Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

NGUZO ZA IMANI


image


Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)


  • Nguzo za Imani.
  1. Kumuamini Mwenyezi Mungu.
  2. Kuamini Malaika wake.
  3. Kuamini Vitabu Vyake.
  4. Kuamini Mitume Wake.
  5. Kuamini siku ya Mwisho.
  6. Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu.

 

  1. Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Imani juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu ni jambo la kwanza kabisa kwa kila mwenye akili timamu kupitia ishara na maumbile mbali mbali yanayotuzunguka.

        Rejea Qur’an (3:190).

   

    -    Baada ya kumtambua, ni kumuabudu ipasavyo na kutomshirikisha katika sifa na majina yake matukufu na kiumbe yeyote.

        Rejea Qur’an (18:109), (31:27), (57:1-7), (59:22-24).

        Rejea Kitabu cha 2, EDK, Shule za Sekondari; Uk.8-16.

 

  1. Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu.

-    Malaika ni viumbe wa Mwenyezi Mungu walioumbwa kutokana na nuru kwa lengo la kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).

 

-    Ni viumbe wa kiroho, wasio na jinsia, wenye mabawa na wenye uwezo wa kujimithilisha na kitu (kiumbe) chochote.

 

-    Hawana matashi ya kibinaadamu kama kula, kulala, kunywa, kuchoka, kuugua na hawana hiari kwa kila wanachoamrishwa na Mwenyezi Mungu (s.w).

    Rejea Qur’an (16:49-50), (7:206) na (21:26-27).

 

  1. Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Kuamini vitabu vya Allah (s.w) ni lazima kwa kila muumini wa kweli kama vilivyoainishwa katika Qur’an, ambavyo baadhi ni;

  1. Suhufi – aliyoteremshiwa Nabii Ibrahim (a.s) na Nabii Musa (a.s).
  2. Taurat – aliyoteremshiwa Nabii Musa (a.s)
  3. Zaburi – aliyoteremshiwa Nabii Daud (a.s)
  4. Injili – aliyoteremshiwa Nabii Isa (a.s) na 
  5. Qur’an – aliyoteremshiwa Nabii au Mtume Muhammad (s.a.w). 

 

-    Vitabu hivi vimeteremshwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika njia sahihi na iliyonyooka ya maisha yao ili kufikia lengo la kuumbwa kwao.

    Rejea Qur’an (57:25) na (5:46).

 

  • Sababu ya Vitabu Vilivyotangulia kutajwa ndani ya Qur’an:
  • Qur’an ndiyo Kitabu cha mwisho kilichoteremshwa kwa ajili ya kuwaongoza walimwengu wote.
  •  Vimetajwa ili kuwafahamisha waislamu juu ya uwiano, usahihi na upotofu wa mafundisho hayo na yale ya Qur’an.
  •  Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha nafasi na utata wa vitabu hivyo kutumika zama hizi kama mwongozo wa maisha.
  • Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha upungufu, mabadilisho na upotofu uliofanywa ndani ya Vitabu hivyo.

Rejea Qur’an (6:92), (2:75), (4:14), (5:15), (5:48) na (16:64).

 

  1. Kuamini Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Mitume ni wanaadamu wanaume walioteliwa ili kuwaongoza na kuwa mifano bora ya kuigwa kwa watu (ummah) wao katika kutekeleza ujumbe wao.

 

  • Idadi kamili ya mitume wote wa Mwenyezi Mungu (s.w) haijulikani, bali waliotajwa ndani ya Qur’an ni 25.

Rejea Qur’an (10:47), (6:83-86)

Rejea Kitabu cha 2, EDK, Shule za Sekondari; Uk.23.

 

  • Sifa za Mitume.
    1. Ni watu walizaliwa, walioa, walikula, waliugua, walikufa, n.k. kama binaadamu wa kawaida isipokuwa Nabii Adamu (a.s).
    2. Walikuwa na kila tabia njema, wakweli, waaminifu na wenye huruma.
    3. Walikuwa na upeo wa Elimu wa hali ya juu kuliko watu wote enzi zao kwa sababu kuletewa kwao wahayi.
    4. Walikuwa Wacha-Mungu wa hali ya juu kuliko watu wote.

