Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Mama mjamzito akiona Dalili zifuatazo awahi kituo Cha afya
1.kutokwa na Damu ukweni.
2.mtoto Kupunguza au kuacha kucheza tumboni.
3.maumivu makali ya tumbo.
4.maumivu makali ya kichwa.
5.kushindwa kuona vizuri.
6.kutokwa na majimaji ukweni.
7.Homa Kali.
Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
1.Aanze kliniki ya ujauzito pale tu atakapojihisi ana mimba.
2.Ahudhurie mahudhurio ya kliniki yote nane.
3.ajifungulie katika kituo Cha huduma ya afya.
4.ahudhurie kliniki baada ya kujifungua Ndani ya siku tatu, baada ya siku ishirini na nane na baada ya siku Arobaini na mbili 42.
5.mama mjamzito anahitaji kula vyakula vyenye virutubisho vya kutosha ili aweze kukidhi mahitaji yake ya kilishe ya kila siku pamoja na Mtoto aliye tumboni.
6.anahitaji kula mlo kamili wenye mchanganyiko kutoka katika makundi matano vinavyopatikana katika jamii ya maziwa, matunda na mbogamboga, nyama,mayai,nafaka na jamii ya kunde.
7.mama anaye nyonyesha ana uhitaji mkubwa wa virutubisho kwaajili yake mwenyewe na kutengeneza maziwa kwa ajili ya mtoto, hivyo anapaswa kula Milo mingi kuliko Kawaida ili kukidhi ongezeko la mahitaji kwa ukuaji wa Mtoto.
8.mama mjamzito anapaswa kula Milo mitatu ya vyakula mchanganyiko na Milo miwili ya ziada kila siku ili kuimarisha Hali yake ya lishe na kuimarisha lishe ya mtoto anaye nyonya.
9.mama amnyonyeshe Mtoto Mara tu anapojifungua (Ndani ya saa moja)
10.mama asimpatie Mtoto chakula au kinywaji kingine chochote au maji mpaka atimize miezi sita
11.mama amwanzishie Mtoto vyakula vya nyongeza Mara anapotimiza miezi sita huku akiendelea kunyonya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kama na wewe unasumbuliwa na hali ya kupitiliza siku zako post hii itakusaidia.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal
Soma Zaidi...PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada.
Soma Zaidi...Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuongezeka uzito kwa wajawazito, Mara nyingi Mama akibeba mimba uongezeka uzito kutoka wiki ya Kwanza mpaka wiki ya mwisho ya kujifungua.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia vidonge vya uzazi wa mpango kwa akina dada.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Soma Zaidi...