Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function kwenye sql na jinsi ya kuzitumia.
Katika somo letu hili tutakwenda kufanya mabadiliko kadhaa kwenye database yetu. Hapa tunakwenda kuongeza column ya jina la baba, pia tutaongeza column ya masomo mawili, na ile ya alama tutaibadilisha kuwa somo. hivyo table yetu itakuwa na column hizi:-
kisha weka data kadhaa kama nilivyoweka mimi. angalia picha hapo chini
kufikia hapo utakuw aupo tayari kwa ajili ya somo. kabla hatujaendelea na somo kwanz anikukumbuse kuwa tayari tulisajifunza baadhi ya function kwenye masomo yaliopita kama:-
Katika somo hili tutaendelea kuangalia function nyingineze. Nikukumbushe tu kwanza sql ina mamia fu functions ambazo hatunazizungumzia. hivyo pitaia link hii https://www.w3schools.com/sql/sql_ref_mysql.asp utaweza kusoma function nyingi.
jinsi ya kuunganisha column
Yaani ipo hivi, hapo kwenye column tuna jina la kwanza na jina la pili, ambapo la kwanza ni la mtoto na la pili ni la baba. sasa tunataka watai kwa kusoma hizo column 2 tuzisome kama moja, hivyo basi itatubidi tuziunganishe.
kufanya hivyo tutatumia concat() ambapo ndani yake utaweka hizo column kwa kuzitenganisha na alama ya koma.
Mfano
SELECT concat(jina_la_kwanza, jina_la_pili) as jina FROM majibu;
sasa hapo kuna changamoto tunatakiwa tuzitatue. unaona hapo majina yamebanana, sasa tunataka kuyatengenisha. Ndani ya function ya concat unaweza pia kuunganisha kwa kuweka vitu vingine. Hivyo nitaongeza empty space kwa kutumia (“ “)
SELECT concat(jina_la_kwanza, " ", jina_la_pili) as jina FROM majibu;
Angalau hapo utaona jina la kwanza na la pili vimeachana kitogo.
Kuweka herufi kubwa au ndogo
Wakati mwingine utataka majina yawe katika format moja tu, kwa mfano kama yote yawe na herufi kubwa tupu ama ndogo tupu. Kuwa herufi kubwa utatumia UPPER() na kuwa herufi ndogo utatumia LOWER(). Ndani ya function utaweka jina la column unayotaka data zake ziwe katika herufi kubwa ama nogo.
Mfano:
SELECT concat(UPPER(jina_la_kwanza), " ", UPPER(jina_la_pili)) as jina FROM majibu;
Hivyo hivyo kuwa herufi ndogo utatumia LOWER()
SELECT concat(LOWER(jina_la_kwanza), " ", LOWER(jina_la_pili)) as jina FROM majibu;
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua. Je umeipenda post hii ? Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutafuta rank ama position kwenye data base yako kwa kutumia sql. Pia utajifunza kuhusu table alias Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza table za database Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza database kwenye mysql kwa kutumia interface ya mysql na kwa kutumia sql langauge Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya mahesabu mbalimbali kwenye database. Kwa mfano kutafuta jumla, idadi na wastani Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili jina la table na jina la column kwenye mysql database. Function hizi ni muhimu katika kubadili data kabla ya kuzionyesha. Hii ni muhimu ili kupata structure maalum ya data. Katika somo hili utajifunza kupata orodha ya database, kubadilibjina la database, kufuta database Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database. Pia utajifunza jinsi ya ku limit kiasi cha data ambazo zitaonekana. Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla. ...
Download App Yetu
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉3
Madrasa kiganjani
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Kitabu cha Afya
👉6
kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
SQL somo la 14: Jinsi ya kutafuta rank na position kwa kutumia sql
SQL - MySQL somo la 6: Jinsibya kutengeneza table kwenye database
SQL - MySQL somo la 3: Jinsi ya kutengeneza database
SQL - MySQL somo la 12: Jinsi ya kutafuta wastani, jumla na idadi kwenye database
Database seomo la 21: Constraints kwenye Database
SQL - MySQL somo la 7: Jinsi ya kubadili jina table na column kwenye database
Database somo la 26: Baadhi ya function za SQL ambayo hutumika kubadili data
SQL -MySQL somo la 4; Jinsi ya kufuta database, kuitumia database na kubadili jina la database pamoja
SQL - MySQL somo la 9: Jinsi ya kusoma data kwenye database
SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database