SQL somo la 15: Jinsi ya kutumia sql function kwenye mysql
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function kwenye sql na jinsi ya kuzitumia.
Katika somo letu hili tutakwenda kufanya mabadiliko kadhaa kwenye database yetu. Hapa tunakwenda kuongeza column ya jina la baba, pia tutaongeza column ya masomo mawili, na ile ya alama tutaibadilisha kuwa somo. hivyo table yetu itakuwa na column hizi:-
- id
- jina_la_kwanza
- jina_la_pili
- kusoma
- kuhesabu
- kuandika
kisha weka data kadhaa kama nilivyoweka mimi. angalia picha hapo chini
kufikia hapo utakuw aupo tayari kwa ajili ya somo. kabla hatujaendelea na somo kwanz anikukumbuse kuwa tayari tulisajifunza baadhi ya function kwenye masomo yaliopita kama:-
- COUNT()
- AVG()
- SUM()
- MAX()
- MIN()
Katika somo hili tutaendelea kuangalia function nyingineze. Nikukumbushe tu kwanza sql ina mamia fu functions ambazo hatunazizungumzia. hivyo pitaia link hii https://www.w3schools.com/sql/sql_ref_mysql.asp utaweza kusoma function nyingi.
jinsi ya kuunganisha column
Yaani ipo hivi, hapo kwenye column tuna jina la kwanza na jina la pili, ambapo la kwanza ni la mtoto na la pili ni la baba. sasa tunataka watai kwa kusoma hizo column 2 tuzisome kama moja, hivyo basi itatubidi tuziunganishe.
kufanya hivyo tutatumia concat() ambapo ndani yake utaweka hizo column kwa kuzitenganisha na alama ya koma.
Mfano
SELECT concat(jina_la_kwanza, jina_la_pili) as jina FROM majibu;
sasa hapo kuna changamoto tunatakiwa tuzitatue. unaona hapo majina yamebanana, sasa tunataka kuyatengenisha. Ndani ya function ya concat unaweza pia kuunganisha kwa kuweka vitu vingine. Hivyo nitaongeza empty space kwa kutumia (“ “)
SELECT concat(jina_la_kwanza, " ", jina_la_pili) as jina FROM majibu;
Angalau hapo utaona jina la kwanza na la pili vimeachana kitogo.
Kuweka herufi kubwa au ndogo
Wakati mwingine utataka majina yawe katika format moja tu, kwa mfano kama yote yawe na herufi kubwa tupu ama ndogo tupu. Kuwa herufi kubwa utatumia UPPER() na kuwa herufi ndogo utatumia LOWER(). Ndani ya function utaweka jina la column unayotaka data zake ziwe katika herufi kubwa ama nogo.
Mfano:
SELECT concat(UPPER(jina_la_kwanza), " ", UPPER(jina_la_pili)) as jina FROM majibu;
Hivyo hivyo kuwa herufi ndogo utatumia LOWER()
SELECT concat(LOWER(jina_la_kwanza), " ", LOWER(jina_la_pili)) as jina FROM majibu;
Kusoma data bila ya kujirudia
Cukulia mfano una table ina zaidi ya data 10000, sasa uataka...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
SQL - MySQL somo la 9: Jinsi ya kusoma data kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database. Pia utajifunza jinsi ya ku limit kiasi cha data ambazo zitaonekana.
Soma Zaidi...Database somo la 26: Baadhi ya function za SQL ambayo hutumika kubadili data
Function hizi ni muhimu katika kubadili data kabla ya kuzionyesha. Hii ni muhimu ili kupata structure maalum ya data.
Soma Zaidi...SQL -MySQL somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye Mysql Database
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za data zinazotumika kwenye mysql database
Soma Zaidi...SQL - somo la 13: Jinsi ya kutumia CASE kwenye SQL
katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutumia case kwenye databse ili kuchakata taarifa za matokeo
Soma Zaidi...Database seomo la 21: Constraints kwenye Database
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 7: Jinsi ya kubadili jina table na column kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili jina la table na jina la column kwenye mysql database.
Soma Zaidi...