SQL - MySQL somo la 6: Jinsibya kutengeneza table kwenye database

SQL - MySQL somo la 6: Jinsibya kutengeneza table kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza table za database

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Katika somo la tano tuliona aina za data ambazo tunakwnda kuzitumia kwenye DATABASE hivyo katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza jedwali au table kwa ajili ya kuhifadhia data.

 

Kabla ya kuanza somo nataka uelewe vyema tunaposema tadatase table tunamaanisha nini hasa. Kama umeshawahi kutumia microsoft access bila shaka umetambuwa namna ambavyo table inavyofanya kazi. Kama ndio kwanza osijali , somo hili ni kwa ajili yako.

 

Kwanza chukulia mfano una excel document yako, ambayo ina majina ya wanafunzi na ya wazazi wao. Hivyo utahitaji kuwa na colum kama tatu hivi. Colum ya kwanza ni namba, ya pili ni jina la mwanafunzi na ya tatu ni jina la baba. Sasa excel yako mathalani itakuwa na wanafunzi 45 hivyo kwenye colum ya namba itaanzia moja hadi 45 kwa kulingana na idadi ya wanafunzi. Na hivyo hivyo colum ya majina nayo italingana na namba. Sasa faili kama hili kwenye database ndio huitwa table.

Yaani kwa ufupi table tunaweza taarifa ambazo zinafanana kwenye database. Mfano database ni ya shule ina madarasa. Hivyo kila darasa utaliandikia table yake, ambayo mfano wake ni sawa na kuwa na kila darasa na faili lake la excel ila zote ni za wanafunzi wa shule ambalo ndio itakuwa database yako.

 

 

Wacha nikupe mfano mwingine huwenda ukafahamu zaidi. Chukulia tunataka kuhifadhi post zetu kwenye database. Hivyo tutatakiwa ktengeneza table ambayo itakuwa na namba ya post, kichwa cha habari cha post, muhtasari wa post, maudhui ya post, picha, aliyechapisha na tarehe. Wacha nikwambie kitu, angalia post kwenye blog utaona zina vitu hivyo, tarehe, aliyechaposha, muhtasari, maudhui yenyewe, na kichwa cha habari.

 

Sasa taarfa kama hiyo tutahitaji kuwa na table ambayo itahifadhi taarifa hizo kwa kila post. Kwa mujibu wa mfano huo table yetu itakuwa na colum 7. hizi kwenye database wakati wa kutengeneza table tutaziita field. Hivyo tunaasema table yetu itakuwa na field 7. ili tupunguze urefu wa maneno wacha tutumie kingereza. Field zetu ni id, titlle, summary, content, image, publisher, date.

 

Ufupi wa maneno ni kuwa ndani ya database taarifa huhifadhiwa kwenye table. Hivyo database moja inaweza kuwa na table hata 100 ama zaidi. Na kila table huhifadhi taarifa zinazofanana ndio maana zinawekwa pamoja. Ok sasa somo letu litakwenda kukufundisha namna ya kutengeneza hizo table.

 

Jinsi ya kutengeneza table kwenye MySQL

Hapa tutatumia MySQL na pia tutatumia SQL command. Jambo la kwanza unalotakiwa ulijuwe ni kuwa utambuwe aina za data zako unazotaka kuziweka pia ujuwe length ya kila data je unataka ihifadhi character ngapi. Kama tulivyoona katika somo lililotangulia kuwa kila aina ya ata ina idadi ya character zake.

 

Kwanza tengeneza database na iite blog. Baada ya hapo ifunguwe hiyo database utaona kunasehemu pameandikwa CREATE TABLE IF NOT EXISTS. Darasa letu litaanzia hapo. Kama umefika hapo fuata hatuwa zifuatazo:-

1. Funguwa database

2. Utaona sehemu pameandika CREATE TABLE IF NOT EXISTS na jini kuna kabosi

3. Weka jina la table hapo weka post

4. Kuna palipoandika number of columns hapo weka 7 idadi ya colum zetu kama ilivyo kwenye maelezo hapo juu

5. Bogya GO

 

6. Utaona ukurasa mpya ambao una vijumba vingivingi lakini ukivihesabu kwa kwenda chini utaona ni 7 kama ulivyoweka hapo mwanzo.

 

7. Cheki kuna palipoandika name kisha msururu wa vijumba unafata kuelekea chini. Hapo unatakiwa ujaze majina ya kila colum kulingana na maelezo ambayo tumeona hapo juu. Hivyo tutajaza kuanzia na id, kisa kijumba kinefuata ni title kisha kinachofuata ni summarty kisha kinachofuata utajaza contente, kisha ujtajaza image kisha publisher kisha date.

 

8. Kisha angalia juu kulia kwa name kuna type. Hapo utajaza kila c">...

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Database Main: ICT File: Download PDF Views 683

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Database seomo la 21: Constraints kwenye Database
Database seomo la 21: Constraints kwenye Database

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database

Soma Zaidi...
SQL -MySQL somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye Mysql Database
SQL -MySQL somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye Mysql Database

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za data zinazotumika kwenye mysql database

Soma Zaidi...
Database somo la 26: Baadhi ya function za SQL ambayo hutumika kubadili data
Database somo la 26: Baadhi ya function za SQL ambayo hutumika kubadili data

Function hizi ni muhimu katika kubadili data kabla ya kuzionyesha. Hii ni muhimu ili kupata structure maalum ya data.

Soma Zaidi...
SQL - somo la 13: Jinsi ya kutumia CASE kwenye SQL
SQL - somo la 13: Jinsi ya kutumia CASE kwenye SQL

katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutumia case kwenye databse ili kuchakata taarifa za matokeo

Soma Zaidi...
Database somo la 22: Primary Key na Foreign Key
Database somo la 22: Primary Key na Foreign Key

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu Primary Key na Foreign Key

Soma Zaidi...
SQL somo la 14: Jinsi ya kutafuta rank na position kwa kutumia sql
SQL somo la 14: Jinsi ya kutafuta rank na position kwa kutumia sql

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutafuta rank ama position kwenye data base yako kwa kutumia sql. Pia utajifunza kuhusu table alias

Soma Zaidi...
Database somo la 24: Transaction kwenye database
Database somo la 24: Transaction kwenye database

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya transaction kwenye database

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 2: Maana ya database na ina za database na kazi zake
SQL - MySQL somo la 2: Maana ya database na ina za database na kazi zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za database, lugha ya sql pamoja kuzijuwa kazi zake

Soma Zaidi...
SQL  somo la 16:  Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database
SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database

Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.

Soma Zaidi...
SQL - MySQL somo la 11: Kudhibiti muonekano wa usomaji wa data kwenye database.
SQL - MySQL somo la 11: Kudhibiti muonekano wa usomaji wa data kwenye database.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa data kutoka kwenye database, kwa kudhibiti mpangilio wake.

Soma Zaidi...