 

  • Kazi za Mitume.
  1. Kufahamisha na kufundisha juu ya uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w) na sifa zake. Qur’an (21:25), (16:36).
  2. Kufahamisha mambo ya ghaibu (Akhera) kama Moto, Pepo, Kiyama, Hisabu, Maisha ya Barzaq (kaburini) n.k. 
  3. Kufundisha njia sahihi ya maisha anayoiridhia Mwenyezi Mungu inayopelekea kunusurika na adhabu zake. Qur’an (3:164).
  4. Kusaidiana na wafuasi wao katika kuamrisha mema na kuondosha maovu katika jamii.
  5. Kuonya kutokana na adhabu na kubashiria mema kwa wafanyao mema.


 

  1. Kuamini Siku ya Mwisho.

-    Ni kuwa na yakini moyoni kuwa kuna maisha mengine baada ya kufa.

  • Hatua za maisha baada ya kufa:
    1. Kutokwa na roho.
    2. Maisha ya kaburini (Barzaq).
    3. Kufufuliwa. 
    4. Kuhesabiwa (Hisabu).
    5. Kuishi Peponi au Motoni milele

    -  Kwa mujibu wa amali zao (vitendo vyao).

 

  1. Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu (s.w).
  • Ni kuwa na yakini moyoni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w) anao mpango wa viumbe vyake vyote alioweka kabla ya kuumba chochote.

 

-    Amekiumba kila kiumbe kwa lengo maalumu na kukikadiria mahitaji yake yote.

    Rejea Qur’an (11:6), (57:22), (54:49) na (25:2). 

  • Nguzo za Imani.
  1. Kumuamini Mwenyezi Mungu.
  2. Kuamini Malaika wake.
  3. Kuamini Vitabu Vyake.
  4. Kuamini Mitume Wake.
  5. Kuamini siku ya Mwisho.
  6. Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu.

 

  1. Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Imani juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu ni jambo la kwanza kabisa kwa kila mwenye akili timamu kupitia ishara na maumbile mbali mbali yanayotuzunguka.

        Rejea Qur’an (3:190).

   

    -    Baada ya kumtambua, ni kumuabudu ipasavyo na kutomshirikisha katika sifa na majina yake matukufu na kiumbe yeyote.

        Rejea Qur’an (18:109), (31:27), (57:1-7), (59:22-24).

        Rejea Kitabu cha 2, EDK, Shule za Sekondari; Uk.8-16.

 

  1. Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu.

-    Malaika ni viumbe wa Mwenyezi Mungu walioumbwa kutokana na nuru kwa lengo la kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).

 

-    Ni viumbe wa kiroho, wasio na jinsia, wenye mabawa na wenye uwezo wa kujimithilisha na kitu (kiumbe) chochote.

 

-    Hawana matashi ya kibinaadamu kama kula, kulala, kunywa, kuchoka, kuugua na hawana hiari kwa kila wanachoamrishwa na Mwenyezi Mungu (s.w).

    Rejea Qur’an (16:49-50), (7:206) na (21:26-27).

 

  1. Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Kuamini vitabu vya Allah (s.w) ni lazima kwa kila muumini wa kweli kama vilivyoainishwa katika Qur’an, ambavyo baadhi ni;

  1. Suhufi – aliyoteremshiwa Nabii Ibrahim (a.s) na Nabii Musa (a.s).
  2. Taurat – aliyoteremshiwa Nabii Musa (a.s)
  3. Zaburi – aliyoteremshiwa Nabii Daud (a.s)
  4. Injili – aliyoteremshiwa Nabii Isa (a.s) na 
  5. Qur’an – aliyoteremshiwa Nabii au Mtume Muhammad (s.a.w). 

 

-    Vitabu hivi vimeteremshwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika njia sahihi na iliyonyooka ya maisha yao ili kufikia lengo la kuumbwa kwao.

