picha

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

(3) Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)


Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako? Nao wanataka wakahukumiwe kwa njia ya twaghuuti; na hali wameamrishwa kukataa njia hiyo. Na Shetani anataka kuwapoteza upotofu (upotevu) ulio mbali (na haki).(4:60)


Na wanapoambiwa "Njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, na (njooni) kwa Mtume," utawaona wanafiki wanajiweka mbali nawe kabisa. Basi itakuwaje utakapowafikia msiba kwa sababu ya yale iliyotanguliza mikono yao?Kisha wakakujia wakiapa "Wallahi! Hatukutaka ila wema na mapatano." Hao ndio wale ambao Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi waachilie mbali, (lakini) uwape mawaidha na uwaambie maneno yenye taathira yatakayoingia katika nafsi (nyoyo) zao. (4:61-63)


Imekuwaje nyinyi kuwa makundi mawili katika khabari ya wanafiki, na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa sababu ya yale (mabaya) waliyoyachuma? Je! Mnataka kumwona mwongofu ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kuwa kapotea? Na aliyemhukumu Mwenyezi Mungu kuwa amekwisha potea hutampatia njia (ya kuambiwa mwongofu). (4:88)


Waambie wanafiki kwamba watapata adhabu inayoumiza. (Wanafiki) ambao huwafanya makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu. Je! Wanataka wapate utukufu kwao? Basi utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu. (Hauko katika mkono wa mtu). Naye amekwisha kuteremshieni katika Kitabu (hiki) ya kwamba mnaposikia Aya za Mwenyezi Mungu zinakataliwa na kufanyiwa stihzai, basi msikae pamoja nao, hata waingie katika mazungumzo mengine. (Mtakapokaa) mtakuwa kama wao. Hakika Mwenyezi Mungu atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja katika Jahannam. (4:138-140)



(Wanafiki) ambao wanakungojeni (mpate msiba): basi mkipata kushinda kunakotoka kwa Mwenyezi Mungu, husema (kukwambieni): "Je! Hatukuwa pamoja nanyi?" (Na kama makafiri wamepata sehemu (ya kushinda) husema: (kuwaambia makafiri), "Je, hatukukurubia kukushindeni (tulipokuwa katika jeshi la Waislamu), tukakuzuilieni na (kudhuriwa na hao). Waislamu?" Basi Mwenyezi Mungu atahukumu baina yenu siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu hatawajaalia makafiri njia ya kuwashinda Waislamu (kabisa kabisa mpaka waiondoshe dini yao. Hawatajaaliwa kupata hayo). Wanafiki hutaka kumdanganya (hata) Mwenyezi Mungu. Naye atawaadhibu kwa sababu ya kudanganya kwao (huko). Na wanaposimama kusali husimama kwa uvivu, wanaonyesha watu (kuwa wanasali) wala hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo. (4:141-42)



Wanayumbayumba baina ya huku (kwa Waislamu na huko kwa makafiri). Huku hawako wala huko hawako. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemhukumu kupotea, huwezi kumpatia njia (ya kuhisabika kuwa mwongofu). Enyi mlioamini! Msiwafanye makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu. Mnataka awe nayo (Mtume wa) Mwenyezi Mungu hoja dhahiri juu yenu (ya kuwa nyinyi wabaya)? Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi (yo yote). (4:143-145)



Katika aya hizi sifa za wanafiki zinaainishwa kama ifuatavyo:
(i)Wanapendelea kuhukumiwa kwa sheria za Kitwaghuut kuliko kuhukumiwa kwa sheria za Allah (s.w)
(ii)Hawako tayari kuishi kwa kufuata Qur-an na Sunnah.
(iii)Hutumia sana viapo katika kuficha uovu wao dhidi ya Uislamu na Waislamu.
(iv)Huwafanya makafiri kuwa marafiki badala ya Waislamu.
(v)Hujikomba kwa makafiri kwa kutaraji kupata vyeo au kuonekana wa maana kwao.
(vi)Wanashirikiana na makafiri katika kuzifanyia stihizai aya za Allah (s.w) na Uislamu kwa ujumla.
(vii)Waislamu wakishinda, hujikomba kuwa pamoja nao na hujinakshi (hujigamba) kuwa wao ndiwo waliosababisha kupatikana kwa ushindi.
(viii)Makafiri wakishinda hujikomba kwao na kujinakshi kuwa ndio waliowawezesha kushinda.
(ix)Hawana msimamo. Kwa Waislamu hawapo na kwa makafiri hawapo. Hivyo hawaaminiki kote kote.
(x)Wanaposimama kuswali, husimama kwa uvivu.
(xi)Hufanya amali kwa riya (kwa kuonyesha watu). (xii Hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo tu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 940

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...
Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu)

Soma Zaidi...
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu

Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu katika uislamu? Nini naana ya elimu ya muongizo. Je elimu ya mazingiravmaana yakeni nini. Ni upi utofauti wa elimu ya muongozo na elimu ya mazingira?

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...