Shirk na aina zake

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Shirk. 

Ni kujaalia kinadharia au kiutendaji kuwa kuna miungu wengine wanaoshirikiana na Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuongoza na kuendesha Ulimwengu.

 

Kuna aina kuu nne za shirk,

  1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Dhaat).
  2. Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Sifaat).
  3. Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ikhtiyaar).
  4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ah-kaam).

   

        1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kujaalia au kuvinasibisha viumbe na uungu kwa kuvipa majina rasmi kama washirika wa Mwenyezi Mungu (s.w) na kuviendea kwa unyenyekevu na ibada maalum kama, kuvisujudia, kuchinja na kuviomba msaada.

Rejea Qur’an (25:2-3), (22:73) na (29:41).

 

        2.  Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwasifu au kuwatukuza viumbe kiwango anachostahiki kusifiwa au kutukuzwa Allah (s.w) peke yake. Kama kuomba dua, baraka na msaada kupitia kwa Wacha-Mungu, mfano kwa baraka za Mtume, Abdul-Qadir, Sharifu au Sheikh fulani n.k.

Rejea Qur’an (53:32), (10:62-64), (2:180), (17:110) na (40:60).

 

          3.  Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwakabidhi viumbe mamlaka kamili ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kuwatii kwayo kama vile kuongoza, kulisha, kulea, kulinda n.k katika maisha ya kila siku kinyume na nafasi au uwezo wao.

Rejea Qur’an (9:31) na (2:208).

 

          4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kutunga sheria au hukumu kinyume na sheria au hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w) alizoziainisha katika vitabu vyake vitukufu na kuzitumia kuhukumu kwazo katika uendeshaji wa maisha ya kila siku.

Rejea Qur’an (5:38), (24:2), (33:36), (5:44-45, 47) na (5:50).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 4680

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kwanini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini?

Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
SHIRK

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.

Soma Zaidi...
Kumuamini mwenyezi Mungu..

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.

Soma Zaidi...