picha

Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Sababu za miguu kufa ganzi.

1. Kupungua kwa virutubisho mbalimbali kwenye mwili,

Kwa kawaida mwili huwa na virutubisho mbalimbali ambavyo ufanya kazi tofautitofauti na vikiongezeka na pia uweza kuleta matatizo na vikipungua na penyewe uleta matatizo na kusababisha miguu kufa ganzi kwa hiyo kama kuna upungufu wa vitamini,B complex usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu kwa hiyo ndio maana watu wenye tatizo hili upewa dawa za vitamini B complex ili kuweza kupunguza kiwango cha ganzi mwilini.

 

2. Pengine kuna tatizo la matumizi ya dawa.

Matumizi ya dawa mbalimbali nazo usababisha kuwepo kwa matatizo ya kwa ganzi kwenye miguu, kwa sababu ya matumizi ya mda mrefu uweza kuleta matatizo kwa mfano kwa matumizi ya dawa za kurefusha maisha kwa wanaozitumia kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu na pia kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu nao pia wana tatizo la kuwepo kwa ganzi kwenye miguu, kwa hiyo wakishagundua tatizo hilo wanapaswa kuwahi kwa daktari ili kuweza kupata matibabu na kuendelea na hali yao ya kawaida.

 

3. Kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili ambapo mwili uelemewa na jinsi ya kusafirisha damu huwa kwa shida hali ambayo Usababisha miguu kufa ganzi.

 

4. Kuwepo kwa Ugonjwa wa kisukari.

Kwa namna moja au nyingine kuna kipindigonjwa wa kisukari hasa wa siku nyingi upatwa na tatizo la kuwepo kwa ganzi mwilini hii ni hali ya kawaida kwa wagonjwa wa kisukari kwa hiyo wakipatwa na tatizo kama hili ni vizuri kabisa kupata matibabu ili kuweza kuendelea na maisha ya kawaida.

 

5. Pia na wagonjwa wenye shinikizo la damu huwa matatizo mbalimbali ambayo Usababisha pia miguu kufa ganzi kwa hiyo ni vizuri kabisa wagonjwa wa hivi wakishapata tatizo kama hili ni kujitahidi kabisa kumwona daktari ili waweze kupata msada zaidi.

 

6. Hili tatizo lipo na linatibika kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kupata msaada zaidi na kuepukana na tatizo hili.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3985

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 ai web app     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa kisonono

Kisonono ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria wa zinaa ambao wanaweza kuwaambukiza wanaume na wanawake. Kisonono mara nyingi huathiri urethra, puru au koo. Kwa wanawake, ugonjwa wa kisonono unaweza pia kuambukiza kizazi.

Soma Zaidi...
Kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Soma Zaidi...
Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi kwenye mapafu

Posti hii inaonyesha dalili za fangasi kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Matibabu ya mba na jinsi ya kuondoa madoa.

​Mba ni maambukizi ya fangasi ya ngozi (Malassezia) yanayotokea kwenye ngozi ya watu wengi. Fangasi huyu huchangia katika kuvuruga utengenezwaji wa rangi ya ngozi (melanin), na kusababisha madoa ya rangi nyeupe, kahawia, au mekundu. Ingawa mba si ugonjwa wa kuambukiza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, ni hali inayoweza kujirudia mara kwa mara. Makala hii inaelezea tiba bora na mbinu za kuondoa madoa yanayobaki baada ya fangasi kuondoka.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...