image

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

Njoo ujifunze vyakula vya kuboresha mbegu za kiume na nguvu za kiume.

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

VYAKULA VYA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME




Ugumba si kwa wanawake tu, wapo hata wanaume wanatatizo hili. Lakini kutokubebesha mimba ama kubeba mimba pekee haimaanishi kuwa wewe ni mgumba. Mwanaume kumbebesha mimba mwanamke kunategemea mambo mengi kutoka kwa mwanaume mwenyewe na kwa mwanamke mwenyewe. Katika makala hii nitazungumzia kipengele kimoja tu nacho ni tatizo la kutokuwa na mbegu bora za kiume.



Mwnaume anapokojoa bao moja anatoa mbegu zaidi ya milioni 300. katika mbegu hizo ni moja tu ndiyo intakayofanikiwa kitungisha mimba. Mamimioni ya mbegu haya yanakufa bila hata ya kulifikia yai, kutokana na udhaifu wao, kutoweza kuogelea vyema, ukali wa tindikali katika tumbo la mwanamke n.k. sasa ili mwanaume aweze kubebesha ujauzito anatakiwa atoe mbegu bora na imara zinazoweza kuishi ndani ya tumbo la mimba kwa muda mrefu.



Inatokea baadhi ya wanaume mbegu zao zinakuwa sio imara kutosheleza. Hii inakuwa ni ngumu kubebesha ujauzito. Lakini kumbuka kama mambo mengine yakiwa sawa hata mwenye mbegu dhaifu inaweza kubebesha mimba endapo itakuwa ni siku sahihi ya kukutana na yai, hazitachukuwa muda kukutana na yai ama zilitolewa nyingi.



Sasa ikiwa tatizo ni hili la mbegu ni dhaifu, je nitawezaje kuboresha mbegu zangu? Yes ni swali zuri sana, na inapasa hasa kulijuwa jibu lake. Mbegu utaweza kuziporesha kwa kubadilisha mlo ama kutumia dawa ama njia nyinginezo. Miongoni mwa njia hizo ni:-



Njia za kuboresha mbegu za kiume.
1.Badili mlo wako.
Muonekano wako leo ni sawa na chakula unachokila. Ladha na ubora wa manii na mbegu za kiume pia hutegemeana na unachokila. Kama unataka kuboresha mbegu za kiume kwanza anza na kubadili mlo wako. Jitahidi kula vyakula vifuatavyo:-



A.Vitamini B-12
Vitamini hivi unaweza kuvipata kwenye nyama, samaki na maziwa. Vitamini hivi husaidia sana katika afya ya mbegu za kiume.



B.Vitamini C
Hivi unaweza kuvipata kwenye machungwa, viaz mbatatai, nyanya, apinach na kwenye matunda yenye uchachu na mapapai na mananasi. Vitamini C pia ni muhumu kwa afya ya mfumo wa kinga



C.Kula vyakula jamii ya korosho na karanga



D.Kula vyakula vyenye lycopene. Vyakula hivi kuwa na rangi nyekundu kama tikiti na nyanya



E.Kula vyakula vyenye madini ya zinc kwa wingi. Unaweza kupata madini haya kwenye nyama, samaki wa baharini kwenye magobeta jamii ya kaa, mimea jamii ya kunde, kula mbegu kama mbegu za maboga na nyingine, maziwa, mayai, jamii ya korosho, baadhi ya mboga za majani kama maharagwe ya kijani na nafaka nzima.



2.Fanya mazoezi ya mara kwa mara.
Mazoezi si kwa ajuli ya hili tu bali pia ni kwa ajili ya kuboresha afya kwa ujumla. Si lazima ufanye mazoezi mareefu, hapana kwa uchache pia inatosha.



3.Punguza kuvaa nguo za ndani zenye joto.
Afya ya mbegu za kiume inategemea pia joto la mwili wako. Hakikisha korodani unazipa hewa ya kutosha. Usivae nguo za kubana nyingi kama chupi, si salama kwa wanaume. Boxa kama haibani sana inatosha.



4.Punguza unywaji wa pombe, na soda kama unakunywa kwa kiasi kikubwa.





                   







           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2099


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo chini ya umri wa miaka mitano ili kuweza kuweka afya yake kwenye njia safi. Soma Zaidi...

Namna ya kutunza joto la mtoto mara tu baada ya kuzaliwa.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kutunza joto la mtoto mara tu anapozaliwa,tunajuwa wazi kuwa Mama anaweza kujifungulia sehemu yoyote ile kabla hajafika hospitalini kwa hiyo mtoto anapaswa kuwa na joto la mwili la kutosha i Soma Zaidi...

mim ninaujauzito wa mwezi mmoja lakini naona kama hali fulani ya damu inanitoka sehemu ya Siri inafanana na damu ya wakati wa period
Kutokuwa na damu wakati wa ujauzito ni hali uliyo ya kawida lakini inapaswa kujuwa sifa za damu hiyo nabje unatoka kwa namna gani. Kama unasumbuliwa na tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

Mambo yanayopelekea ugumba.
Post huu inahusu zaidi mambo yanayopelekea ugumba kwa wanaume, ni mambo ambayo uchangia au upelekea mwanaume kukosa uzazi. Soma Zaidi...

Faida za Uzazi wa mpango
Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA. Soma Zaidi...

DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI
Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho. Soma Zaidi...

Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua. Soma Zaidi...

Mimba kutoka kabla ya umri wake
Posti hii inahusu zaidi kuhusu kwa mimba kutoka kabla ya mda wake,ni kitendo ambacho mimba utoka kabla ya wiki ishilini na na nane. Soma Zaidi...

Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito Soma Zaidi...

Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa kisukari wakati wa ujauzito.
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito. Soma Zaidi...

Madhara ya kupungua kwa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa homoni ya projestron ikipungua mwilini na pia kuweza kutambua dalili za kupungua kwa homoni hii ya progesterone. Soma Zaidi...