picha

Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.

Mama mjamzito akiona Dalili zifuatazo awahi kituo Cha afya

1.kutokwa na Damu ukweni.

2.mtoto Kupunguza au kuacha kucheza tumboni.

3.maumivu makali ya tumbo.

4.maumivu makali ya kichwa.

5.kushindwa kuona vizuri.

6.kutokwa na majimaji ukweni.

7.Homa Kali.

 

Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.

1.Aanze kliniki ya ujauzito pale tu atakapojihisi ana mimba.

2.Ahudhurie mahudhurio ya kliniki yote nane.

3.ajifungulie katika kituo Cha huduma ya afya.

4.ahudhurie kliniki baada ya kujifungua Ndani ya siku tatu, baada ya siku ishirini na nane na baada ya siku Arobaini na mbili 42.

5.mama mjamzito anahitaji kula vyakula vyenye virutubisho vya kutosha ili aweze kukidhi mahitaji yake ya kilishe ya kila siku pamoja na Mtoto aliye tumboni.

6.anahitaji kula mlo kamili wenye mchanganyiko kutoka katika makundi matano vinavyopatikana katika jamii ya maziwa, matunda na mbogamboga, nyama,mayai,nafaka na jamii ya kunde.

7.mama anaye nyonyesha ana uhitaji mkubwa wa virutubisho kwaajili yake mwenyewe na kutengeneza maziwa kwa ajili ya mtoto, hivyo anapaswa kula Milo mingi kuliko Kawaida ili kukidhi ongezeko la mahitaji kwa ukuaji wa Mtoto.

8.mama mjamzito anapaswa kula Milo mitatu ya vyakula mchanganyiko na Milo miwili ya ziada kila siku ili kuimarisha Hali yake ya lishe na kuimarisha lishe ya mtoto anaye nyonya.

9.mama amnyonyeshe Mtoto Mara tu anapojifungua (Ndani ya saa moja)

10.mama asimpatie Mtoto chakula au kinywaji kingine chochote au maji mpaka atimize miezi sita

11.mama amwanzishie Mtoto vyakula vya nyongeza Mara anapotimiza miezi sita huku akiendelea kunyonya.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/11/Tuesday - 12:13:18 am Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1669

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 web hosting    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰6 ai web app   

Post zinazofanana:

Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.

Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea

Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa

Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.

Soma Zaidi...
Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.

Soma Zaidi...