picha

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

1. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo usababishwa na bakteria ambao uingia na kushambulia sehemu za ndani za kibofu Cha mkojo, bakteria hao wanaweza kutoka sehemu mbalimbali kama vile kwenye mkojo wenyewe ikiwa mkojo umekaa kwa mda mrefu bila kutolewa nje hao bakteria wanaweza kushambulia sehemu za ndani ya kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi kwenye kibofu Cha yanayoambatana na uvimbe.kwa hiyo ni lazima kukojoa tu baada ya kuhisi mkojo Ili kuepuka madhara ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

 

2. Kutumia sana ngono zembe yaani kujamiiana bila kutumia kondomu.

Hii ni mojawapo ya sababu ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa ya ngono ambapo bakteria kutoka kwa mtu Mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine ambaye Hana maambukizi na kusababisha kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kushambulia na kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hasa hasa kama bakteria hawa wasipotibiwa  mapema uweza kuleta madhara makubwa zaidi na kusababisha ugumba. Kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana.

 

3. Kuaribika kwa sehemu za kuchuja mkojo.

Wakati mwingine Kuna kuharibika kwa sehemu mbalimbali zinazohusika na kuchuja mkojo, kama vile figo, nephroni na sehemu zote kwa hiyo hali hii usababisha bakteria kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mkojo hauwezi kutoka kwa wakati au pengine kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, hali ambayo usababisha bakteria kuendelea kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo. Kwa hiyo tunapaswa kuangalia mfumo wote wa kibofu Cha mkojo.

 

4. Kutumia catheter kwa mda mrefu au mara kwa mara.

Hii ni sababu mojawapo ambayo ufanya kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, kwa sababu catheter inaweza kuharibu kwenye milija wa mkojo na kusababisha bakteria kuingia na kuleta madhara makubwa ambayo yanasababisha kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo inabidi catheter kuwepo kwa mda unaohitajika, mda isizidi Ili kuzuia maambukizi.kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuhakikisha kuwa catheter unatolewa kwa mda.

 

5. Wanawake wanaotumia uzazi wa mpango.

Wanawake wengi wanaoweka mipira kwaenye uke illi kuzuia  mimba isitungwe usababisha bakteria kupita na kuingia kwenye sehemu ya kibofu Cha mkojo na kuleta madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mipira hiyo uacha uwazi ambao usababisha bakteria kuweza kupita na kuzaliana huko na kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3661

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 ai web app     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Namna ya Kupunguza Stress kwa Njia Asilia

Katika ulimwengu wa sasa wenye kasi kubwa, msongo wa mawazo (stress) umekuwa changamoto ya kawaida kwa wengi. Makala hii inakupa mbinu rahisi, asilia, na zenye ufanisi unazoweza kuzitumia kila siku ili kutuliza akili yako, kuboresha afya yako ya hisia, na kurejesha furaha.

Soma Zaidi...
Kichwa kinaniuma mbele sielewi nini

Zijuwe sababu za kuumwa nankichwa upande mmoja wa kichwa.

Soma Zaidi...
Unene kupita kiasi wakati wa ujauzito: Athari zake.

Uzito wa mwili wakati wa ujauzito una nafasi muhimu sana katika afya ya mama na mtoto. Ingawa ni kawaida kupata uzito wakati wa kulea mimba, unene uliopitiliza (Obesity) kabla au wakati wa ujauzito huleta changamoto za kiafya zinazoweza kuwa hatari. Makala hii inaangazia athari za unene uliokithiri na jinsi unavyoweza kuathiri mchakato wa ujauzito na uzazi kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya kibofu Cha nyongo

Saratani ya kibofu cha nyongo ni Saratani inayoanzia kwenye kibofu cha nyongo. Nyongo yako ni kiungo kidogo, chenye umbo la peari upande wa kulia wa tumbo lako, chini ya ini lako. Kibofu cha nyongo huhifadhi nyongo, Kioevu cha usaga

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
Kutetemeka kwa mikono au mwili bila sababu.

Kutetemeka (tremor) ni miondoko isiyo ya hiari ya sehemu yoyote ya mwili, kwa kawaida mikono, kichwa, au sauti, inayotokana na mikazo ya misuli ya mara kwa mara. Ingawa wengi huhisi ni tatizo la wazee pekee, linaweza kutokea kwa mtu yeyote na kwa sababu mbalimbali. Makala haya yanafafanua sababu za kutetemeka, kuanzia hali za kawaida za muda mfupi hadi changamoto za neva zinazohitaji matibabu.

Soma Zaidi...