Kuwa mwenye Kumtegemea Allah

35.

Kuwa mwenye Kumtegemea Allah

35. Kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w)



Muislamu wa kweli daima huwa jasiri kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu katika kila hali. Ana yakini kuwa hapana lolote litakalomfika, baya au zuri, ila litakuwa linatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na ana yakini kuwa ulinzi wa maisha yake na mahitajio yake yote ya kimaisha yako mikononi mwa Mwenyezi Mungu (s.w). Mwenyezi Mungu (s.w) anatuamrisha tumtegemee Yeye tu katika aya zifuatazo:


Na tegemea kwa Yule aliye na uhai wa milele ambaye hatakufa ”. (25:58)



“... Na kwa Mwenyezi Mungu wategemee Waislamu. Na tuna nini tusimtegemee Mwenyezi Mungu, na hali Ametuonyesha njia zetu. Na tutayavumilia maudhi yenu. Basi kw a Mw enyezi Mungu w ategemee wategemeao”. (14:11-1 2)


“...Na anayemuogopa Mw enyezi Mungu, (Allah) humtengenezea njia ya kuokoka (na kila balaa); na humpa riziki kwa namna asiyoitazamia. Na anayem tegemea Mw enyezi Mungu yeye hum toshea. Kw a yakini Mw enyezi Mungu anatimiza kusudio lake. Hakika Mwenyezi Mungu amekwisha kiwekea kila kitu kipimo chake”. (65:2-3).
Kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa kila jambo na hasa wakati wa dhiki na kuhitajia msaada, huzidisha imani na ujasiri kwa waumini. Hebu turejee aya zifuatazo:
“Wale ambao watu w aliwaambia: “Watu wamekukusanyikieni. Kwa hiyo waogopeni”. Lakini (maneno hay o) yakawazid ishia imani wakasema Mwenyezi Mungu anatutosha. Naye ni Mlinzi bora kabisa. Basi w akarudi (vitani na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake), hakuna ubaya uliowagusa; na wakafuata yanayomridhisha Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kuu”. (3:173-174)



“Na Waislamu walipoyaona majeshi (ya makafiri) walisema, “Haya ndiyo aliyotuahidi Mw enyezi Mungu na Mtume wake. Mw enyezi Mungu na Mtume wake wamesema kweli,na (jambo hili) halikuwazidishia ila imani na utii. (33:22).


“Hakika waumini wa kweli ni wale ambao anapotajwa Mwenyezi Mungu nyoyo zao hujaa hofu; na wanaposomewa Aya Zake huwazidishia imani na wakamtegema Mola wao tu basi”. (8 : 2)



Hivyo Waislamu hatuna budi kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kila hali. Tukifanya hivyo imani yetu itazidi na tutakuwa na moyo wa ujasiri wa kutuwezesha kupambana na hali yoyote ngumu itakayotukabili kwa sababu tunayakini kuwa halitufikii lolote, baya au zuri, ila liko katika makadirio ya Mwenyezi Mungu (s.w). Ni vyema hapa tukumbushe kuwa kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w) ni kutekeleza wajibu wetu kwa juhudi na maarifa katika jambo lolote tunalolifanya kisha matokeo ya jitihada zetu tumuachie Mwenyezi Mungu (s.w). Hii hasa ndio maana ya kumtegemea Allah (s.w) kama tunavyojifunza.katika aya zifuatazo:


“Naam, wanaoelekeza nyuso zao kwa Mwenyezi Mungu na wakawa ni watendaji mema, basi wao watapata malipo yao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika. (2:112).
Na kwamba, mtu hatapata ila kwa yale anayoyafanya. (53:39).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1670

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?

Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)

Soma Zaidi...
Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jeraha kwenye ngozi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k

Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Soma Zaidi...
Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat

"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...