Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa Mama akimaliza kujifungua utokwa na damu kidogo tu na ya kawaida ila Kuna kipindi Mama anatokwa na damu nyingi sana hali inayosababisha matatizo makubwa kwa Mama kama huduma haijatolewa.kuna aina mbili za kutokwa na damu aina ya kwanza ni Ile Mama anatokwa na damu pindi tu anapomaliza kujifungua na mara nyingine Mama anatokwa na damu baada ya Masaa ishilini na manne Hadi wiki sita.
2. Sababu ya kwanza ya Mama kutokwa na damu ni pale mfuko wa kizazi unaposhindwa kisinyaa,kwa asilimia sabini wanawake wanaopatwa na tatizo hili ni kwa sababu ya mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa kwa sababu Ile sehemu inayokuwa imeshikikia plasenta kwa kawaida uwa na mirija inayokuwa inasafirisha chakula kwa mtoto, kwa hiyo baada ya kujifungua mfuko wa kizazi unapaswa kusinyaa Ili kuweza kufunika Ile sehemu ya mishipa ya damu isiendelee kutoa damu, kwa hiyo mfuko wa uzazi usipofunga Ile mishipa uendelea kutoa damu hali inayosababisha kuendelea kuvuja kwa damu nyingi baada ya kujifungua.
3. Kubakizwa baadhi ya vipande vya plasenta au kondo la nyuma kwenye mfuko wa kizazi.
Kwa kawaida tunafahamu kuwa baada ya mtoto kutoka kifuatacho ni kondo la nyuma, na kondo hilo huwa Lina visehemu vyake ambavyo kwa lugha ya kitaalamu huitwa lobe, kwa kawaida hizo lobe uanzia kumi na Saba mpaka ishilini na ikitokea wakati mama anajifungua akabaki sehemu yoyote ya lobe usababisha Mama kutoa damu nyingi baada ya kujifungua. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangalia hizo lobe na kuzitoa vizuri Ili kuepukana kuvuja kwa damu.
4. Pengine Mama anakuwa na kovu kwenye sehemu yoyote ya mfuko wa kizazi, au pengine anakuwa amepasuka kwa ndani, hasa hasa akina Mama wanapojifungua kwa mara ya kwanza wanakuwa wamepasuka kwa sababu njia bado ni ndogo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuangalia sehemu iliyochanika na kuishona Ili kuweza kuepuka tatizo la kuvuja kwa damu baada ya kujifungua. Au pengine akina Mama wanakunywa dawa za kuongeza uchungu hali inayosababisha kuwepo kwa uchungu mwingi na njia bado inakuwa imefungwa kwa hiyo Mama ulazimisha kusukuma na kusababisha kuchanika sana sehemu za Siri na kusababisha damu kuvuja sana
5. Tatizo la damu kushindwa kuganda.
Kama tulivyotangulia kusema kwamba, mtoto anapokuwa tumboni upata chakula chake kupitia kondo la nyuma na kondo hilo huwa Lina mirija ya damu na pindi mtoto akizaliwa kondo la nyuma nalo utoka, lakini sehemu ya kondo la nyuma lilipotoka Kuna mishipa ya damu uendelea kutoa damu, Ili mishipa hiyo iache kutoa damu ni lazima mfuko wa kizazi kusinyaa na kufunika sehemu hiyo na pengine kunapaswa kuwepo na vitu vinavyosababisha damu kuganda kwa hiyo Kuna wanawake wengine hawana madini ya kusababisha damu kuganda hali inayosababisha damu kuendelea kutoka kwa wingi.
6. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujua kwamba tatizo hili la kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua ni hatari na kama hakuna uangalizi mzuri Mama anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo ni wito wangu kwamba akina Mama wote wanapaswa kujifungua hospital Ili kama Kuna matatizo kama haya ni vizuri kudili nayo hospital kuliko vijijini, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa elimu kuhusu jambo hili Ili wote kwa ujumla tuweze kutokomeza vifo vya akina Mama pindi wanapojifungua.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.
Soma Zaidi...Zijuwe dalili 17 za mimba na mimba changa, kuanzia siku ya kwanza mpaka mwezi mmoja
Soma Zaidi...Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?
Soma Zaidi...Mdau anauliza ni muda gani mwanamke anaweza kujijuwa kuwa amepata ujauzito.
Soma Zaidi...Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma kwa mtoto mwenye shida ya kupumua, mtoto kama ana shida ya kupumua tunaangalia dalili kwanza na baadaye tunaweza kutoa huduma kulingana na Dalili.
Soma Zaidi...Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka.
Soma Zaidi...Je anapatwa maumivu Γ°ΕΈΛΒ makali wakati wa tendo la ndoa ama ukiwa katika hedhi? Soma makala hii hadi mwisho
Soma Zaidi...