Database seomo la 21: Constraints kwenye Database
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database
Constraints kwenye Database
1. Maana ya Constraints
Constraints ni sheria au vikwazo vinavyowekwa kwenye safu (columns) za jedwali katika database ili kuhakikisha kuwa data inayoingizwa ni halali, sahihi, na thabiti. Constraints husaidia kudhibiti aina, muundo, na mahusiano ya data kati ya jedwali tofauti.
2. Aina za Constraints
MySQL inatoa aina mbalimbali za constraints, kila moja ikiwa na kazi maalum:
a) PRIMARY KEY
- Hutambulisha kila rekodi kwenye jedwali kipekee.
- Safu iliyo na Primary Key haiwezi kuwa na thamani inayojirudia wala kuwa tupu (NULL).
- Jedwali linaweza kuwa na Primary Key moja tu.
Mfano wa Primary Key:
CREATE TABLE Wanafunzi (
mwanafunzi_id INT AUTO_INCREMENT PRIMARY KEY,
jina VARCHAR(50),
darasa VARCHAR(10)
);
b) FOREIGN KEY
- Huweka uhusiano kati ya safu ya jedwali moja na Primary Key ya jedwali lingine.
- Inazuia kuingiza data isiyo na uhusiano sahihi.
- Inaweza kuwekwa na sheria za utegemezi kama
ON DELETE CASCADEauON DELETE SET NULL.
Mfano wa Foreign Key:
CREATE TABLE Madarasa (
darasa_id INT PRIMARY KEY,
jina_la_darasa VARCHAR(20)
);
CREATE TABLE Wanafunzi (
mwanafunzi_id INT PRIMARY KEY,
jina VARCHAR(50),
darasa_id INT,
FOREIGN KEY (darasa_id) REFERENCES Madarasa(darasa_id)
ON DELETE CASCADE
);
c) UNIQUE
- Inazuia safu kuwa na thamani zinazojirudia.
- Tofauti na Primary Key, jedwali linaweza kuwa na constraints nyingi za UNIQUE.
Mfano wa UNIQUE:
CREATE TABLE Walimu (
mwalimu_id INT PRIMARY KEY,
barua_pepe VARCHAR(100) UNIQUE
);
d) NOT NULL
- Inahakikisha kuwa safu haiwezi kuwa na thamani tupu (NULL).
Mfano wa NOT NULL:
CREATE TABLE Bidhaa (
bidhaa_id INT PRIMARY KEY,
jina VARCHAR(50) NOT NULL,
bei DECIMAL(10, 2)
);
e) CHECK
- Inathibitisha kuwa thamani ya safu inakidhi masharti fulani.
- Ingawa MySQL imeweka msaada mdogo kwa
CHECK, inafanya kazi katika matoleo ya MySQL 8.0 na kuendelea.
Mfano wa CHECK:
CREATE TABLE Wafanyakazi (
mfanyakazi_id INT PRIMARY KEY,
umri INT CHECK (umri >= 18)
);
f) DEFAULT
- Huweka thamani ya chaguo-msingi kwenye safu ikiwa hakuna thamani iliyoingizwa.
Mfano wa DEFAULT:
C...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 web hosting 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
SQL - MySQL somo la 12: Jinsi ya kutafuta wastani, jumla na idadi kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya mahesabu mbalimbali kwenye database. Kwa mfano kutafuta jumla, idadi na wastani
Soma Zaidi...Database somo la 23: View kwenye Database
Katika somo hili utakwend akujifunza nadharia nzima ya view.
Soma Zaidi...SQL somo la 19: Stored Procedure katika MySQL na Tofauti na Function
Somo hili ni muendelezo wa pale tulipoishia katika somo lililopita, hapa tutakwenda kusoma Stored Procedure katika MySQL na Tofauti na Function
Soma Zaidi...SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database
Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 6: Jinsibya kutengeneza table kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza table za database
Soma Zaidi...SQL somo la 15: Jinsi ya kutumia sql function kwenye mysql
Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function kwenye sql na jinsi ya kuzitumia.
Soma Zaidi...