Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwa jamii.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba Ukimwi ni Ugonjwa ambao hauna dawa na umeweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuleta madhara katika jamii kwa hiyo tunapaswa kujiadhari na ugonjwa huu kwa sababu hauna dawa na unasababisha kifo kwa kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna madhara au matokeo hasi yaliyotokana na Ugonjwa huu kama ifuatavyo.
2. Kushuka kwa uchumi wa nchi.
Kwa sababu selikali inatumia hela kubwa kununua vidonge vya kupunguza nguvu za virusi na kutumia pesa kwa kulipa mishahara wafanyakazi wanaohusika na kutoa dawa, na pia kutoa semina mbalimbali kutoka sehemu moja kwenda nyingine ili kuhamasisha watu wapime na kujua afya zao, kwa kufanya hivyo uchumi unashuka badala ya pesa hizo zingetumika kujenga barabara na shughuli nyingine za kimaendeleo, kwa hiyo kuwepo kwa gonjwa hili kumesababisha kushuka kwa uchumi.
3. Pia kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha vifo vya wapendwa wetu,ambapo kumesababisha kuwepo kwa watoto wengi wa mitaani na yatima kila kona kwa sababu ya kutokuwepo mtu wa kuwatunza na kuwapatia mahitaji yao, hali ambayo Usababisha kuongezeka kwa vituo vya watoto yatima na watoto wa mitaani.
4. Vile vie kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa Magonjwa mengine kwa sababu kinga ya mwili inaposhuka tu na Magonjwa nyemelezi yanaongezeka kwa hiyo kuna Magonjwa yaliyosababishwa na kushusha kwa immunity kama vile kifua kikuu, kuharisha na magonjwa mengine kama hayo.
5.Kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa kiasi cha wagane na wajane kwenye jamii na pia vijana kushambuliwa na Ugonjwa huu na hivyo kupunguza nguvu kazi ya nchi.
6.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Ugonjwa huu na kujiwekea mikakati ili tuweze kupunguza idadi ya Maambukizi kwenye jamii zetu kwa sababu Tanzania bila Ukimwi inawezekana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
VIDONDA VYA TUMBO SUGU
VIDONDA VYA TUMBO SUGU Matibabu ya vidonda vya tumbo mara nyingi hufanikiwa, na kusababisha uponyaji wa vidonda.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe au puto katika mshipa wa damu kwenye ubongo. Uvimbe kwenye Ubongo unaweza kuvuja au kupasuka, na kusababisha kuvuja damu kwenye ubongo. Mara nyingi, kupasuka kwa Uvimbe wa Ubongo hutokea katika nafasi kati
Soma Zaidi...Kujiamini na jinsi ya kuondoa hofu ya kushindwa.
Hofu ya kushindwa ni moja ya vikwazo vikubwa vinavyozuia watu wengi kufikia malengo na ndoto zao. Inatufanya tubaki kwenye maeneo tuliyoyazoea (comfort zone) na kuogopa kujaribu fursa mpya. Makala haya yanachambua jinsi hofu hii inavyofanya kazi na kukupa mbinu za kisaikolojia za kukusaidia kujenga ujasiri na kubadili mtazamo wako kuelekea mafanikio makubwa.
Soma Zaidi...Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.
Post hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ni Maambukizi ambayo hutokea kwenye mifupa kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Maumivu ya shingo na mabega kutokana na kazi za ofisini.
Msongo wa mawazo (stress) ni hali ya kawaida ya kisaikolojia na kimwili inayotokana na shinikizo la maisha. Ingawa kiasi kidogo cha msongo kinaweza kuchochea ubunifu na utendaji, msongo wa muda mrefu ni hatari kwa afya ya mwili na akili. Makala haya yanachunguza kwa kina dalili za msongo wa mawazo—kuanzia mabadiliko ya kihisia, kimwili, hadi kitabia—pamoja na mikakati ya kitaalamu ya kuyatambua na kuyadhibiti mapema ili kuzuia madhara ya kudumu.
Soma Zaidi...