picha

Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.

Mama mjamzito akiona Dalili zifuatazo awahi kituo Cha afya

1.kutokwa na Damu ukweni.

2.mtoto Kupunguza au kuacha kucheza tumboni.

3.maumivu makali ya tumbo.

4.maumivu makali ya kichwa.

5.kushindwa kuona vizuri.

6.kutokwa na majimaji ukweni.

7.Homa Kali.

 

Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.

1.Aanze kliniki ya ujauzito pale tu atakapojihisi ana mimba.

2.Ahudhurie mahudhurio ya kliniki yote nane.

3.ajifungulie katika kituo Cha huduma ya afya.

4.ahudhurie kliniki baada ya kujifungua Ndani ya siku tatu, baada ya siku ishirini na nane na baada ya siku Arobaini na mbili 42.

5.mama mjamzito anahitaji kula vyakula vyenye virutubisho vya kutosha ili aweze kukidhi mahitaji yake ya kilishe ya kila siku pamoja na Mtoto aliye tumboni.

6.anahitaji kula mlo kamili wenye mchanganyiko kutoka katika makundi matano vinavyopatikana katika jamii ya maziwa, matunda na mbogamboga, nyama,mayai,nafaka na jamii ya kunde.

7.mama anaye nyonyesha ana uhitaji mkubwa wa virutubisho kwaajili yake mwenyewe na kutengeneza maziwa kwa ajili ya mtoto, hivyo anapaswa kula Milo mingi kuliko Kawaida ili kukidhi ongezeko la mahitaji kwa ukuaji wa Mtoto.

8.mama mjamzito anapaswa kula Milo mitatu ya vyakula mchanganyiko na Milo miwili ya ziada kila siku ili kuimarisha Hali yake ya lishe na kuimarisha lishe ya mtoto anaye nyonya.

9.mama amnyonyeshe Mtoto Mara tu anapojifungua (Ndani ya saa moja)

10.mama asimpatie Mtoto chakula au kinywaji kingine chochote au maji mpaka atimize miezi sita

11.mama amwanzishie Mtoto vyakula vya nyongeza Mara anapotimiza miezi sita huku akiendelea kunyonya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1886

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Njia za kuzuia ugumba

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia ugumba, ni njia ambazo utumiwa na wapenzi ambao wameshindwa kupata watoto hasa kwa wale ambao wamezaliwa wakiwa na uwezo wa kupata watoto lakini kwa sababu tofauti tofauti wanashindwa kupata watoto kwa hiyo njia zifu

Soma Zaidi...
UTI na ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI kwa wajawazito

Soma Zaidi...
Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Soma Zaidi...
Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho

Wajawazito wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiungulia, makala hii itakujulisha njia za kukabiliana na kiungulia, dalili zake na dawa zake

Soma Zaidi...
Mambo ambayo mama anapaswa kujua akiwa mjamzito

Posti hii inahusu zaidi mambo anyopaswa kujua akiwa mjamzito. Ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa mama akiwa mjamzito.

Soma Zaidi...
Nimetoka kufanya tendo la ndoa ghafla tumbo likaanza kukaza upande wa kushoto na kutoka maji yenye uzito wa kawaida kama ute mengi je hii itakuwa ni nini

Maumivu yavtumbo huwenda yakachanganya sana, Keane yanahusianana sababu nyingi sana. Kina baadhi ya watu hupata na maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa ama punde tu baada ya kumaliza.

Soma Zaidi...