Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

1. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo usababishwa na bakteria ambao uingia na kushambulia sehemu za ndani za kibofu Cha mkojo, bakteria hao wanaweza kutoka sehemu mbalimbali kama vile kwenye mkojo wenyewe ikiwa mkojo umekaa kwa mda mrefu bila kutolewa nje hao bakteria wanaweza kushambulia sehemu za ndani ya kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi kwenye kibofu Cha yanayoambatana na uvimbe.kwa hiyo ni lazima kukojoa tu baada ya kuhisi mkojo Ili kuepuka madhara ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

 

2. Kutumia sana ngono zembe yaani kujamiiana bila kutumia kondomu.

Hii ni mojawapo ya sababu ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa ya ngono ambapo bakteria kutoka kwa mtu Mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine ambaye Hana maambukizi na kusababisha kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kushambulia na kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hasa hasa kama bakteria hawa wasipotibiwa  mapema uweza kuleta madhara makubwa zaidi na kusababisha ugumba. Kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana.

 

3. Kuaribika kwa sehemu za kuchuja mkojo.

Wakati mwingine Kuna kuharibika kwa sehemu mbalimbali zinazohusika na kuchuja mkojo, kama vile figo, nephroni na sehemu zote kwa hiyo hali hii usababisha bakteria kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mkojo hauwezi kutoka kwa wakati au pengine kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, hali ambayo usababisha bakteria kuendelea kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo. Kwa hiyo tunapaswa kuangalia mfumo wote wa kibofu Cha mkojo.

 

4. Kutumia catheter kwa mda mrefu au mara kwa mara.

Hii ni sababu mojawapo ambayo ufanya kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, kwa sababu catheter inaweza kuharibu kwenye milija wa mkojo na kusababisha bakteria kuingia na kuleta madhara makubwa ambayo yanasababisha kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo inabidi catheter kuwepo kwa mda unaohitajika, mda isizidi Ili kuzuia maambukizi.kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuhakikisha kuwa catheter unatolewa kwa mda.

 

5. Wanawake wanaotumia uzazi wa mpango.

Wanawake wengi wanaoweka mipira kwaenye uke illi kuzuia  mimba isitungwe usababisha bakteria kupita na kuingia kwenye sehemu ya kibofu Cha mkojo na kuleta madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mipira hiyo uacha uwazi ambao usababisha bakteria kuweza kupita na kuzaliana huko na kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2805

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maambukizi ya H.pylori (Vidonda vya tumbo)
Maambukizi ya H.pylori (Vidonda vya tumbo)

Maambukizi ya H. pylori hutokea wakati aina ya bakteria inayoitwa Helicobacter pylori (H. pylori) inapoambukiza tumbo lako. Hii kawaida hutokea wakati wa utoto. Sababu ya kawaida ya Vidonda vya tumbo, maambukizi ya H. pylori yanaweza kuwa katika za

Soma Zaidi...
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.

Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.

Soma Zaidi...
   Dalili za madhara ya ini
Dalili za madhara ya ini

Ini Ni kiungo kikubwa Sana mwili na hutumika kuondoa sumu mwili ambayo hujulikana Kama detoxification

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Namna ya kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.

Posti hii inahusu zaidi njia zinazotumika ili kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.

Soma Zaidi...
MARADHI YA MOYO: KUPALALAIZI, PRESHA, SHAMBULIZI LA MOYO, Atherosclerosis;
MARADHI YA MOYO: KUPALALAIZI, PRESHA, SHAMBULIZI LA MOYO, Atherosclerosis;

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Halow samahan dokta nmekuwa nikiumwa tumbo muda mwingi takriban wiki ya 3 halipon naharisha kuna muda nikila chakula hata kama kdogo tu maumivu makali,je nifanyaje msaada
Halow samahan dokta nmekuwa nikiumwa tumbo muda mwingi takriban wiki ya 3 halipon naharisha kuna muda nikila chakula hata kama kdogo tu maumivu makali,je nifanyaje msaada

Mvurugiko katika mfumo wa chakula mwilinivunaweza kusababisha maumivu ya tumbo, kuharisha, kutapika na kuchoka pia. Lakini zipo sababu nyingine kama kuwana ujauzito. Nini ufanye endapo unasumbuliwana hali hii

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu
Madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu ni madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mgonjwa pale ambapo matibabu yanapokuwa hayatolewi kwa mgonjwa wa maumivu chini ya kitovu.

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka/hypotension
Presha ya kushuka/hypotension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka/ hypotension

Soma Zaidi...
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,

Soma Zaidi...
 Sababu za maumivu ya matiti na chuchu
Sababu za maumivu ya matiti na chuchu

Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako

Soma Zaidi...