Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.
Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono.
1. Ili kuweza kuzuia ugonjwa wa kisonono ni vizuri kabisa kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ambapo utokea pale mtu mmoja anapojamiiana na mwingine ambaye ana ugonjwa huo bila kutumia kinga kwa hiyo ugonjwa huo utoka kwa mto mmoja kwenda kwa mwingine.
2. Na pia uweza kusambaa wakati mtoto anapozaliwa.
Pale mtoto akitaka kupita kwenye via vya uzazi vya Mama kabla hajatoka nje anaweza kupata ugonjwa huu ikiwa Mama ana ugonjwa wa kisonono, kwa hiyo baada ya kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ni vizuri kujua njia za kutibu kama ifuatavyo.
3. Kutumia kondom wakati wa kujamiiana.
Kama una wasiwasi na mpenzi unayejamiiana naye ni vizuri kabisa kutumia kondom, kwa sababu katika matumizi ya kinga wadudu hawawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine wakati wa kujamiiana.
4. Matumizi ya gloves kwa wahudumu wa afya ni muhimu sana.
Kwa Sababu ugonjwa huu kwa wakati mwingine unaweza kutokea kwa kupitia kwenye maji maji, kwa hiyo Mama kama anafanyiwa uchunguzi wa kwenye via vya uzazi Ili kuangalia njia na mambo mengine wakati wa uchungu ni vizuri kutumia gloves Ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huu.
5. Kitu kikubwa na cha maana zaidi ni kiwapima wanawake wajawazito.
Kwa kufanya hivyo ni rahisi kumtambua ni nani mgonjwa na kumwanzishia matibabu au ni nani ambaye sio mgonjwa na kuweza kujikinga zaidi, kwa hiyo ikitokea Mama anaumwa ni vizuri kabisa kumtibu na mwenza wake na wakati wa matibabu waache kujamiiana kwa mda mpaka matibabu yatakapoisha,
6. Kuachana na tabia ya kuchangiana nguo.
Kuna tabia ya watu kuchangiana nguo kama vile chupi na taulo, tabia hii kwa wingi utaikuta kwa wanafunzi wa secondary hasa wasichana wanaoishi kwenye shule za bweni, ni vibaya kwa sababu kama Kuna mwenye ugonjwa huu anaweza akasambaza kwa wengine.
7. Na pia kuachana na tabia ya kutumia via vya uzazi vya bandia, kwa mfano unaweza kukuta mtoto wa kike ana uboo uliotengenezwa kwa bandia akisikia hamu ya kuwa na mwanaume anautumia huo na pia Kuna kipindi anawapatia wengine nao wanaotumia kama Kuna mmoja wapo ana ugonjwa wa kisonono unaweza kukuta wanafunzi wengi Wana ugonjwa huu hata kama wako bweni na hawatoki nje.
8 . Vile vile elimu inapaswa kutolewa kwa wingi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu Kuna ambao hawana taarifa kabisa kuhusu kuwepo kwa magonjwa haya, na kwamba yanatibika ni vizuri kabisa kutoa elimu kwa jamii Ili kujua yafuatayo. Njia zinasababisha kuwepo kwa ugonjwa huu, matibabu yake, madhara ya ugonjwa huu na pia namna ya kuepuka ugonjwa huu.
9. Kwa kufanya hivyo jamii itaweza kushutuka na kufuata utaratibu unaofaa Ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama na pia wanawasaidia watoto wadogo kuepukana na kuzaliwa na ugonjwa huu ambapo usababisha magonjwa ya macho kama mtoto amezaliwa nao hata pengine kuwepo kwa upofu kama matibabu hayajafanyika mapema
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kumfurahisha Mwenza Wako
Mahusiano yenye furaha hayajitokezi kwa bahati; yanajengwa kupitia juhudi za makusudi. Posti hii inatoa mwongozo wa mbinu rahisi lakini zenye nguvu za kumfanya mwenza wako ajihisi anathaminiwa, anapendwa, na anafurahia maisha ya pamoja nawe.
Soma Zaidi...Ishara za Uchungu wa Kujifungua Zinapoanza
Kipindi cha mwisho cha ujauzito kinaweza kuambatana na mchanganyiko wa msisimko na wasiwasi. Posti hii inaangazia ishara kuu ambazo mwili hutoa wakati uchungu wa uzazi unapoanza, ikikupa mwongozo wa wakati mwafaka wa kwenda hospitali.
Soma Zaidi...Dalili za Mwanzoni za Virusi vya UKIMWI
Makala haya yanatoa mwongozo kuhusu dalili za awali zinazoweza kujitokeza baada ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (HIV). Tunasisitiza kuwa dalili hizi si mahususi kwa HIV pekee na njia pekee ya kujua hali yako ya afya ni kufanya vipimo vya maabara.
Soma Zaidi...Dalili za UKIMWI kwa Vijana wa Kiume
Posti hii inatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu dalili zinazoweza kujitokeza kwa kijana wa kiume mwenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU). Lengo ni kuondoa unyanyapaa na kuhimiza umuhimu wa kupima na kuanza matibabu mapema.
Soma Zaidi...TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).
TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa,ni madhara ambayo utokea endapo Maambukizi kwenye mifupa yasipotibiwa kwa mda wake.
Soma Zaidi...