Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini
Minyoo ni katika wadudu vimelea vinavyowapa shida watu wengi leo hii. Minyoo sio virusi wala bakteria kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakidhania.minyoo ipo katika makundi meengi na huishi katika maeneo mbalimbali kwenye miili yetu ikiwemo tumbo, ini, utumbo, ubongo na kwenye damu na maeneo mengine. Dalili za minyoo hutofautiana sana kulingana na aina ya minyoo na wapi ipo. Lakini zipo dalili zenye kufanana kwa minyoo wote. Katika makala hii nitakwenda kukujuza baadhi ya dalili za minyoo katika mwili wako, pia tutaona sababu za kupata minyoo, wapi minyoo inapatikana na vipi tutaizuia:-
Utaweza kupata minyoo katika hali zifuatazo:-
1.kula kitu kisichooshwa kwema kwa maji yaliyo safi na salama
2.Kunywa maji ambayo si masafi na si salama
3.Kula nyama ambayo haikuiva vyema, ama nyama mbichi
4.Kutembea pekupeku kwenye ardhi yeye minyoo
5.Kula udongo,
6.Kinyesi cha wanyama na binadamu
DALILI ZA MINYOO
Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote. Na dalili za minyoo pia hutofautiana sana, kulingana na aina za minyoo. Lakini zifuatazo ni katika dalili kuu:-
1.Kichefuchefu
2.Kukosa hamu ya kula
3.Maumivu ya tumbo
4.Kupungua uzito
5.Uchovu wa viungo
6.Kuona utelezi mwingi kama kamasi kwenye kinyesi
7.Kuona minyoo kwenye kinyesi.
8.Kuona damu kwenye kinyesi
9.Tumbo kujaa
Dalili hizi kama nilivyotangulia kusema kuwa zinatofautiana kulingana na aina ya minyoo. Sasa hebu tuone kwa ufupi dalili hizi kulingana na aina ya minyoo:-
1.minyoo aina na tapeworm dalili zao ni:
A.Kuvimba kwa ngozi ama kujaa ama kujaa kwa tumbo
B.Kuwa na alegi
C.Kuwa na homa
D.Matatizo katika mfumo wa fahamu, kama kifafa
2.minyoo aina ya hookworm dalili zao ni kama:-
A.Kuwashwa
B.Kupata ugonjwa wa anaemia (upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu) hivyo kukosa oksijeni ya kutosha mwilini
C.Kuwa na uchovu wa hali ya juu.
3.minyoo aina ya trichinosis, minyoo hawa wana dalili kama:-
A.Kupata homa
B.Kuvimba kwa uso
C.Maumivu ya misuli na kuchoka
D.Maumivu ya kichwa
E.Kutokupenda kupigwa na mwanga
F.Matatizo katika macho (conjuctivist)
NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO
Kwa kuwa tumekwisha kuona namna ambavyo minyoo huenezwa, hivyo basi ni rahisi sasa kutaja namna ya kubambana na minyoo. Njia hizo ni kama :-
1.usile chakula, nyama ana samaki ambaye hajapikwa vyema, ama kula nyama mbichi ama isiyoiva
2.Epuka kugusagusa nyama unapoandaa chakula chako, tenganisha nyama kivyake na vyakula vingine wakati unapoandaa kupika.
3.Safisha vyema vyembo ambavyo vimegusa nyama ambayo haikupikwa
4.Usile mimea ambayo inaishi ndani ya maji yabaridi
5.Usitembee miguu wazi kwenye maeneo machafu ambayo yana kinyesi
6.Safisha vyema kinyesi cha wanyama.
7.Hakikisha unapika vizuri nyama mpaka uhakikishe imewiva vyema,
8.Wanya kungβata kucha ama kunyonya vidole
9.Hakikisha unaosha kila unachokila kwa maji yaliyo safi na salama.
10.Usafi wa mwili, mavazi na mazingira ni muhimu kwa ajili ya kupambana na minyoo.
11.Kuwacha kabisa kula udongo
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.
Soma Zaidi...Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Je umeshawahi kujiukiza kuwa, dawa ya P2 ni kweli inaweza kuzuia mimba, ukifanya mapenzi siku hatari?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.
Soma Zaidi...