SQL - somo la 13: Jinsi ya kutumia CASE kwenye SQL
katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutumia case kwenye databse ili kuchakata taarifa za matokeo
katika somo hili utakwenda kujifunza namna ambavyo unaweza kutumia case katika kuchakata data husika.
chukulia mfano una list hii ya wanafunzi na maksi zao kwenye database yako. sasa tunataka data zetu ziweke column nyingine ya kuonyesha grade,kama ni 41 kwenda juu hiyo ni A, na 31 kwenda 40 hiyo ni B na 21 - 30 hiyo ni C na 11 - 20 hiyo ni D na 0 - 10 hiyo ni F. sasa hapo ndipo tunahitaji kutumia case.
program yetu itakwenda kuangalia yenyewe hizo maksi kisha itatengeneza column nyingine ya GRADE. kwanza tengeneza database iize matokeo ama jina lolote, kisha tengeneza tebo iite majibu ama jina lolote. kisha weka data hizo hapo chini. usisahau kuweka column ya id ama tumia code hizi za sql kutengeneza database na tebo hiyo
CREATE TABLE `majibu` (
`id` int(11) NOT NULL,
`jina` varchar(255) NOT NULL,
`alama` int(11) NOT NULL
) ENGINE=InnoDB DEFAULT CHARSET=utf8mb4 COLLATE=utf8mb4_general_ci;
INSERT INTO `majibu` (`id`, `jina`, `alama`) VALUES
(1, 'Juma', 45),
(2, 'Halima', 32),
(3, 'Daudi', 15),
(4, 'Saidi', 28),
(5, 'Semeni', 8);
ALTER TABLE `majibu`
ADD PRIMARY KEY (`id`);
ALTER TABLE `majibu`
MODIFY `id` int(11) NOT NULL AUTO_INCREMENT, AUTO_INCREMENT=6;
COMMIT;
Kanuni za kutumia case
kwanza utaandika keyword case ikifuatiwa na keyword WHEN kisha itafuatiwa na sharti unalotaka kuweka mfano case WHEN alama > 40 baada ya kuweka sharti utawekakeyword THEN ikifuatiwa na matokeo yaani nni kitokee endapo shari limetimia? mfano case WHEN alama > 40 THEN A itafuatiwa na ELSE ili kuonyesha matokeo nini kionekane endapo sharti halikufikiwa.mfano case WHEN alama > 40 THEN A ELSE “ongeza bidii”. mwisho wa case yako baada ya kuweka sharti zako zote utamaliza na neno END likifuatiwa na AS utaweka jina la column mpya yenye hizo grade. kwa mfano column yetu hapo tutaiita GRADE.
case WHEN alama > 40 THEN A ELSE “ongeza bidii” END as GRADE. code nzima itaonekana hivi
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
ELSE 'Ongeza bidii'
END as GRADE
FROM `majibu` ;
Sasa wacha wacha tuweke case kwa ajili ya ku display grade A, B, C, D na F
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
WHEN alama > 30 AND alama <41 THEN 'B'
WHEN alama > 20 AND alama < 31 THEN 'C'
WHEN alama > 10 AND alama < 20 THEN 'D'
ELSE 'F'
END as GRADE
FROM `majibu` ;
Kwa namna kama hii tunaweza kuongeza column nyingine. kwa mfano tunataka kuweka column ya maoni ya mwalimu, akiwa amepata A ni vizuri sana, B ni vizuri C ni wastani D ni dhaifu F ni mbaya.
SELECT *,
CASE
WHEN alama > 40 THEN 'A'
WHEN alama >...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
SQL somo la 14: Jinsi ya kutafuta rank na position kwa kutumia sql
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kutafuta rank ama position kwenye data base yako kwa kutumia sql. Pia utajifunza kuhusu table alias
Soma Zaidi...SQL -MySQL somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye Mysql Database
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za data zinazotumika kwenye mysql database
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 8: Jinsi ya kuweka data (taarifa) kwenye database
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka data kwenye database, ku edit pamoja na kufuta kwa kutumia SQL na Myql interface
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 1: Jinsi ya kutumia database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandaa kompyuta ama simu yako kwa ajili ya mafunzo ya database
Soma Zaidi...SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database
Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 12: Jinsi ya kutafuta wastani, jumla na idadi kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya mahesabu mbalimbali kwenye database. Kwa mfano kutafuta jumla, idadi na wastani
Soma Zaidi...