image

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab



Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wasemao kweli, na wanawake wasemao kweli, na wanaume wanaosubiri, na wanawake wanaosubiri, na wanaume wanaonyenyekea na wanawake wanaonyenyekea, na wanaume wanaotoa (Zaka na) sadaka, na wanawake wanaotoa (Zaka na) sadaka, na wanaume wanaofunga, na wanawake wanaofunga, na wanaume wanaojihifadhi tupu zao, na wanawake wanaojihifadhi, na wanaume wanaomtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wanawake wanaomtaja Mwenyezi Mungu (kwa wingi) Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na ujira mkubwa. (33:35)


Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu (upotevu) ulio wazi (kabisa). (33:36).



Mafunzo
Kutokana na aya hizi tunapata mafunzo yafuatayo:
Kwanza,
Muumini wa kweli ni yule anayejitahidi kwa kadiri ya uwezo wake kutekeleza yale yote yaliyoorodheshwa katika aya (33:35) na kutekeleza maamrisho mengine yote ya Allah (s.w) na Mtume wake pamoja na kuacha makatazo yote ya Allah (s.w) na Mtume wake. Kwa muhtasari sifa za waumini zilizoorodheshwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo.



(i)Wenye kutoa shahada ya kweli kwa kutekeleza vilivyo maamrisho yote ya Allah(s.w) na kuacha makatazo yake yote.
(ii)Wenye kuziingiza katika matendo nguzo zote za imani.
(iii)Wenye kumtii Allah (s.w) na Mtume wake ipasavyo katika kukiendea kila kipengele cha maisha na kuwatii wenye mamlaka juu yao kwa mujibu ya maelekezo ya Allah (s.w) na Mtume wake.
(iv)Wenye kusema na kusimamia ukweli
(v)Wenye kujipinda katika kufanya subira katika kuendesha maisha yao ya kila siku na katika kusimamisha Uislamu katika jamii.
(vi)Wenye kujiepusha na kibri, majivuno, majigambo, n.k. katika kuhusuhubiana na watu katika mchakato wa maisha ya kila siku.
(vii)Wenye kutoa yale Allah(s.w) aliyowaruzuku kwa ajili ya kuwahurumia wenye kuhitajia na pia kwa ajili ya kuundeleza Uislamu na kuusimamisha katika jamii.
(viii)Wenye kuleta mara kwa mara funga za sunnah baada ya kuikamilisha funga ya Ramadhani na funga za kafara kwa yule aliyelazimika kwazo. Yaani wenye kuwa katika
swaumu angalu siku tatu kwa kila mwezi.
(ix)Wanaojihifadhi na zinaa na kujiepusha na vishawishi vyote vya zinaa.
(x) Wenye kumtaja na kumbumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi.



Pili, katika Uislamu waumini wanaume na waumini wanawake wana haki sawa mbele ya Allah (s.w). anayeheshimiwa zaidi mbele ya Allah ni yule aliye mchaji zaidi kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:


"Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamume (mmoja, Adamu) na (yule yule) mwanamke (mmoja, Hawwa). Na tumekufanyeni mataifa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu).Hakika aheshimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Allah zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Allah ni mjuzi mwenye habari (za mambo yote)." (49:13)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 333


Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Je ni ipi nafasi ya Elimukatika dini ya uislamu? Soma Zaidi...

Historia ya Mwanadamu
Soma Zaidi...

Himizo la kuwasamehe waliotukosea
β€œNa wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Soma Zaidi...

KAZI ZA MALAIKA
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Soma Zaidi...

Kujiepusha na ubadhirifu (israfu) na ubakhili
Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah
Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio. Soma Zaidi...

Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij
Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Ilhamu katika uislamu?
Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali. Soma Zaidi...

ENYI WAJA WANGU NIMEIKATAZA NAFSI YANGU DHULMA
Soma Zaidi...

NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)
Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu) Soma Zaidi...