Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto

Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto

MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO




Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.



Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.



Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-
A.Homa
B.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivu
C.Kuvimba kwa tumbo
D.Kuona damu kwenye kinyesi
E.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaa
F.Kupungua uzito
G.Ngozi kuwa na njano.



Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.
Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-



A.Homa
B.Kichefuchefu
C.Kutapika
D.Tumbo kujaa na kuiwa gumu
E.Kuharisha
F.Kukosa choo



2.Gesi tumboni.
Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-
A.Kumeza hewa sana
B.Kula kupitiliza
C.Kuvuta sigara
D.Kutafuna bigjii
E.Chakula kutokumeng’enywa vyema
F.Kula vyakula vyenye gesi
G.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.



3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-
A.Kiungulia
B.Kuhisi kishiba na tumbo kujaa
C.Kucheua gesi
D.kichefuchefu



4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-
A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)
B.Maumivu kuongezeka
C.Maumivu wakati unaponyanyua kitu
D.Kujihisi umeshiba
5. kuwa na vijiwe kwenye figo
Vijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-



A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kali
B.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa mara
C.Kichefuchefu
D.Vomiting
E.Homa



Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-
A.Tumbo la chango
B.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengine
C.Kuwa na shida kwenye ovari
D.Kuwa na ujauzito uliotungia nje
E.Kuwa na ugonjwa wa PID





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 16006

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi

Kiufipi posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa ukosefu wa mkojo

Posti hii inaonyesha namna ya kujizuia,Mambo ya Hatari,na na Mambo yanayopelekea Ugonjwa wa ukosefu wa mkojo

Soma Zaidi...
Njia za kutibu saratani

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.

Soma Zaidi...
Matibabu ya fangasi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya fangasi

Soma Zaidi...
MJUE MBU, NA YAJUWE MARADHI MAKUU MATANO (5) HATARI YANAYOAMBUKIZWA NA MBU, malaria kukamata namba moja kwenye maradhi hayo)

Mbu ni katika wadudu ambao husababisja vifo vya maelfu kila mwaka, na mamilioni ya watu wanaathirika na maradhi yaletwayo na mbu.

Soma Zaidi...
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chano chake

Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.

Soma Zaidi...
Je pumu inaweza kusababishwa na virusi ama bakteria?

Hapa utakwenda kujifunza jinsi ambavyo pumu inaweza kuwa na mahusiano kwa kuwepo kwa aina flani ya bakteria ama virusi.

Soma Zaidi...
MAMBO HATARI KWA MWENYE VIDONDA VYA TUMBO

MAMBO HATARI KWA MWENYE VIDONDA VYA TUMBO Tukiachia mbali kuchukua dawa aina ya NSAIDs, unaweza kuwa na hatari ya kuongezeka kwa vidonda vya tumbo ikiwa: Utakuwa ni mvutaji wa sigara.

Soma Zaidi...
Fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo

HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu.

Soma Zaidi...