SQL -MySQL somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye Mysql Database
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina mbalimbali za data zinazotumika kwenye mysql database
TYPE OF DATA IN MySQL:
Somo hili linakwenda kukufundisha aina za taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database (type of data). Ili kuelewa maana ya hili somo, chukulia database kama storage yako au memori kadi. Sasa kwenye memori kadi utaweza kuhifadhi video, miziki, document na nyinginezo. Ila sasa kwa upande wa database huwezi kuhifadhi video, ama mziki au document kama pdf kama ilivyo kwenye memory card. Katika database kuna namna yake ya kuweza kuhifadhi hizi media file..
Hivyo ili kujuwa ni taarifa zipi sasa unaweza kuzihifadhi kwenye database? Kama video inaweza kukaa kwenye database na umejifunza kuwa blog zinatumia database vipi post ya blog itaweza kuwa na image ama video? Haya yote utajifunza katika mlolongo wa somo hili na yanayofata.
Aina za data kwenye MySQL database:
1. CHAR
2. VARCHAR
3. BINARY
4. VARBINARY
5. TINYBLOB
6. TINYTEXT
7. TEXT
8. MEDIUMTEXT
9. MEDIUMBLOB
10. LONGTEXT
11. LONGBLOB
12. ENUM
13. SET
14. BIT
15. TINYINT
16. BOOL
17. BOOLEAN
18. SMALLINT
19. MEDIUMINT
20. INT
21. INTEGER
22. BIGINT
23. FLOAT
24. DOUBLE
25. DECIMAL
26. DEC
27. DATE
28. DATETIME
29. TIMESTAMP
30. TIME
31. YEAR
Kabla hatujaziona data hizi na jinsi zinavyofanya kazi kwanza kuna mbambo hapa tunatakiwa tuyaweke wazi. Kwanza tunatakiwa tielewe maana ya charcter, utf, text, letter, unicode, non-unicode.
Katika uandishi jumla ya herufi, namba na alama za kiuandishi kama emoji, visitari, vinukta , alama za koma na kadhalika, jumla ya yote haya yanaitwa character. Mfano neno “hallo bongoclass!!!” hapa kuna jumla ya mane mawili ambayo ni halo na neno bongoclass. Lakini haya maneno mawili yana jumala ya character 21 ukijumlisha na hizo funga semi na fungua na space moja. Hivyo ukisikia character zipo hivi.
Sasa wanaposema character set ni seti maalumu ya hizo character ambayo hutumika katika kifaa cha kielectrinic ili kupeleka taarifa kutoka kifaa kwenda kingine. Kwa mfano unapoandika code. Kwa mfano katika visimu vya batani kama mtu akikutumia emoj haitaonyesha lakini utaona kuna viduara duara na vijialama. Hii ni kwa sababu character set inayotumika kwenye simu ya batani haiwezi kutafasiri baadhi ya character zilizotoka kwenye simu ya smart phone.
Hizi set zipo nyingi ila standard ambayo hukubali angalau character karibia zote, ila si zote ni UTF-8. hiki ni kifupisho cha maneno Unicode (or Universal Coded Character Set) Transformation Format – 8-bit.
...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
SQL - MySQL somo la 9: Jinsi ya kusoma data kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kutoka kwenye database. Pia utajifunza jinsi ya ku limit kiasi cha data ambazo zitaonekana.
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 1: Jinsi ya kutumia database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandaa kompyuta ama simu yako kwa ajili ya mafunzo ya database
Soma Zaidi...SQL - MySQL somo la 8: Jinsi ya kuweka data (taarifa) kwenye database
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuweka data kwenye database, ku edit pamoja na kufuta kwa kutumia SQL na Myql interface
Soma Zaidi...Database somo la 22: Primary Key na Foreign Key
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu Primary Key na Foreign Key
Soma Zaidi...SQL somo la 16: Jinsi ya kuandaa matokeo ya Mtihani kwa kutumia database
Katika somo hili tutakwenda kumalizia program yetu ya kutengeneza matokeo ya wanafunzi kwa kuweka position kwa kila somo na position ya ujumla.
Soma Zaidi...SQL -MySQL somo la 4; Jinsi ya kufuta database, kuitumia database na kubadili jina la database pamoja
Katika somo hili utajifunza kupata orodha ya database, kubadilibjina la database, kufuta database
Soma Zaidi...