35.
35. Kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w)
Muislamu wa kweli daima huwa jasiri kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu katika kila hali. Ana yakini kuwa hapana lolote litakalomfika, baya au zuri, ila litakuwa linatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na ana yakini kuwa ulinzi wa maisha yake na mahitajio yake yote ya kimaisha yako mikononi mwa Mwenyezi Mungu (s.w). Mwenyezi Mungu (s.w) anatuamrisha tumtegemee Yeye tu katika aya zifuatazo:
Na tegemea kwa Yule aliye na uhai wa milele ambaye hatakufa ”. (25:58)
“... Na kwa Mwenyezi Mungu wategemee Waislamu. Na tuna nini tusimtegemee Mwenyezi Mungu, na hali Ametuonyesha njia zetu. Na tutayavumilia maudhi yenu. Basi kw a Mw enyezi Mungu w ategemee wategemeao”. (14:11-1 2)
“...Na anayemuogopa Mw enyezi Mungu, (Allah) humtengenezea njia ya kuokoka (na kila balaa); na humpa riziki kwa namna asiyoitazamia. Na anayem tegemea Mw enyezi Mungu yeye hum toshea. Kw a yakini Mw enyezi Mungu anatimiza kusudio lake. Hakika Mwenyezi Mungu amekwisha kiwekea kila kitu kipimo chake”. (65:2-3).
Kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa kila jambo na hasa wakati wa dhiki na kuhitajia msaada, huzidisha imani na ujasiri kwa waumini. Hebu turejee aya zifuatazo:
“Wale ambao watu w aliwaambia: “Watu wamekukusanyikieni. Kwa hiyo waogopeni”. Lakini (maneno hay o) yakawazid ishia imani wakasema Mwenyezi Mungu anatutosha. Naye ni Mlinzi bora kabisa. Basi w akarudi (vitani na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake), hakuna ubaya uliowagusa; na wakafuata yanayomridhisha Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kuu”. (3:173-174)
“Na Waislamu walipoyaona majeshi (ya makafiri) walisema, “Haya ndiyo aliyotuahidi Mw enyezi Mungu na Mtume wake. Mw enyezi Mungu na Mtume wake wamesema kweli,na (jambo hili) halikuwazidishia ila imani na utii. (33:22).
“Hakika waumini wa kweli ni wale ambao anapotajwa Mwenyezi Mungu nyoyo zao hujaa hofu; na wanaposomewa Aya Zake huwazidishia imani na wakamtegema Mola wao tu basi”. (8 : 2)
Hivyo Waislamu hatuna budi kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kila hali. Tukifanya hivyo imani yetu itazidi na tutakuwa na moyo wa ujasiri wa kutuwezesha kupambana na hali yoyote ngumu itakayotukabili kwa sababu tunayakini kuwa halitufikii lolote, baya au zuri, ila liko katika makadirio ya Mwenyezi Mungu (s.w). Ni vyema hapa tukumbushe kuwa kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w) ni kutekeleza wajibu wetu kwa juhudi na maarifa katika jambo lolote tunalolifanya kisha matokeo ya jitihada zetu tumuachie Mwenyezi Mungu (s.w). Hii hasa ndio maana ya kumtegemea Allah (s.w) kama tunavyojifunza.katika aya zifuatazo:
“Naam, wanaoelekeza nyuso zao kwa Mwenyezi Mungu na wakawa ni watendaji mema, basi wao watapata malipo yao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika. (2:112).
Na kwamba, mtu hatapata ila kwa yale anayoyafanya. (53:39).
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.
Soma Zaidi...Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.
Soma Zaidi...Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu)
Soma Zaidi...Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.
Soma Zaidi...Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?
Soma Zaidi...Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere..
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nuzo 6 za imani ya uislamu na pia utajifunz akuhusu mafunzo yanayoweza kupatikana kwenye Nguzo hizi.
Soma Zaidi...