picha

Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Sababu za miguu kufa ganzi.

1. Kupungua kwa virutubisho mbalimbali kwenye mwili,

Kwa kawaida mwili huwa na virutubisho mbalimbali ambavyo ufanya kazi tofautitofauti na vikiongezeka na pia uweza kuleta matatizo na vikipungua na penyewe uleta matatizo na kusababisha miguu kufa ganzi kwa hiyo kama kuna upungufu wa vitamini,B complex usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu kwa hiyo ndio maana watu wenye tatizo hili upewa dawa za vitamini B complex ili kuweza kupunguza kiwango cha ganzi mwilini.

 

2. Pengine kuna tatizo la matumizi ya dawa.

Matumizi ya dawa mbalimbali nazo usababisha kuwepo kwa matatizo ya kwa ganzi kwenye miguu, kwa sababu ya matumizi ya mda mrefu uweza kuleta matatizo kwa mfano kwa matumizi ya dawa za kurefusha maisha kwa wanaozitumia kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu na pia kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu nao pia wana tatizo la kuwepo kwa ganzi kwenye miguu, kwa hiyo wakishagundua tatizo hilo wanapaswa kuwahi kwa daktari ili kuweza kupata matibabu na kuendelea na hali yao ya kawaida.

 

3. Kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili ambapo mwili uelemewa na jinsi ya kusafirisha damu huwa kwa shida hali ambayo Usababisha miguu kufa ganzi.

 

4. Kuwepo kwa Ugonjwa wa kisukari.

Kwa namna moja au nyingine kuna kipindigonjwa wa kisukari hasa wa siku nyingi upatwa na tatizo la kuwepo kwa ganzi mwilini hii ni hali ya kawaida kwa wagonjwa wa kisukari kwa hiyo wakipatwa na tatizo kama hili ni vizuri kabisa kupata matibabu ili kuweza kuendelea na maisha ya kawaida.

 

5. Pia na wagonjwa wenye shinikizo la damu huwa matatizo mbalimbali ambayo Usababisha pia miguu kufa ganzi kwa hiyo ni vizuri kabisa wagonjwa wa hivi wakishapata tatizo kama hili ni kujitahidi kabisa kumwona daktari ili waweze kupata msada zaidi.

 

6. Hili tatizo lipo na linatibika kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kupata msaada zaidi na kuepukana na tatizo hili.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3327

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 web hosting     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake

Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake

Soma Zaidi...
Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi kwenye mapafu

Posti hii inaonyesha dalili za fangasi kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)

Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu

Soma Zaidi...
ninatatizo la miguu kuuma nimepima wanasema seli nyeupe za damu ipo chini Sana sasa nauliza dawa hizi za vitamin k na sindano vinaweza nisaidia?

Upungufu wa damu ni tatizo la kiafya, lakini kupunguwa seli nyeupe za damu ni tatizo zaidi, nikwa sabaabu seli hizi ndizo ambazo hupambana na wadudu shambulizi wanapoingia mwilini.

Soma Zaidi...
Madhara ya kushindwa kupitisha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.

Soma Zaidi...