Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.


image


Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.


Sababu za Mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa Mama akimaliza kujifungua utokwa na damu kidogo tu na ya kawaida ila Kuna kipindi Mama anatokwa na damu nyingi sana hali inayosababisha matatizo makubwa kwa Mama kama huduma haijatolewa.kuna aina mbili za kutokwa na damu aina ya kwanza ni Ile Mama anatokwa na damu pindi tu anapomaliza kujifungua na mara nyingine Mama anatokwa na damu baada ya Masaa ishilini na manne Hadi wiki sita.

 

2. Sababu ya kwanza ya Mama kutokwa na damu ni pale mfuko wa kizazi unaposhindwa kisinyaa,kwa asilimia sabini wanawake wanaopatwa na tatizo hili ni kwa sababu ya mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa kwa sababu Ile sehemu inayokuwa imeshikikia plasenta kwa kawaida uwa na mirija inayokuwa inasafirisha chakula kwa mtoto, kwa hiyo baada ya kujifungua mfuko wa kizazi unapaswa kusinyaa Ili kuweza kufunika Ile sehemu ya mishipa ya damu isiendelee kutoa damu, kwa hiyo mfuko wa uzazi usipofunga Ile mishipa uendelea kutoa damu hali inayosababisha kuendelea kuvuja kwa damu nyingi baada ya kujifungua.

 

3. Kubakizwa baadhi ya vipande vya plasenta au kondo la nyuma kwenye mfuko wa kizazi.

Kwa kawaida tunafahamu kuwa baada ya mtoto kutoka kifuatacho ni kondo la nyuma, na kondo hilo huwa Lina visehemu vyake ambavyo kwa lugha ya kitaalamu huitwa lobe, kwa kawaida hizo lobe uanzia kumi na Saba mpaka ishilini na ikitokea wakati mama anajifungua akabaki sehemu yoyote ya lobe usababisha Mama kutoa damu nyingi baada ya kujifungua. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangalia hizo lobe na kuzitoa vizuri Ili kuepukana kuvuja kwa damu.

 

4. Pengine Mama anakuwa na kovu kwenye sehemu yoyote ya mfuko wa kizazi, au pengine anakuwa amepasuka kwa ndani, hasa hasa akina Mama wanapojifungua kwa mara ya kwanza wanakuwa wamepasuka kwa sababu njia bado ni ndogo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuangalia sehemu iliyochanika na kuishona Ili kuweza kuepuka tatizo la kuvuja kwa damu baada ya kujifungua. Au pengine akina Mama wanakunywa dawa za kuongeza uchungu hali inayosababisha kuwepo kwa uchungu mwingi na njia bado inakuwa imefungwa kwa hiyo Mama ulazimisha kusukuma na kusababisha kuchanika sana sehemu za Siri na kusababisha damu kuvuja sana 

 

5. Tatizo la damu kushindwa kuganda.

Kama tulivyotangulia kusema kwamba, mtoto anapokuwa tumboni upata chakula chake kupitia kondo la nyuma na kondo hilo huwa Lina mirija ya damu na pindi mtoto akizaliwa kondo la nyuma nalo utoka, lakini sehemu ya kondo la nyuma lilipotoka Kuna mishipa ya damu uendelea kutoa damu, Ili mishipa hiyo iache kutoa damu ni lazima mfuko wa kizazi kusinyaa na kufunika sehemu hiyo na pengine kunapaswa kuwepo na vitu vinavyosababisha damu kuganda kwa hiyo Kuna wanawake wengine hawana madini ya kusababisha damu kuganda hali inayosababisha damu kuendelea kutoka kwa wingi.

 

6. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujua kwamba tatizo hili la kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua ni hatari na kama hakuna uangalizi mzuri Mama anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo ni wito wangu kwamba akina Mama wote wanapaswa kujifungua hospital Ili kama Kuna matatizo kama haya ni vizuri kudili nayo hospital kuliko vijijini, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa elimu kuhusu jambo hili Ili wote kwa ujumla tuweze kutokomeza vifo vya akina Mama pindi wanapojifungua.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali. Soma Zaidi...

image Madhara ya fangasi ukeni
Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke. Soma Zaidi...

image Madhara ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto. Soma Zaidi...

image tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba
Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi? Soma Zaidi...

image Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula. Soma Zaidi...

image Changamoto za ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu Soma Zaidi...

image Kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren. Soma Zaidi...

image Ujue Ute kwenye uke
Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kupata mtoto wa kiume
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume. Soma Zaidi...