Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto
Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO
Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.
Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.
Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-
A.Homa
B.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivu
C.Kuvimba kwa tumbo
D.Kuona damu kwenye kinyesi
E.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaa
F.Kupungua uzito
G.Ngozi kuwa na njano.
Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.
Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-
A.Homa
B.Kichefuchefu
C.Kutapika
D.Tumbo kujaa na kuiwa gumu
E.Kuharisha
F.Kukosa choo
2.Gesi tumboni.
Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-
A.Kumeza hewa sana
B.Kula kupitiliza
C.Kuvuta sigara
D.Kutafuna bigjii
E.Chakula kutokumeng’enywa vyema
F.Kula vyakula vyenye gesi
G.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.
3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-
A.Kiungulia
B.Kuhisi kishiba na tumbo kujaa
C.Kucheua gesi
D.kichefuchefu
4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-
A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)
B.Maumivu kuongezeka
C.Maumivu wakati unaponyanyua kitu
D.Kujihisi umeshiba
5. kuwa na vijiwe kwenye figo
Vijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-
A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kali
B.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa mara
C.Kichefuchefu
D.Vomiting
E.Homa
Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-
A.Tumbo la chango
B.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengine
C.Kuwa na shida kwenye ovari
D.Kuwa na ujauzito uliotungia nje
E.Kuwa na ugonjwa wa PID
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 web hosting 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?
Hivi huwa unachunguza choo chako? ivi huwa kinazama kwenye maji ama kinaelea? Kila damu ama malendalenda, je ni cheusi sana na kina harufu kali sana.
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu ugonjwa wa makende kushindwa kushuka
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya makende kushindwa t, hiki ni tatizo na huleta madhara
Soma Zaidi...Dalili za kuaribika kwa mishipa ya retina.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu ambaye ana tatizo kwenye mishipa ya retina,ni tatizo ambalo uwakumba wafu wengi wenye matatizo ya kisukari.
Soma Zaidi...VIPIMO VYA MINYOO (UTAJUAJE KAMA UNA MINYOO)? fecal test, blood test, colonoscopy tape test X-ray, MRI na CT scan.
VIPIMO VYA MINYOO Haitoshelezi kuwa na dalili pekee ukathibitisha kuwa una minyoo.
Soma Zaidi...Hatua za Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.
Soma Zaidi...Matibabu ya vidonda sugu
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya vidonda vya tumbo sugu
Soma Zaidi...