Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwa jamii.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba Ukimwi ni Ugonjwa ambao hauna dawa na umeweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuleta madhara katika jamii kwa hiyo tunapaswa kujiadhari na ugonjwa huu kwa sababu hauna dawa na unasababisha kifo kwa kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna madhara au matokeo hasi yaliyotokana na Ugonjwa huu kama ifuatavyo.

 

 

 

 

2. Kushuka kwa uchumi wa nchi.

Kwa sababu selikali inatumia hela kubwa kununua vidonge vya kupunguza nguvu za virusi na kutumia pesa kwa kulipa mishahara wafanyakazi wanaohusika na kutoa dawa, na pia kutoa semina mbalimbali kutoka sehemu moja kwenda nyingine ili kuhamasisha watu wapime na kujua afya zao, kwa kufanya hivyo uchumi unashuka badala ya pesa hizo zingetumika kujenga barabara na shughuli nyingine za kimaendeleo, kwa hiyo kuwepo kwa gonjwa hili kumesababisha kushuka kwa uchumi.

 

 

 

 

3. Pia kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha vifo vya wapendwa wetu,ambapo kumesababisha kuwepo kwa watoto wengi wa mitaani na yatima kila kona kwa sababu ya kutokuwepo mtu wa kuwatunza na kuwapatia mahitaji yao, hali ambayo Usababisha kuongezeka kwa vituo vya watoto yatima na watoto wa mitaani.

 

 

 

 

 

4. Vile vie kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa Magonjwa mengine kwa sababu kinga ya mwili inaposhuka tu na Magonjwa nyemelezi yanaongezeka kwa hiyo kuna Magonjwa yaliyosababishwa na kushusha kwa immunity kama vile kifua kikuu, kuharisha na magonjwa mengine kama hayo.

 

 

 

 

 

5.Kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa kiasi cha wagane na wajane kwenye jamii na pia vijana kushambuliwa na Ugonjwa huu na hivyo kupunguza nguvu kazi ya nchi.

 

 

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Ugonjwa huu na kujiwekea mikakati ili tuweze kupunguza idadi ya Maambukizi kwenye jamii zetu kwa sababu Tanzania bila Ukimwi inawezekana.

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 5709

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Dalili za malaria

Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama.

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Soma Zaidi...
Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)

maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri

Soma Zaidi...
Kupambana na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari

Soma Zaidi...
Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).

Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre

Soma Zaidi...
Dalili za kisukari aina ya type 2

Kisukari cha Aina ya 2, ambacho wakati mmoja kilijulikana kama Kisukari cha watu wazima au kisichotegemea insulini, ni ugonjwa sugu unaoathiri jinsi mwili wako unavyobadilisha sukari (glucose), chanzo muhimu cha nishati ya mwili wako.

Soma Zaidi...
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.

Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt

Soma Zaidi...
Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?

Kama unahisi maumivu ya tumbo huwenda umejiuliza swali hili ukiwa kama mwanamke "Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?". Post hii inakwenda kujibu swali hili

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga

Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali

Soma Zaidi...