Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili jina la table na jina la column kwenye mysql database.
Katika somo lililotangaulia tumejifunza namna ya kutengeneza table. Sasa katika somo hili tutajifunza jinsi ya kuedit jina la table, kufuta. Tutafanya haya kwa kutumia MySQL na kwa kutumia SQL command. Kabla hujaanza somo hili tengeneza table nyingine kisha iite text. Table hiyo ndio tunakwenda kuifanyia mazoezi ya kuiedit jina na kuifuta. Fuata maelekezo ya somo lililotangulia kutengeneza table.
1. Jinsi ya kubadili jina la table kwenye MySQL
Tunabadili jina kwa sababu maalumy, huwenda jina la mwanzo ni gumu sana ama haliendani na data ambazo zipo kwenye database. Ama linafanana na table nyingine ambayo unataka kuitengeneza. Ili kufanya hivi yaani kubadili jina fuata hatuwa zifuatazo:-
1. Tengeneza Table kwa kutumia command hii
CREATE TABLE IF NOT EXISTS test (
id INT,
name VARCHAR (255),
aka VARCHAR (255)
)
2. Bofya hiyo table itafunguka utaona hizo column ambazo umetengeneza.
3. Ingia kwenye operations
4. Kwenda chini hadi ukute palipoandika table options
5. Chini utaona palipoandikwa Rename table to na mbele yake kuna kabox.
6. Kwenye kabox hako weka jina unalotaka lisomeke kwenye table yako mfano tutumie jaribio, hivyo futa jina la mwanzo kisha weka jaribio hapo
7. Bofya GO
8. Mpaka kufika hapo jina la table yako litakuwa limebadilika kuwa jaribio
2. Kubadili jina la table kwa kutumia SQL command
Sasa kama huhitaji kutumia MySQL interface kufanya hivyo unaweza kutumia SQL fuata hatuwa zifuatazo:-
1. Funguwa uwanja wa SQL
2. Kubadili jina tunatumia RENAME TABLE au ALTER TABLE kisha inafatiwa na jina la mwanzo ambalo ni jaribio kisha unaandika to kisha unaweka jina jipya mfano test. Statement hii itakuwa hivi
3. RENAME TABLE jaribio to test;
4. Pia unaweza kutumia hii kubadili jina ALTER TABLE test RENAME to jaribio
5. Baada ya hapo bofya GO
6. Kufikia hapo utakuwa umebadili jina la table yako.
3. Kubadili jina la column
Chukulia unataka kubadili jina la column lmfano katika katika table hiyo tuliotoka kuirename ina column tatui mabzo ni id, name na aka. Sasa tunataka kubadili name tuweke firstname badala ya kuwa nme. Kufanya hivi kwa kutumia MySQL fuata hatuw zifuatazo:-
1. Bofya hiyo table
2. Bofya palipoandika structure
3. Utaona column zote tatu zipo hapo
4. Kwa upande wa kulia kwa kila column kuna palipoandikwa change. Bofya hapo
5. Kutakuja ukurasa wenye vijibox vingi
6. Tafuta kibox kilichoanikwa name
7. Futa name kisha andika jina unalotaka kubadili mfano firstname kumbuka hakuna kuruka nafasi katika kuandika majina.
8. Bofya neno save lipo upande wa kulia
9. Mpaka kufika hapo utakuwa umeweza kubadili jina la column.
10.
4. Kubadili jina la column kwa kutumia SQL
Tofauti na kupitia hatuwa hizo nyingi kwa kutumia SQL unaweza kubadili kwa haraka zaidi. Kufanya hivo fata hatuwa zifuatazo:-
1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
2. Kuba">...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandaa kompyuta ama simu yako kwa ajili ya mafunzo ya database
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database. Pia utajifunza jinsi ya ku limit kiasi cha data ambazo zitaonekana.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za data zinazotumika kwenye mysql database
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza table za database
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuunganisha table zaidi ya moja kwneye database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu Primary Key na Foreign Key
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya transaction kwenye database
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za database, lugha ya sql pamoja kuzijuwa kazi zake
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka data kwenye database, ku edit pamoja na kufuta kwa kutumia SQL na Myql interface
Soma Zaidi...