Navigation Menu



Shirk na aina zake

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Shirk. 

Ni kujaalia kinadharia au kiutendaji kuwa kuna miungu wengine wanaoshirikiana na Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuongoza na kuendesha Ulimwengu.

 

Kuna aina kuu nne za shirk,

  1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Dhaat).
  2. Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Sifaat).
  3. Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ikhtiyaar).
  4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ah-kaam).

   

        1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kujaalia au kuvinasibisha viumbe na uungu kwa kuvipa majina rasmi kama washirika wa Mwenyezi Mungu (s.w) na kuviendea kwa unyenyekevu na ibada maalum kama, kuvisujudia, kuchinja na kuviomba msaada.

Rejea Qur’an (25:2-3), (22:73) na (29:41).

 

        2.  Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwasifu au kuwatukuza viumbe kiwango anachostahiki kusifiwa au kutukuzwa Allah (s.w) peke yake. Kama kuomba dua, baraka na msaada kupitia kwa Wacha-Mungu, mfano kwa baraka za Mtume, Abdul-Qadir, Sharifu au Sheikh fulani n.k.

Rejea Qur’an (53:32), (10:62-64), (2:180), (17:110) na (40:60).

 

          3.  Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwakabidhi viumbe mamlaka kamili ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kuwatii kwayo kama vile kuongoza, kulisha, kulea, kulinda n.k katika maisha ya kila siku kinyume na nafasi au uwezo wao.

Rejea Qur’an (9:31) na (2:208).

 

          4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kutunga sheria au hukumu kinyume na sheria au hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w) alizoziainisha katika vitabu vyake vitukufu na kuzitumia kuhukumu kwazo katika uendeshaji wa maisha ya kila siku.

Rejea Qur’an (5:38), (24:2), (33:36), (5:44-45, 47) na (5:50).

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 3337


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Nguzo za imani
Zifuatazo Ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuamini siku ya mwisho
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu Ndio Dini Pekee Inayostahiki Kufuatwa na Watu?
Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu umeipa Elimu nafasi ya kwanza?
Soma Zaidi...

vigawanyo vya elimu
Soma Zaidi...

Nguzo za Imani kwa mujibu wa mafunzo ya kiislami.
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu nguzo sita za imani katika Uislamu. Soma Zaidi...

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an. Soma Zaidi...

Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi
Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi. Soma Zaidi...

Hijabu na kujikinga na zinaa
Soma Zaidi...

mwanadamu hawezi kuishi bila ya Dini
Soma Zaidi...