picha

SQL -MySQL somo la 4; Jinsi ya kufuta database, kuitumia database na kubadili jina la database pamoja

Katika somo hili utajifunza kupata orodha ya database, kubadilibjina la database, kufuta database

Katika somo hili la nne tutakwenda kujifunza mambo makuu matatu ambayo ni:-

1. Kubadili jina la database

2. Kufuta database

3. Kutumia SQL kufanya mabo hayo yaliyotajwa juu na mengineyo.

 

Kama ulishiriki mafunzo katika somo la tatu ulijifunza namna ya kutengeneza database kwa kutumia MySQL na kwa mutumia SAL command. Sasa katika somo hili tutakwenda kutumia database zetu mbili ambazo tulizitengeneza katika somo la tatu.

 

1. Kuona orodha ya database:

Hili ni jambo rahisi tu, baada ya kuingia kwenye MySQL, angalia menu yako, kisha bofya databases hapo utaona orodha ya database zote ambazo umetengeneza.

 

Sasa tunataka kufanya kitu kama hicho cha kuona orodha ta database kwa kutumia SQL language. Kufanya hivi fuata hatuwa hiz:-

1. Kwenye menu bofya SQL

2. Utakuja uwanja wa kuandika SQL hapo tumia command hii

3. SHOW DATABASES;

4. Baada ya hapo bofya neno GO lipo kwa chini pande wa kulia

5. Kumbuka kuwa katika kuandika SQL mwisho tunamalizia na hizo semicolon (;) kama ilivyo hapo juu.

6. Baada ya hapo utaona orodha ya database zote ulizotengeneza.

 

2. Kutumia database

Baada ya kuona orodha ya database zote hatuwa inayofata ni kuitumia hiyo database ama hizo database. Kutumia database maana yake ni kufanya hicho ambacho ulikusudia kwenye hiyo database kwa mfano kufuta, kubadili jiana ama kuweka data ama kuondoa na kubadili.

 

Kufanya hivi kwenye MySQL pia ni rahisi sana, unachotakiwa kufanya ni kubofya hiyo database yako. Ukishaubofya utaona umefunguka na kama kuna taarifa utaanza kuona majedwali yaliyopo.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL pia ni rahisi, fuata hatuwa zifuatazo:-

1. Ingia kwenye uwanja wa SQL

2. Andika command hii

3. USE post;

4. Baada ya hapo bofya neno GO

5. Command yetu hapo ni USE na hiyo post ni database ambayo tayari ipo hivyo tunataka kuitumia. Command hiyo ni maneno ya kiingereza yanayoweza kufahamika kuwa ni kuiambai MySQL kutumia database inayoitwa post.

6. Mpaka kufika hapo utakuwa tayari kutumia database hiyo na unaweza kuifanya unachotaka.

 

3. Kubadili jina la database

Kwa kutumia MySQL baada ya kubofya hiyo databas...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Database Main: Masomo File: Download PDF Views 589

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

SQL - MySQL somo la 1: Jinsi ya kutumia database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandaa kompyuta ama simu yako kwa ajili ya mafunzo ya database

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 10: Kupangilia muonekano wa data wakati wa kuzisoma kwenyed database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database katika mitindo mbalimbali kama kutoka kubwa kwenda ndogo, ama ndogo kwenda kubwa na mingineyo.

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 2: Maana ya database na ina za database na kazi zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za database, lugha ya sql pamoja kuzijuwa kazi zake

Soma Zaidi...
SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database

Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.

Soma Zaidi...
SQL somo la 17: Jinsi ya kutengeneza variable kwenye mysql

Katika somo ili utakwend akujifunza jinsi ya kuweza kutengeneza variable kwenye database ya mysql

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 8: Jinsi ya kuweka data (taarifa) kwenye database

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka data kwenye database, ku edit pamoja na kufuta kwa kutumia SQL na Myql interface

Soma Zaidi...