Navigation Menu



Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab



Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu." Na taifa moja miongoni mwao liliposema "Enyi, wenyeji wa Yathribu (Madina)! Hamna mahali pa kukaa nyinyi, basi rudini Na kundi jingine miongoni mwao likaomba ruhusa kwa Mtume kwa kusema: "Hakika nyumba zetu ni tupu, (hapana watu, tunakwenda zetu)," lakini hazikuwa tupu, hawakutaka ila kukimbia tu. Na lau kama yaliingia (Majeshi ya makafiri) juu yao katika pande zote , kisha wakaombwa kufanya vita (juu ya Waislamu) wangevifanya, na wasingelikaa humo (Madina tena) ila muda kidogo tu (33:12-1 4)


Na kwa yakini walikwishafanya ahadi na Mwenyezi Mungu zamani ya kwamba hawatageuza migongo ; na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuulizwa. (33:15)



Sema: "Kukimbia hakutakufaeni kama mkikimbia mauti au kuuawa, na kwa hivyo, hamtastareheshwa ila kidogo tu, (kisha mara mtakufa)." Sema: "Ni nani ambaye aweza kukulindeni na Mwenyezi Mungu kama (Mungu) akikutakieni uovu, au akikutakieni rehema?" Wala hawatapata mlinzi wala msaidizi kinyume cha Mwenyezi Mungu.Bila shaka Mwenyezi Mungu anawajua wale wanaojizuia miongoni mwenu (wasende vitani pamoja na Mtume) na wawaambiao ndugu zao; "Njooni kwetu (wala msende kwa Muhammad);" wala hawendi katika mapigano ila kidogo tu (ili kuwadanganya Waislamu). (33:16-1 8)


Wakakufanyieni choyo (kukusaidieni) lakini inapokuja hofu, utawaona wanakutazama, macho yao yanazungukazunguka kama yule aliyezimia kwa mauti; lakini hofu inapoondoka, wanakuudhini kwa ndimi zao kali, wanaifanyia choyo kheri, (hawataki kusaidia). Hao hawakuamini, kwa hivyo Mwenyezi Mungu ameviondoshea thawabu vitendo vyao; na hayo ni sahali kwa Mwenyezi Mungu. (Mpaka sasa kwa woga wao) Wanafikiri yale makundi (ya maadui) hayajaondoka. Na kama makundi hayo yangekuja (tena), wangependa laiti wangekua wako jangwani pamoja na Mabedui, wakiuliza tu habari zenu. Na kama wangalikuwa pamoja nanyi wasingalipigana ila kidogo tu. (Mara wangelikimbia kwa woga wao). (33:19-20)



Sifa za wanafiki zilizoainishwa katika aya hizi ni hizi zifuatazo:
(i) Humdhania Mwenyezi Mungu na Mtume wake dhana mbaya. Walisema wakati ule wa Mtume (s.a.w): "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu."
(ii) Huwahofisha na kuwakatisha tamaa waumini ili warudi nyuma wasipambane na maadui wa Uislamu.
(iii) Hutoa nyudhuru za uwongo ili kuepa majukumu ya kuuhami Uislamu na kuuendeleza.
(iv) Huvunja ahadi kila wanapoahidi.
(v) Hawako tayari kupata misukosuko kwa ajili ya Uislamu na huogopa kufa. Hivyo hujitenga mbali na mapigano dhidi ya maadui wa Uislamu.




                   


           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 462


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...

Mgawanyo wa Elimu Usiokubalika katika uislamu.
Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake
Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Furqaan (25:64-76)
Soma Zaidi...

Ni haramu kwa Waumini kuwaoa au kuolewa na Wazinifu, Washirikina na Mahabithi
Soma Zaidi...

Aina kuu za dini
Katika kipengele hichi tutajifunza aina kuu mbili za dini. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat
"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi. Soma Zaidi...