Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
1. Ndio nyenzo pekee inayomuwezesha mwanaadamu kumtambua Mola wake na kuweza kumuabudu ipasavyo.
“Kwa hakika wanaomuogopa (wanaomuabudu) Mwenyezi Mungu ipasavyo miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu” (35:28).
2. Elimu iliyosomwa kwa murengo wa Qur’an na Sunnah ndio inayomuwezesha muumini kuwa Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni.
“Na kumbukeni aliposema Allah kuwaambia Malaika kwamba ataweka ardhini khalifa (kiongozi)” (2:30) pia rejea (2:38).
3. Kutafuta elimu ni ibada maalum yenye hadhi kubwa kuliko ibada zote mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) inayopelekea mja kufanya ibada vilivyo.
“……Na (waumini) waliopewa elimu watapata daraja (kubwa) zaidi…” (58:11).
4. Mwenye elimu ndio ana nafasi bora ya kumtambua na kumuabudu Mola wake ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yake.
Rejea Qur’an (35:28), (39:9) na (58:11).
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo)
Soma Zaidi...Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.
Soma Zaidi...Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.
Soma Zaidi...Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.
Soma Zaidi...Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.
Soma Zaidi...