Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono.

1. Ili kuweza kuzuia ugonjwa wa kisonono ni vizuri kabisa kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ambapo utokea pale mtu mmoja anapojamiiana na mwingine ambaye ana ugonjwa huo bila kutumia kinga kwa hiyo ugonjwa huo utoka kwa mto mmoja kwenda kwa mwingine.

 

 

2. Na pia uweza kusambaa wakati mtoto anapozaliwa.

Pale mtoto akitaka kupita kwenye via vya uzazi vya Mama kabla hajatoka nje anaweza kupata ugonjwa huu ikiwa Mama ana ugonjwa wa kisonono, kwa hiyo baada ya kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ni vizuri kujua njia za kutibu kama ifuatavyo.

 

 

3. Kutumia kondom wakati wa kujamiiana.

Kama una wasiwasi na mpenzi unayejamiiana naye ni vizuri kabisa kutumia kondom, kwa sababu katika matumizi ya kinga wadudu hawawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine wakati wa kujamiiana.

 

 

4. Matumizi ya gloves kwa wahudumu wa afya ni muhimu sana.

Kwa Sababu ugonjwa huu kwa wakati mwingine unaweza kutokea kwa kupitia kwenye maji maji, kwa hiyo Mama kama anafanyiwa uchunguzi wa kwenye via vya uzazi Ili kuangalia njia na mambo mengine wakati wa uchungu ni vizuri kutumia gloves Ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huu.

 

 

5. Kitu kikubwa na cha maana zaidi ni kiwapima wanawake wajawazito.

Kwa kufanya hivyo ni rahisi kumtambua ni nani mgonjwa na kumwanzishia matibabu au ni nani ambaye sio mgonjwa na kuweza kujikinga zaidi, kwa hiyo ikitokea Mama anaumwa ni vizuri kabisa kumtibu na mwenza wake na wakati wa matibabu waache kujamiiana kwa mda mpaka matibabu yatakapoisha,

 

 

6. Kuachana na tabia ya kuchangiana nguo.

Kuna tabia ya watu kuchangiana nguo kama vile chupi na taulo, tabia hii kwa wingi utaikuta kwa wanafunzi wa secondary hasa wasichana wanaoishi kwenye shule za bweni, ni vibaya kwa sababu kama Kuna mwenye ugonjwa huu anaweza akasambaza kwa wengine.

 

 

7. Na pia kuachana na tabia ya kutumia via vya uzazi vya bandia, kwa mfano unaweza kukuta mtoto wa kike ana uboo uliotengenezwa kwa bandia akisikia hamu ya kuwa na mwanaume anautumia huo na pia Kuna kipindi anawapatia wengine nao wanaotumia kama Kuna mmoja wapo ana ugonjwa wa kisonono unaweza kukuta wanafunzi wengi Wana ugonjwa huu hata kama wako bweni na hawatoki nje.

 

 

8 . Vile vile elimu inapaswa kutolewa kwa wingi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu Kuna ambao hawana taarifa kabisa kuhusu kuwepo kwa magonjwa haya, na kwamba yanatibika ni vizuri kabisa kutoa elimu kwa jamii Ili kujua yafuatayo. Njia zinasababisha kuwepo kwa ugonjwa huu, matibabu yake, madhara ya ugonjwa huu na pia namna ya kuepuka ugonjwa huu.

 

 

9. Kwa kufanya hivyo jamii itaweza kushutuka na kufuata utaratibu unaofaa Ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama na pia wanawasaidia watoto wadogo kuepukana na kuzaliwa na ugonjwa huu ambapo usababisha magonjwa ya macho kama mtoto amezaliwa nao hata pengine kuwepo kwa upofu kama matibabu hayajafanyika mapema

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1830

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

  Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).
Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).

Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre

Soma Zaidi...
Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)
Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)

Post hii inaelezea kuhusiana naร‚ย Sarataniร‚ย ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia.

Soma Zaidi...
ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini
ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini

Post hii itakwenda kuzungumzia ugonjwa wa gout unaosababishwa na ongezeko la asidi mwilini.

Soma Zaidi...
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.

Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.
Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.

Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu

Soma Zaidi...
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV

Soma Zaidi...
Dalili ya pressure ya kupanda
Dalili ya pressure ya kupanda

Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya

Soma Zaidi...
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia

Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...
Dawa za kutuliza maumivu na kazi zake
Dawa za kutuliza maumivu na kazi zake

Post hii inahusu zaidi dawa za kupunguza maumivu na kazi zake, ni dawa ambazo upunguza maumivu kwenye mwili wa binadamu.

Soma Zaidi...
 Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu
Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa yanayosababisha madhara kwenye mapafu na kitaalamu hujulikana Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu

Soma Zaidi...