Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.
Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono.
1. Ili kuweza kuzuia ugonjwa wa kisonono ni vizuri kabisa kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ambapo utokea pale mtu mmoja anapojamiiana na mwingine ambaye ana ugonjwa huo bila kutumia kinga kwa hiyo ugonjwa huo utoka kwa mto mmoja kwenda kwa mwingine.
2. Na pia uweza kusambaa wakati mtoto anapozaliwa.
Pale mtoto akitaka kupita kwenye via vya uzazi vya Mama kabla hajatoka nje anaweza kupata ugonjwa huu ikiwa Mama ana ugonjwa wa kisonono, kwa hiyo baada ya kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ni vizuri kujua njia za kutibu kama ifuatavyo.
3. Kutumia kondom wakati wa kujamiiana.
Kama una wasiwasi na mpenzi unayejamiiana naye ni vizuri kabisa kutumia kondom, kwa sababu katika matumizi ya kinga wadudu hawawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine wakati wa kujamiiana.
4. Matumizi ya gloves kwa wahudumu wa afya ni muhimu sana.
Kwa Sababu ugonjwa huu kwa wakati mwingine unaweza kutokea kwa kupitia kwenye maji maji, kwa hiyo Mama kama anafanyiwa uchunguzi wa kwenye via vya uzazi Ili kuangalia njia na mambo mengine wakati wa uchungu ni vizuri kutumia gloves Ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huu.
5. Kitu kikubwa na cha maana zaidi ni kiwapima wanawake wajawazito.
Kwa kufanya hivyo ni rahisi kumtambua ni nani mgonjwa na kumwanzishia matibabu au ni nani ambaye sio mgonjwa na kuweza kujikinga zaidi, kwa hiyo ikitokea Mama anaumwa ni vizuri kabisa kumtibu na mwenza wake na wakati wa matibabu waache kujamiiana kwa mda mpaka matibabu yatakapoisha,
6. Kuachana na tabia ya kuchangiana nguo.
Kuna tabia ya watu kuchangiana nguo kama vile chupi na taulo, tabia hii kwa wingi utaikuta kwa wanafunzi wa secondary hasa wasichana wanaoishi kwenye shule za bweni, ni vibaya kwa sababu kama Kuna mwenye ugonjwa huu anaweza akasambaza kwa wengine.
7. Na pia kuachana na tabia ya kutumia via vya uzazi vya bandia, kwa mfano unaweza kukuta mtoto wa kike ana uboo uliotengenezwa kwa bandia akisikia hamu ya kuwa na mwanaume anautumia huo na pia Kuna kipindi anawapatia wengine nao wanaotumia kama Kuna mmoja wapo ana ugonjwa wa kisonono unaweza kukuta wanafunzi wengi Wana ugonjwa huu hata kama wako bweni na hawatoki nje.
8 . Vile vile elimu inapaswa kutolewa kwa wingi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu Kuna ambao hawana taarifa kabisa kuhusu kuwepo kwa magonjwa haya, na kwamba yanatibika ni vizuri kabisa kutoa elimu kwa jamii Ili kujua yafuatayo. Njia zinasababisha kuwepo kwa ugonjwa huu, matibabu yake, madhara ya ugonjwa huu na pia namna ya kuepuka ugonjwa huu.
9. Kwa kufanya hivyo jamii itaweza kushutuka na kufuata utaratibu unaofaa Ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama na pia wanawasaidia watoto wadogo kuepukana na kuzaliwa na ugonjwa huu ambapo usababisha magonjwa ya macho kama mtoto amezaliwa nao hata pengine kuwepo kwa upofu kama matibabu hayajafanyika mapema
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 web hosting π4 ai web app π5 kitabu cha Simulizi π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi
Kubana kwa kifuwa ni katika hali ambazo si naweza kuhatarisha maisha. Huwenda kuwa ni miongoni mwa dalili za magonjwa mengi. Je unadhani na HIv na UKIMWI ni moja ya magonjwa hayo?
Soma Zaidi...Dalili za tatizo la nguvu za kiume
Tatizo la nguvu za kiume ni changamoto inayowakumba wanaume wengi duniani, lakini mara nyingi huogopwa kulizungumzia kutokana na aibu au hofu. Hali hii inaweza kuathiri afya ya mwili, akili, na hata mahusiano ya kimapenzi. Kutambua dalili mapema ni hatua muhimu ya kupata matibabu sahihi na kurejesha hali ya kawaida. Katika makala hii, tutachambua dalili kuu za tatizo la nguvu za kiume, sababu zake, pamoja na ukweli muhimu unaopaswa kufahamika
Soma Zaidi...Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa uti wa mgongo, ni ugonjwa unaoshambulia sehemu inayofunika ubongo na pia sehemu ya spinal cord
Soma Zaidi...Mbinu za kuzuia na kuepukana na maradhi ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepukana na tatizo la ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.
Soma Zaidi...Vitamini B12: Kazi zake na vyakula vyenye wingi wake.
Vitamini B12 (cobalamin) ni kirutubisho muhimu sana ambacho mwili wa binadamu hauwezi kujitengenezea wenyewe. Ni vitamini inayoyeyuka kwenye maji na ina jukumu la msingi katika kudumisha mfumo wa neva, utengenezaji wa damu, na ufanisi wa DNA. Ukosefu wake unaweza kusababisha madhara makubwa kiafya, ikiwemo upungufu wa damu na matatizo ya neva. Makala haya yanalenga kutoa elimu kuhusu kazi za vitamini hii na jinsi unavyoweza kuipata kupitia lishe bora.
Soma Zaidi...Mashambulizi ya hofu (Panic Attacks): Hatua za kuchukua yanapotokea.
βMashambulizi ya hofu (panic attacks) ni hali ya ghafla ya woga mkali inayoweza kuambatana na dalili za kimwili zinazotisha. Makala haya yanafafanua kwa kina nini ni mashambulizi ya hofu, hatua za haraka za kuchukua yanapotokea, na umuhimu wa kutafuta msaada wa kitaalamu ili kudhibiti afya ya akili kwa muda mrefu.
Soma Zaidi...