SQL - somo la 13: Jinsi ya kutumia CASE kwenye SQL
katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutumia case kwenye databse ili kuchakata taarifa za matokeo
katika somo hili utakwenda kujifunza namna ambavyo unaweza kutumia case katika kuchakata data husika.
chukulia mfano una list hii ya wanafunzi na maksi zao kwenye database yako. sasa tunataka data zetu ziweke column nyingine ya kuonyesha grade,kama ni 41 kwenda juu hiyo ni A, na 31 kwenda 40 hiyo ni B na 21 - 30 hiyo ni C na 11 - 20 hiyo ni D na 0 - 10 hiyo ni F. sasa hapo ndipo tunahitaji kutumia case.
program yetu itakwenda kuangalia yenyewe hizo maksi kisha itatengeneza column nyingine ya GRADE. kwanza tengeneza database iize matokeo ama jina lolote, kisha tengeneza tebo iite majibu ama jina lolote. kisha weka data hizo hapo chini. usisahau kuweka column ya id ama tumia code hizi za sql kutengeneza database na tebo hiyo
CREATE TABLE `majibu` (
`id` int(11) NOT NULL,
`jina` varchar(255) NOT NULL,
`alama` int(11) NOT NULL
) ENGINE=InnoDB DEFAULT CHARSET=utf8mb4 COLLATE=utf8mb4_general_ci;
INSERT INTO `majibu` (`id`, `jina`, `alama`) VALUES
(1, 'Juma', 45),
(2, 'Halima', 32),
(3, 'Daudi', 15),
(4, 'Saidi', 28),
(5, 'Semeni', 8);
ALTER TABLE `majibu`
ADD PRIMARY KEY (`id`);
ALTER TABLE `majibu`
MODIFY `id` int(11) NOT NULL AUTO_INCREMENT, AUTO_INCREMENT=6;
COMMIT;
Kanuni za kutumia case
kwanza utaandika keyword case ikifuatiwa na keyword WHEN kisha itafuatiwa na sharti unalotaka kuweka mfano case WHEN alama > 40 baada ya kuweka sharti utawekakeyword THEN ikifuatiwa na matokeo yaani nni kitokee endapo shari limetimia? mfano case WHEN alama > 40 THEN A itafuatiwa na ELSE ili kuonyesha matokeo nini kionekane endapo sharti halikufikiwa.mfano case WHEN alama > 40 THEN A ELSE “ongeza bidii”. mwisho wa case yako baada ya kuweka sharti zako zote utamaliza na neno END likifuatiwa na AS utaweka jina la column mpya yenye hizo grade. kwa mfano column yetu hapo tutaiita GRADE.
case WHEN alama > 40 THEN A ELSE “ongeza bidii” END as GRADE. code nzima itaonekana hivi
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
ELSE 'Ongeza bidii'
END as GRADE
FROM `majibu` ;
Sasa wacha wacha tuweke case kwa ajili ya ku display grade A, B, C, D na F
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
WHEN alama > 30 AND alama <41 THEN 'B'
WHEN alama > 20 AND alama < 31 THEN 'C'
WHEN alama > 10 AND alama < 20 THEN 'D'
ELSE 'F'
END as GRADE
FROM `majibu` ;
Kwa namna kama hii tunaweza kuongeza column nyingine. kwa mfano tunataka kuweka column ya maoni ya mwalimu, akiwa amepata A ni vizuri sana, B ni vizuri C ni wastani D ni dhaifu F ni mbaya.
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
WHEN alama >...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
SQL - MySQL somo la 12: Jinsi ya kutafuta wastani, jumla na idadi kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya mahesabu mbalimbali kwenye database. Kwa mfano kutafuta jumla, idadi na wastani
Soma Zaidi...SQL somo la 18: Jinsi ya kutengeneza function kwenye mysql database
Wakati mwingne utahitaji kuwa na function ili kurahisisha uchakataji wa data nyingi bila ya kurudia rudia kuandika code.
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 9: Jinsi ya kusoma data kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database. Pia utajifunza jinsi ya ku limit kiasi cha data ambazo zitaonekana.
Soma Zaidi...Database seomo la 21: Constraints kwenye Database
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu nadharia ya Constraints kwenye Database
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 1: Jinsi ya kutumia database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandaa kompyuta ama simu yako kwa ajili ya mafunzo ya database
Soma Zaidi...Database somo la 25: Utangulizi wa Database ya sqlite
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu aina nyingine ya database inayoitwa sqlite. Hii haihitaji server, na ni faili moja tu.
Soma Zaidi...