picha

SQL - MySQL somo la 11: Kudhibiti muonekano wa usomaji wa data kwenye database.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa data kutoka kwenye database, kwa kudhibiti mpangilio wake.

Katika somo lililotangulia tumejifunza amna a kupangilia taarifa za kwenye databse. Tuliona namna ya kutumia ORDER BY. Isha tukapanga data zetu kutoka kubwa kwenda ndogo na kinyume chake. Sasa katika somo hili tutatkwenda kuendelea na nnamna ya kupangilia data hizo ila kwa kutumia WHERE .

 

Kwa nini tunatumia where ?

Tunatumia WHERE endapo tuna masharti yanatakiwa yafikiwe ili data kuonekanna. Kwa mfano unataka kusoma menu zote ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000. hapa hili tunaita ni sharti ama condition. Sasa ili sharti hili liweze kufanya kazi kwenye SQL tunatumia where.

 

1. Mfano wa kwanza

Tunahitaji kusoma data zote ambazo price yake ni sawa na  1000.

Kufanya hivyo tutatumia alama ya = mbele ya where. Hivyocommand nzima itaonekana.

SELECT * FROM `menu` WHERE price =1000

hapo menu itakayoonekana ni ile tu ambayo proce yake ni sawa na 1000.

 

2. Mfano wa pili

Tunataka kusoma data ambazo id yake ni 3, 4, na 8. yaani data tu zenye id hizo ndizo tunataka kuziona na si nyinginezo. Hivyo tunatarajia kuwa na row tatu tu. Kufanya hivyo tutatumia OR kwa maana au. Yaani eidha id iwe 3 au id iwe 4 au id iwe 8. Na command yote itaonekana hivi

SELECT * FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8;  pia unweza kuondoa nyota na kupunguza column

SELECT name, price FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8;

 

3. Mafno wa tatu

Chukulia mfano kwenye menu kuna ugali mbili. Kuna ugali nyama abayo ni 1500 na kuna ugali ng’onda ambaypo ji 1000. sasa mimi nataka kusoma ile ambayo ni ugali nyama ya 1500. kumbuka zote ni ugali na kwenye menu zitanasomeka hivyo hivyo. Ili kuona ya ugali 1500 tu tunatakiwa tutumie AND yaani tuselect ugali lakini kwa ulazima kuwa na id yake iwe 1. ambapo kwenye menu yetu id 1 ni ugali hivyo itakuwa hivi:-

SELECT * FROM menu WHERE name = 'ugali' AND id =1

 

Kuna jambo hapa unatakiwa ulijuwe. Tunapotumia string (sting ni mkusanyiko wa herufi na namba, rejea mafunzo ya php) value inatakiwa ikae ndani ya alama za kufnga na funguwa semi ‘’ kama ulivyo kwenye mfano 'ugali'.

 

4. Tofauti ya AND na OR. 

Unapotumia AND maana yake ni lazima masharti yafikiwe ili data kuonek...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Database Main: Masomo File: Download PDF Views 1382

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

SQL somo la 15: Jinsi ya kutumia sql function kwenye mysql

Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function kwenye sql na jinsi ya kuzitumia.

Soma Zaidi...
SQL somo la 19: Stored Procedure katika MySQL na Tofauti na Function

Somo hili ni muendelezo wa pale tulipoishia katika somo lililopita, hapa tutakwenda kusoma Stored Procedure katika MySQL na Tofauti na Function

Soma Zaidi...
Database seomo la 21: Constraints kwenye Database

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database

Soma Zaidi...
SQL somo la 18: Jinsi ya kutengeneza function kwenye mysql database

Wakati mwingne utahitaji kuwa na function ili kurahisisha uchakataji wa data nyingi bila ya kurudia rudia kuandika code.

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 10: Kupangilia muonekano wa data wakati wa kuzisoma kwenyed database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database katika mitindo mbalimbali kama kutoka kubwa kwenda ndogo, ama ndogo kwenda kubwa na mingineyo.

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 12: Jinsi ya kutafuta wastani, jumla na idadi kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya mahesabu mbalimbali kwenye database. Kwa mfano kutafuta jumla, idadi na wastani

Soma Zaidi...