Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
MAUMIVU YA TUMBO KWA CHINI UPANDE WA KUSHOTO
Sehemu ya kushoto ya tumbo lako kwa chini hupatikana mwishilizo wa utumbo mkubwa. Pia kwa upande wa wanawake sehemu hii hupatikana ovari ya kushoto. Katika hali za kawaida maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto sio jambo la kuogopesha sana. Kwani maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe bila ya kuhitaji uangalizi wa kidaktari.
Je na wewe ni mmoja kati ya wanaosumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa shini upande wa kushoto? Je una muda gani na tatizo hili?. makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza sababu za maumivu ya tumbo sehemu ya chini upand wa kushoto.
Kama nilivyotangulia kukuijuza kuwa maumivu haya si jambo la kuogopesha. Basi ni vyema kwa haraka ukamuona daktari endapo utaona dalili zifuatazo:-
A.Homa
B.Sehemu husika kuwa na ugumu na maumivu
C.Kuvimba kwa tumbo
D.Kuona damu kwenye kinyesi
E.Kuendelea kuwa na kichefuchefu na kutapika kwa masik kadhaa
F.Kupungua uzito
G.Ngozi kuwa na njano.
Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
1.Kuwa na shida kwenye utumbo mkubwa.
Hii hutikea pale kwenye utumbo mkubwa kunapoota kama vijifuko vijidogo. Hivi sio jambo la kuogopa sana kiafya maana mara nyingi havina madhara na hupotea vyenyewe. Hali hii huwapata sana wenye umri zaidi ya miaka 40. sasa ikitokea vijifuko hivi vimeshambuliwa na vijidudu huvimba na kuleta maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Dalili zake ni kama:-
A.Homa
B.Kichefuchefu
C.Kutapika
D.Tumbo kujaa na kuiwa gumu
E.Kuharisha
F.Kukosa choo
2.Gesi tumboni.
Sababu nyingine ni kujaa gesi tumboni. Gesi tumboni inaweza kusababishwa na:-
A.Kumeza hewa sana
B.Kula kupitiliza
C.Kuvuta sigara
D.Kutafuna bigjii
E.Chakula kutokumeng’enywa vyema
F.Kula vyakula vyenye gesi
G.Kuwa na bakteria kwenye utumbo mkubwa.
3.Kuvimbiwa ama chakula kutokumeng’enywa vyema tumboni. Hali hii huplekea maumivu ya tumbo kwa juu. Maumivu haya wakati mwingine husambaa na kuathiri chini ya tumbo upande wa kushoto. Mtu pia ataona dalili kama:-
A.Kiungulia
B.Kuhisi kishiba na tumbo kujaa
C.Kucheua gesi
D.kichefuchefu
4.Ngiri henia; henia ina dalili kama:-
A.Kuongezeka uvimbe maeneo ya tumboni (si kila henia)
B.Maumivu kuongezeka
C.Maumivu wakati unaponyanyua kitu
D.Kujihisi umeshiba
5. kuwa na vijiwe kwenye figo
Vijiwe vya kwenye vigo vinatokana na mkusanyiko wa madini ya chumvi. Vijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibofu ama maeneo mengine kwenye mfumo wa mkojo. Vijijiwe hvi vinaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto. Pia vinaweza kusababisha maumivu ya mgongo upande mmoja na nyuma pia na kwenye mbavu. Tofauti na dalili hizi pia mgonjwa anaweza kupata dalili zifuatazo:-
A.Mkojo wenye rangi ya kahawiya, nyekundu ama mawingu mawingu na haruu kali
B.Mkojo wenye maumivu makali unaotokea mra kwa mara
C.Kichefuchefu
D.Vomiting
E.Homa
Maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kulia kwa wanawake, husababishwa na yafuatayo:-
A.Tumbo la chango
B.Kuota tishu za tumbo la uzazi maeneo mengine
C.Kuwa na shida kwenye ovari
D.Kuwa na ujauzito uliotungia nje
E.Kuwa na ugonjwa wa PID
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPosti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi watu walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu, pamoja na kuwepo Kwa sababu zinazopekekea kupata tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ila Kuna watu wenye hali Fulani wako kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu kama
Soma Zaidi...Pumu ni ugonjwa wa njia ya upumuaji unaojulikana na kizuizi cha muda mrefu cha njia ya upumuaji. Inahusisha mfumo wa upumuaji unaobana njia ya hewa, Inaweza kuwa ya nje (hii hutokea kwa vijana kutokana na mizio) au ya ndani (hutokea kwa wazee)
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi,ni kutokana na kazi zao pamoja na mazingira yao kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa ukimwi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
Soma Zaidi...