe kazi zake ni kulinda mwili zidi ya vijidudu vya maradhi kama bakteria, fangasi, virusi na protozoa. Kwa ufupi seli hizi ni kama ndio walinzi wa mwili endapo zitapunguwa mwili utakuwa hatarini. Seli hizi hutafuta vijidudu hivi popote vilipo na kuviuwa kwa kuvimwagia kemikalia mbazo zitavifanya vife. Seli hai yeupe ndizo huitwa cd4. Kwa hiyo kazi kuu ya seli za CD4 ni kupambana na vijidudu shambulizi ndaniya mwili.



Sasa virusi vya ukimwi (VVU) vinapoingia mwilini moja kwa moja hutafuta seli za CD4, Huziingia ndani yake na kuanza kuzaliana humo. Baada ya kuwa virusi bni vingi ndani ya sli hiyo hupasuka na kumwaga virusi nje, na seli ile hufa kabia. Maelfu ya virusi hivi vilivyitoka kwenye seli moja huvamia seli nyingine na mhakato hujirudia. Baada ya muda wa miaka kadhaa mtu huyu atakuwa na upungufu wa kinga mwilini na hapo ndipo huambiwa ana ukimwi.



C. Hatuwa ya tatu (ukimwi).
Kikawaida mtu mwenye afya aha seli za cd4 500 mpaka 1500 kwenye kipimo kimoja. Sasa kama ana VVU huanza kuharibu seli hizi hadi hupunguwa chini ya kiwango hiko. Zikipunguwa kutoka 500 hadi 200 hapa huambiwa mtu huy ana upungufu wa kinga mwilini yaani UKIMWI. tafiti zinaonyesha kuwa baada ya kufikia hatuwa hii ya cd4 200 kama mtu huyu hataanza matibabu maalumu itachukuwa mikaa mitatu hadi kufariki. Hatuwa hii mgonjwa ataanza kuona dalili za ukimwi ambazo ni:-

1. Kupunguwa uzito kwa asilimia 10 bila ya sababu maalumu
2. Kuharisha mfululizo
3. Kuota upele kuzungukia maeneo mbalimbali ya mwili hadi sehemu za siri
4. Kuota majipu
5. Kusumbuliwa na fangasi mara kwa mara
6. Kuwa na homa za mara kwa mara
7. Kukonda sana bila ya sababu maalumu
8. Kuwa na uchovu wa mara kwa mara
9. Kupata maradhi nyemelezi kama kifua kikuu, kisukari, saratani, mkanda wa jeshi na mengineyo.



Nini mtu afanye baada ya kugundulika kuwa ni muathirika?
Vyema kwanza kupata ushauri kutoka kwa mtoa huduma ya ushauri nasaha. Hii itasaidia kumuweza mtu vyema kiakili, na kumuandaa kukabiliana na changamoto. Pia itamsaidia kujifunza Zaidi kuhusu namna ya kuishi na virusi vya ukimwi. pia atatakiwa kuanza matibabu haraka iwezekanavyo. Matibabu haya yatamsaidia ku:-

1. Kupunguza uzalishaji wa virusi vipya ndani ya mwili
2. Kuzuia virusi vya ukimwi visiharibu seli nyingine za mwili
3. Kumfanya mtu asifike kwenye hatuwa ya tatu ya kuambiwa ana ukimwi
4. Kupunguza uwezo wa mtu kumuambukiza mwingine.



Ni muda gani virusi huonekana kwenye kipimo?
Vipimo vya VVU vipo katika makundi kadhaa. Vipo ambavyo hipima kwa kutumia damu, vipo kwa kutumia mate. Tukiacha mbali hayo yote ni kuwa virusi vya ukimwi huanza kuonekana baada ya wiki tatu jhadi miezi mitatu kwa ajili ya uthibitisho Zaidi. Pia vipo vipimo ambavyo kuweza kuonyesha mapema Zaidi ila mara nyingi hivi havipatikani kwa urahiri.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 4466

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)

Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea

Soma Zaidi...
Je minyoo inaweza kusababisha mmeng'enyo wa chakula kuwa dhaifu?

Mfumo wa chakula unaweza kuwa dhaifu kwa sababu nyingi ikiwepo vyakula vyenyewe, vinywaji ama maradhi. Vipi kuhusu minyoo? Endelea na makala hii utajifunza zaidi.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Kuvimba ubongo (Encephalitis)

Post hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa ubongo ambao kitaalamu huitwa Encephalitis, Ni Maambukizi ya virusi ni sababu ya kawaida ya hali hiyo. Ugonjwa wa Kuvimba ubongo unaweza kusababisha dalili zinazofanana na Homa, kama vile Homa au

Soma Zaidi...
Kwa nini kung’atwa na mbu hakuambukizi UKIMWI?

Ingawa mbu hunyonya damu kwa binadamu, hawana uwezo wa kueneza virusi vya UKIMWI (VVU). Sababu ni kwamba virusi vya VVU haviwezi kuishi wala kuzaliana ndani ya mwili wa mbu, na pia mbu hawaingizi damu ya mtu mmoja kwa mwingine wanapong’ata.

Soma Zaidi...
Dalilili za Ngozi kuwa kavu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ngozi kuwa kavu si mbaya, lakini inaweza kusumbua na isipendeze, ikitengeneza mistari laini na Mikunjo.

Soma Zaidi...
Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Dalili za uchovu wa joto mwilini.

Uchovu wa joto ni hali ambayo dalili zake zinaweza kujumuisha kutokwa na jasho kubwa na mapigo ya haraka, ambayo ni matokeo ya joto la mwili wako. Ni mojawapo ya magonjwa matatu yanayohusiana na joto, huku tumbo la joto likiwa kali zaidi na Kihar

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa kisukari aina ya 1 (type 1)

Kisukari cha Aina ya 1, ambacho wakati mmoja kilijulikana kama Kisukari cha changa au Kisukari kitegemeacho insulini, ni hali sugu ambapo kongosho hutoa insulini kidogo au haitoi kabisa, homoni inayohitajika kuruhusu sukari (glucose) iingie kwenye se

Soma Zaidi...