Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Mama mjamzito akiona Dalili zifuatazo awahi kituo Cha afya
1.kutokwa na Damu ukweni.
2.mtoto Kupunguza au kuacha kucheza tumboni.
3.maumivu makali ya tumbo.
4.maumivu makali ya kichwa.
5.kushindwa kuona vizuri.
6.kutokwa na majimaji ukweni.
7.Homa Kali.
Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
1.Aanze kliniki ya ujauzito pale tu atakapojihisi ana mimba.
2.Ahudhurie mahudhurio ya kliniki yote nane.
3.ajifungulie katika kituo Cha huduma ya afya.
4.ahudhurie kliniki baada ya kujifungua Ndani ya siku tatu, baada ya siku ishirini na nane na baada ya siku Arobaini na mbili 42.
5.mama mjamzito anahitaji kula vyakula vyenye virutubisho vya kutosha ili aweze kukidhi mahitaji yake ya kilishe ya kila siku pamoja na Mtoto aliye tumboni.
6.anahitaji kula mlo kamili wenye mchanganyiko kutoka katika makundi matano vinavyopatikana katika jamii ya maziwa, matunda na mbogamboga, nyama,mayai,nafaka na jamii ya kunde.
7.mama anaye nyonyesha ana uhitaji mkubwa wa virutubisho kwaajili yake mwenyewe na kutengeneza maziwa kwa ajili ya mtoto, hivyo anapaswa kula Milo mingi kuliko Kawaida ili kukidhi ongezeko la mahitaji kwa ukuaji wa Mtoto.
8.mama mjamzito anapaswa kula Milo mitatu ya vyakula mchanganyiko na Milo miwili ya ziada kila siku ili kuimarisha Hali yake ya lishe na kuimarisha lishe ya mtoto anaye nyonya.
9.mama amnyonyeshe Mtoto Mara tu anapojifungua (Ndani ya saa moja)
10.mama asimpatie Mtoto chakula au kinywaji kingine chochote au maji mpaka atimize miezi sita
11.mama amwanzishie Mtoto vyakula vya nyongeza Mara anapotimiza miezi sita huku akiendelea kunyonya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Habari Mimi ni mjamzito was miezi Tisa sasa nimeanza kutokwa na maji kidogo kidogo ukeni bila uchungu na no mimba yangu ya kwanza he Kuna shida?
Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni.
Soma Zaidi...Kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki tendo la ndoa wakati wa ujauzito faida na hasara zake
Soma Zaidi...DARASA LA AFYA NA AFYA YA UZAZI
Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho.
Soma Zaidi...Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba
Soma Zaidi...Faida za Uzazi wa mpango
Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA.
Soma Zaidi...Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...