Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
1. Ndio nyenzo pekee inayomuwezesha mwanaadamu kumtambua Mola wake na kuweza kumuabudu ipasavyo.
“Kwa hakika wanaomuogopa (wanaomuabudu) Mwenyezi Mungu ipasavyo miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu” (35:28).
2. Elimu iliyosomwa kwa murengo wa Qur’an na Sunnah ndio inayomuwezesha muumini kuwa Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni.
“Na kumbukeni aliposema Allah kuwaambia Malaika kwamba ataweka ardhini khalifa (kiongozi)” (2:30) pia rejea (2:38).
3. Kutafuta elimu ni ibada maalum yenye hadhi kubwa kuliko ibada zote mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) inayopelekea mja kufanya ibada vilivyo.
“……Na (waumini) waliopewa elimu watapata daraja (kubwa) zaidi…” (58:11).
4. Mwenye elimu ndio ana nafasi bora ya kumtambua na kumuabudu Mola wake ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yake.
Rejea Qur’an (35:28), (39:9) na (58:11).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...عَنْ أَبِي ذَرٍّ جُنْدَبِ بْنِ جُنَادَةَ، وَأَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ رَسُولِ اللَ...
Soma Zaidi...Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.
Soma Zaidi...Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).
Soma Zaidi...Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.
Soma Zaidi...Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)
Soma Zaidi...