    Rejea Qur’an (57:25) na (5:46).

 

  • Sababu ya Vitabu Vilivyotangulia kutajwa ndani ya Qur’an:
  • Qur’an ndiyo Kitabu cha mwisho kilichoteremshwa kwa ajili ya kuwaongoza walimwengu wote.
  •  Vimetajwa ili kuwafahamisha waislamu juu ya uwiano, usahihi na upotofu wa mafundisho hayo na yale ya Qur’an.
  •  Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha nafasi na utata wa vitabu hivyo kutumika zama hizi kama mwongozo wa maisha.
  • Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha upungufu, mabadilisho na upotofu uliofanywa ndani ya Vitabu hivyo.

Rejea Qur’an (6:92), (2:75), (4:14), (5:15), (5:48) na (16:64).

 

  1. Kuamini Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w).

-    Mitume ni wanaadamu wanaume walioteliwa ili kuwaongoza na kuwa mifano bora ya kuigwa kwa watu (ummah) wao katika kutekeleza ujumbe wao.

 

  • Idadi kamili ya mitume wote wa Mwenyezi Mungu (s.w) haijulikani, bali waliotajwa ndani ya Qur’an ni 25.

Rejea Qur’an (10:47), (6:83-86)

Rejea Kitabu cha 2, EDK, Shule za Sekondari; Uk.23.

 

  • Sifa za Mitume.
    1. Ni watu walizaliwa, walioa, walikula, waliugua, walikufa, n.k. kama binaadamu wa kawaida isipokuwa Nabii Adamu (a.s).
    2. Walikuwa na kila tabia njema, wakweli, waaminifu na wenye huruma.
    3. Walikuwa na upeo wa Elimu wa hali ya juu kuliko watu wote enzi zao kwa sababu kuletewa kwao wahayi.
    4. Walikuwa Wacha-Mungu wa hali ya juu kuliko watu wote.

 

  • Kazi za Mitume.
  1. Kufahamisha na kufundisha juu ya uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w) na sifa zake. Qur’an (21:25), (16:36).
  2. Kufahamisha mambo ya ghaibu (Akhera) kama Moto, Pepo, Kiyama, Hisabu, Maisha ya Barzaq (kaburini) n.k. 
  3. Kufundisha njia sahihi ya maisha anayoiridhia Mwenyezi Mungu inayopelekea kunusurika na adhabu zake. Qur’an (3:164).
  4. Kusaidiana na wafuasi wao katika kuamrisha mema na kuondosha maovu katika jamii.
  5. Kuonya kutokana na adhabu na kubashiria mema kwa wafanyao mema.


 

  1. Kuamini Siku ya Mwisho.

-    Ni kuwa na yakini moyoni kuwa kuna maisha mengine baada ya kufa.

  • Hatua za maisha baada ya kufa:
    1. Kutokwa na roho.
    2. Maisha ya kaburini (Barzaq).
    3. Kufufuliwa. 
    4. Kuhesabiwa (Hisabu).
    5. Kuishi Peponi au Motoni milele

    -  Kwa mujibu wa amali zao (vitendo vyao).

 

  1. Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu (s.w).
  • Ni kuwa na yakini moyoni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w) anao mpango wa viumbe vyake vyote alioweka kabla ya kuumba chochote.

 

-    Amekiumba kila kiumbe kwa lengo maalumu na kukikadiria mahitaji yake yote.

    Rejea Qur’an (11:6), (57:22), (54:49) na (25:2). 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    4 ICT       ðŸ‘‰    5 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    6 Hadiythi za alif lela u lela    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Tags Dini , DARSA , ALL , Tarehe 2022/01/01/Saturday - 03:58:34 pm     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 1197



Post Nyingine


image Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Swala ya jamaa.
Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa. Soma Zaidi...

image Shahada mbili
Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku. Soma Zaidi...

image Madhumuni ya dola ya uislamu
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo) Soma Zaidi...

image Mambo muhimu anayofanyiwa muislamu kabla ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...