picha

Shirk na aina zake

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Shirk. 

Ni kujaalia kinadharia au kiutendaji kuwa kuna miungu wengine wanaoshirikiana na Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuongoza na kuendesha Ulimwengu.

 

Kuna aina kuu nne za shirk,

  1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Dhaat).
  2. Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Sifaat).
  3. Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ikhtiyaar).
  4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ah-kaam).

   

        1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kujaalia au kuvinasibisha viumbe na uungu kwa kuvipa majina rasmi kama washirika wa Mwenyezi Mungu (s.w) na kuviendea kwa unyenyekevu na ibada maalum kama, kuvisujudia, kuchinja na kuviomba msaada.

Rejea Qur’an (25:2-3), (22:73) na (29:41).

 

        2.  Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwasifu au kuwatukuza viumbe kiwango anachostahiki kusifiwa au kutukuzwa Allah (s.w) peke yake. Kama kuomba dua, baraka na msaada kupitia kwa Wacha-Mungu, mfano kwa baraka za Mtume, Abdul-Qadir, Sharifu au Sheikh fulani n.k.

Rejea Qur’an (53:32), (10:62-64), (2:180), (17:110) na (40:60).

 

          3.  Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kuwakabidhi viumbe mamlaka kamili ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kuwatii kwayo kama vile kuongoza, kulisha, kulea, kulinda n.k katika maisha ya kila siku kinyume na nafasi au uwezo wao.

Rejea Qur’an (9:31) na (2:208).

 

          4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w).

Ni kutunga sheria au hukumu kinyume na sheria au hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w) alizoziainisha katika vitabu vyake vitukufu na kuzitumia kuhukumu kwazo katika uendeshaji wa maisha ya kila siku.

Rejea Qur’an (5:38), (24:2), (33:36), (5:44-45, 47) na (5:50).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/15/Saturday - 07:32:52 am Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 5099

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 web hosting    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Dalili za kuwepo mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Dhana ya ibada kwa mtazamo wa uislamu..

Mtazamo wa uislamu juu ya ibada (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuamini siku ya mwisho

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Mazingatio kabla ya kuosha maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu katika mtazamo wa Uislamu

Katika Uislamu elimu imegawanyika katika Elimu ya muongozo na elimu ya mazingira.

Soma Zaidi...