picha

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono.

1. Ili kuweza kuzuia ugonjwa wa kisonono ni vizuri kabisa kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ambapo utokea pale mtu mmoja anapojamiiana na mwingine ambaye ana ugonjwa huo bila kutumia kinga kwa hiyo ugonjwa huo utoka kwa mto mmoja kwenda kwa mwingine.

 

 

2. Na pia uweza kusambaa wakati mtoto anapozaliwa.

Pale mtoto akitaka kupita kwenye via vya uzazi vya Mama kabla hajatoka nje anaweza kupata ugonjwa huu ikiwa Mama ana ugonjwa wa kisonono, kwa hiyo baada ya kujua njia za kusambaa kwa ugonjwa huu ni vizuri kujua njia za kutibu kama ifuatavyo.

 

 

3. Kutumia kondom wakati wa kujamiiana.

Kama una wasiwasi na mpenzi unayejamiiana naye ni vizuri kabisa kutumia kondom, kwa sababu katika matumizi ya kinga wadudu hawawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine wakati wa kujamiiana.

 

 

4. Matumizi ya gloves kwa wahudumu wa afya ni muhimu sana.

Kwa Sababu ugonjwa huu kwa wakati mwingine unaweza kutokea kwa kupitia kwenye maji maji, kwa hiyo Mama kama anafanyiwa uchunguzi wa kwenye via vya uzazi Ili kuangalia njia na mambo mengine wakati wa uchungu ni vizuri kutumia gloves Ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huu.

 

 

5. Kitu kikubwa na cha maana zaidi ni kiwapima wanawake wajawazito.

Kwa kufanya hivyo ni rahisi kumtambua ni nani mgonjwa na kumwanzishia matibabu au ni nani ambaye sio mgonjwa na kuweza kujikinga zaidi, kwa hiyo ikitokea Mama anaumwa ni vizuri kabisa kumtibu na mwenza wake na wakati wa matibabu waache kujamiiana kwa mda mpaka matibabu yatakapoisha,

 

 

6. Kuachana na tabia ya kuchangiana nguo.

Kuna tabia ya watu kuchangiana nguo kama vile chupi na taulo, tabia hii kwa wingi utaikuta kwa wanafunzi wa secondary hasa wasichana wanaoishi kwenye shule za bweni, ni vibaya kwa sababu kama Kuna mwenye ugonjwa huu anaweza akasambaza kwa wengine.

 

 

7. Na pia kuachana na tabia ya kutumia via vya uzazi vya bandia, kwa mfano unaweza kukuta mtoto wa kike ana uboo uliotengenezwa kwa bandia akisikia hamu ya kuwa na mwanaume anautumia huo na pia Kuna kipindi anawapatia wengine nao wanaotumia kama Kuna mmoja wapo ana ugonjwa wa kisonono unaweza kukuta wanafunzi wengi Wana ugonjwa huu hata kama wako bweni na hawatoki nje.

 

 

8 . Vile vile elimu inapaswa kutolewa kwa wingi kuhusu ugonjwa huu kwa sababu Kuna ambao hawana taarifa kabisa kuhusu kuwepo kwa magonjwa haya, na kwamba yanatibika ni vizuri kabisa kutoa elimu kwa jamii Ili kujua yafuatayo. Njia zinasababisha kuwepo kwa ugonjwa huu, matibabu yake, madhara ya ugonjwa huu na pia namna ya kuepuka ugonjwa huu.

 

 

9. Kwa kufanya hivyo jamii itaweza kushutuka na kufuata utaratibu unaofaa Ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama na pia wanawasaidia watoto wadogo kuepukana na kuzaliwa na ugonjwa huu ambapo usababisha magonjwa ya macho kama mtoto amezaliwa nao hata pengine kuwepo kwa upofu kama matibabu hayajafanyika mapema

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2335

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 web hosting     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 ai web app     ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰5 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa pombe wakati Mtoto akiwa tumboni

Ugonjwa wa ulevi wakati Mtoto akiwa tumboni (fetasi) ni hali ya mtoto inayotokana na unywaji pombe wakati wa ujauzito wa mama. Ugonjwa wa pombe wa fetasi husababisha uharibifu wa ubongo na matatizo ya ukuaji.

Soma Zaidi...
Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).

Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa Ebola.

Virusi vya Ebola ni virusi vinavyohusiana vinavyosababisha Homa zaร‚ย hemorrhagic magonjwa yanayoambatana na kutokwa na damu nyingi (kuvuja damu), viungo kushindwa kufanya kazi na, mara nyingi, kifo. Virusi vya Ebola na virusi huishi kwa wanyama, na wanad

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa, ni dalili ambazo ujitokeza tu mtoto anapozaliwa kwa hiyo dalili hizi zinapaswa kuzuiwa ili zisilete madhara makubwa.

Soma Zaidi...