SABABU ZA MAMA KUTOKWA NA DAMU NYINGI BAADA YA KUJIFUNGUA.


image


Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.


Sababu za Mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa Mama akimaliza kujifungua utokwa na damu kidogo tu na ya kawaida ila Kuna kipindi Mama anatokwa na damu nyingi sana hali inayosababisha matatizo makubwa kwa Mama kama huduma haijatolewa.kuna aina mbili za kutokwa na damu aina ya kwanza ni Ile Mama anatokwa na damu pindi tu anapomaliza kujifungua na mara nyingine Mama anatokwa na damu baada ya Masaa ishilini na manne Hadi wiki sita.

 

2. Sababu ya kwanza ya Mama kutokwa na damu ni pale mfuko wa kizazi unaposhindwa kisinyaa,kwa asilimia sabini wanawake wanaopatwa na tatizo hili ni kwa sababu ya mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa kwa sababu Ile sehemu inayokuwa imeshikikia plasenta kwa kawaida uwa na mirija inayokuwa inasafirisha chakula kwa mtoto, kwa hiyo baada ya kujifungua mfuko wa kizazi unapaswa kusinyaa Ili kuweza kufunika Ile sehemu ya mishipa ya damu isiendelee kutoa damu, kwa hiyo mfuko wa uzazi usipofunga Ile mishipa uendelea kutoa damu hali inayosababisha kuendelea kuvuja kwa damu nyingi baada ya kujifungua.

 

3. Kubakizwa baadhi ya vipande vya plasenta au kondo la nyuma kwenye mfuko wa kizazi.

Kwa kawaida tunafahamu kuwa baada ya mtoto kutoka kifuatacho ni kondo la nyuma, na kondo hilo huwa Lina visehemu vyake ambavyo kwa lugha ya kitaalamu huitwa lobe, kwa kawaida hizo lobe uanzia kumi na Saba mpaka ishilini na ikitokea wakati mama anajifungua akabaki sehemu yoyote ya lobe usababisha Mama kutoa damu nyingi baada ya kujifungua. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangalia hizo lobe na kuzitoa vizuri Ili kuepukana kuvuja kwa damu.

 

4. Pengine Mama anakuwa na kovu kwenye sehemu yoyote ya mfuko wa kizazi, au pengine anakuwa amepasuka kwa ndani, hasa hasa akina Mama wanapojifungua kwa mara ya kwanza wanakuwa wamepasuka kwa sababu njia bado ni ndogo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuangalia sehemu iliyochanika na kuishona Ili kuweza kuepuka tatizo la kuvuja kwa damu baada ya kujifungua. Au pengine akina Mama wanakunywa dawa za kuongeza uchungu hali inayosababisha kuwepo kwa uchungu mwingi na njia bado inakuwa imefungwa kwa hiyo Mama ulazimisha kusukuma na kusababisha kuchanika sana sehemu za Siri na kusababisha damu kuvuja sana 

 

5. Tatizo la damu kushindwa kuganda.

Kama tulivyotangulia kusema kwamba, mtoto anapokuwa tumboni upata chakula chake kupitia kondo la nyuma na kondo hilo huwa Lina mirija ya damu na pindi mtoto akizaliwa kondo la nyuma nalo utoka, lakini sehemu ya kondo la nyuma lilipotoka Kuna mishipa ya damu uendelea kutoa damu, Ili mishipa hiyo iache kutoa damu ni lazima mfuko wa kizazi kusinyaa na kufunika sehemu hiyo na pengine kunapaswa kuwepo na vitu vinavyosababisha damu kuganda kwa hiyo Kuna wanawake wengine hawana madini ya kusababisha damu kuganda hali inayosababisha damu kuendelea kutoka kwa wingi.

 

6. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kujua kwamba tatizo hili la kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua ni hatari na kama hakuna uangalizi mzuri Mama anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo ni wito wangu kwamba akina Mama wote wanapaswa kujifungua hospital Ili kama Kuna matatizo kama haya ni vizuri kudili nayo hospital kuliko vijijini, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa elimu kuhusu jambo hili Ili wote kwa ujumla tuweze kutokomeza vifo vya akina Mama pindi wanapojifungua.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Hadiythi za alif lela u lela    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito faida na hasara zake Soma Zaidi...

image Zijue sababu zinazosababisha kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume
Kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume kunamaanisha kuwa Majimaji (shahawa) unayotoa wakati wa kufika kileleni huwa na mbegu chache kuliko kawaida. Hesabu yako ya manii inachukuliwa kuwa chini kuliko kawaida ikiwa una chini ya mbegu milioni 15. Kuwa na idadi ndogo ya manii hupunguza uwezekano kwamba moja ya manii yako itarutubisha yai la mwenza wako, na hivyo kusababisha mimba. Hata hivyo, wanaume wengi ambao wana idadi ndogo ya manii bado wanaweza kuzaa mtoto. Soma Zaidi...

image Dalili ninazoziona kwangu chuchu zinauma na sjapata period mwezi huu na nlishiriki tarehe 19 mwezi wa tisa
Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu. Soma Zaidi...

image Sababu za kutangulia kwa kitovu wakati Mtoto anazaliwa
Posti hii inahusu zaidi sababu za kutangulia kwa kitovu wakati wa mtoto anapozaliwa. Soma Zaidi...

image Mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo yanayopunguza nguvu za kiume Soma Zaidi...

image Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa
Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye Soma Zaidi...

image Chanzo cha tatizo la mvurugiko wa hedhi.
Posti hii inahusu zaidi chanzo cha mvurugiko wa hedhi, Kuna kipindi hedhi uvurugika kabisa, pengine unaweza kupata hedhi mara mbili kwa mwezi au kukosa au pengine siku kuwa zaidi ya tano mpaka Saba au kuwa chache, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali tutakavyoona hapo mbeleni. Soma Zaidi...

image Mimi ni mama ninaye nyonyesha toka nimejefunguwa sijawai kuziona siku zangu lakini nilipo choma sindano za yutiai nikaaza kutokwa na tamu kama siku tano na mwanangu ana mwaka moja je ninahatali ya kubeba mimba
Kunyonyesha ni moja katika njia za asili za kuzuia upatikanaji wa miba nyingine. Hata hivyo hii haimaanishi kuwa huwezi kupata mimba ukiwa unavyonyesha. Soma Zaidi...

image Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali. Soma Zaidi...

image Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha Soma Zaidi...