Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?

Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)

Jibu

Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?

 

1. Ndio nyenzo pekee inayomuwezesha mwanaadamu kumtambua Mola wake na kuweza kumuabudu ipasavyo.

 

“Kwa hakika wanaomuogopa (wanaomuabudu) Mwenyezi Mungu ipasavyo miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu” (35:28).

 

2. Elimu iliyosomwa kwa murengo wa Qur’an na Sunnah ndio inayomuwezesha muumini kuwa Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni.

 

“Na kumbukeni aliposema Allah kuwaambia Malaika kwamba ataweka ardhini khalifa (kiongozi)” (2:30) pia rejea (2:38). 

 

3. Kutafuta elimu ni ibada maalum yenye hadhi kubwa kuliko ibada zote mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) inayopelekea mja kufanya ibada vilivyo.

 

“……Na (waumini) waliopewa elimu watapata daraja (kubwa) zaidi…” (58:11).

 

4. Mwenye elimu ndio ana nafasi bora ya kumtambua na kumuabudu Mola wake ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yake.


Rejea Qur’an (35:28), (39:9) na (58:11).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1403

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jeraha kwenye ngozi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya uislamu.

Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.

Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).

Soma Zaidi...