Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.
Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono.
1. Ili kuweza kuzuia ugonjwa wa kisonono ni vizuri kabisa kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ambapo utokea pale mtu mmoja anapojamiiana na mwingine ambaye ana ugonjwa huo bila kutumia kinga kwa hiyo ugonjwa huo utoka kwa mto mmoja kwenda kwa mwingine.
2. Na pia uweza kusambaa wakati mtoto anapozaliwa.
Pale mtoto akitaka kupita kwenye via vya uzazi vya Mama kabla hajatoka nje anaweza kupata ugonjwa huu ikiwa Mama ana ugonjwa wa kisonono, kwa hiyo baada ya kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ni vizuri kujua njia za kutibu kama ifuatavyo.
3. Kutumia kondom wakati wa kujamiiana.
Kama una wasiwasi na mpenzi unayejamiiana naye ni vizuri kabisa kutumia kondom, kwa sababu katika matumizi ya kinga wadudu hawawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine wakati wa kujamiiana.
4. Matumizi ya gloves kwa wahudumu wa afya ni muhimu sana.
Kwa Sababu ugonjwa huu kwa wakati mwingine unaweza kutokea kwa kupitia kwenye maji maji, kwa hiyo Mama kama anafanyiwa uchunguzi wa kwenye via vya uzazi Ili kuangalia njia na mambo mengine wakati wa uchungu ni vizuri kutumia gloves Ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huu.
5. Kitu kikubwa na cha maana zaidi ni kiwapima wanawake wajawazito.
Kwa kufanya hivyo ni rahisi kumtambua ni nani mgonjwa na kumwanzishia matibabu au ni nani ambaye sio mgonjwa na kuweza kujikinga zaidi, kwa hiyo ikitokea Mama anaumwa ni vizuri kabisa kumtibu na mwenza wake na wakati wa matibabu waache kujamiiana kwa mda mpaka matibabu yatakapoisha,
6. Kuachana na tabia ya kuchangiana nguo.
Kuna tabia ya watu kuchangiana nguo kama vile chupi na taulo, tabia hii kwa wingi utaikuta kwa wanafunzi wa secondary hasa wasichana wanaoishi kwenye shule za bweni, ni vibaya kwa sababu kama Kuna mwenye ugonjwa huu anaweza akasambaza kwa wengine.
7. Na pia kuachana na tabia ya kutumia via vya uzazi vya bandia, kwa mfano unaweza kukuta mtoto wa kike ana uboo uliotengenezwa kwa bandia akisikia hamu ya kuwa na mwanaume anautumia huo na pia Kuna kipindi anawapatia wengine nao wanaotumia kama Kuna mmoja wapo ana ugonjwa wa kisonono unaweza kukuta wanafunzi wengi Wana ugonjwa huu hata kama wako bweni na hawatoki nje.
8 . Vile vile elimu inapaswa kutolewa kwa wingi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu Kuna ambao hawana taarifa kabisa kuhusu kuwepo kwa magonjwa haya, na kwamba yanatibika ni vizuri kabisa kutoa elimu kwa jamii Ili kujua yafuatayo. Njia zinasababisha kuwepo kwa ugonjwa huu, matibabu yake, madhara ya ugonjwa huu na pia namna ya kuepuka ugonjwa huu.
9. Kwa kufanya hivyo jamii itaweza kushutuka na kufuata utaratibu unaofaa Ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama na pia wanawasaidia watoto wadogo kuepukana na kuzaliwa na ugonjwa huu ambapo usababisha magonjwa ya macho kama mtoto amezaliwa nao hata pengine kuwepo kwa upofu kama matibabu hayajafanyika mapema
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 web hosting π3 Kitabu cha Afya π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Madrasa kiganjani π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Ni zipi dalili za awali za pumu
Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.
Soma Zaidi...Jinsi ya kujenga afya ya akili katika ulimwengu wa sasa.
βKatika ulimwengu wa kidijitali na wenye kasi kubwa, afya ya akili imekuwa rasilimali muhimu zaidi kwa binadamu. Makala haya yanachunguza mbinu za kisayansi na kivitendo za kujenga ustahimilivu wa kiakili, kudhibiti mfadhaiko wa teknolojia, na kukuza usawaziko wa maisha. Kupitia mwongozo huu, utajifunza jinsi ya kuweka mipaka, kuboresha mahusiano, na kutumia mazoea ya kujijali (self-care) ili kudumisha utulivu wa ndani katikati ya changamoto za kisasa.
Soma Zaidi...Maumivu ya kichwa cha mara kwa mara (Migraine): Dalili na tiba.
Migraine si maumivu ya kawaida ya kichwa; ni hali ya mfumo wa neva inayoweza kuathiri vibaya maisha ya kila siku ya mtu. Inajidhihirisha kwa maumivu makali ya upande mmoja wa kichwa, yanayoambatana na kichefuchefu, kutapika, na unyeti mkubwa kwa mwanga na sauti. Makala haya yanafafanua kwa kina kile kinachotokea wakati wa shambulio la migraine, jinsi ya kutofautisha na maumivu mengine ya kichwa, na mikakati ya kitaalamu ya kudhibiti na kutibu hali hii.
Soma Zaidi...Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.
Soma Zaidi...Upele wa vipele (Shingles): Dalili na matibabu.
Upele wa vipele (Shingles), unaojulikana kitaalamu kama Herpes Zoster, ni ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kirusi kilekile kinachosababisha tetekuwanga (Chickenpox). Baada ya mtu kupona tetekuwanga, kirusi hicho hubaki kimejificha katika mfumo wa neva kwa miaka mingi. Kinapochochewa na kupungua kwa kinga ya mwili, uzee, au msongo wa mawazo, kirusi hujitokeza tena kama upele wa vipele. Makala haya yanaelezea dalili zake na jinsi ya kupata matibabu ya haraka.
Soma Zaidi...