Menu



Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwa jamii.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba Ukimwi ni Ugonjwa ambao hauna dawa na umeweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuleta madhara katika jamii kwa hiyo tunapaswa kujiadhari na ugonjwa huu kwa sababu hauna dawa na unasababisha kifo kwa kuwepo kwa Ugonjwa huu kuna madhara au matokeo hasi yaliyotokana na Ugonjwa huu kama ifuatavyo.

 

 

 

 

2. Kushuka kwa uchumi wa nchi.

Kwa sababu selikali inatumia hela kubwa kununua vidonge vya kupunguza nguvu za virusi na kutumia pesa kwa kulipa mishahara wafanyakazi wanaohusika na kutoa dawa, na pia kutoa semina mbalimbali kutoka sehemu moja kwenda nyingine ili kuhamasisha watu wapime na kujua afya zao, kwa kufanya hivyo uchumi unashuka badala ya pesa hizo zingetumika kujenga barabara na shughuli nyingine za kimaendeleo, kwa hiyo kuwepo kwa gonjwa hili kumesababisha kushuka kwa uchumi.

 

 

 

 

3. Pia kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha vifo vya wapendwa wetu,ambapo kumesababisha kuwepo kwa watoto wengi wa mitaani na yatima kila kona kwa sababu ya kutokuwepo mtu wa kuwatunza na kuwapatia mahitaji yao, hali ambayo Usababisha kuongezeka kwa vituo vya watoto yatima na watoto wa mitaani.

 

 

 

 

 

4. Vile vie kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa Magonjwa mengine kwa sababu kinga ya mwili inaposhuka tu na Magonjwa nyemelezi yanaongezeka kwa hiyo kuna Magonjwa yaliyosababishwa na kushusha kwa immunity kama vile kifua kikuu, kuharisha na magonjwa mengine kama hayo.

 

 

 

 

 

5.Kuwepo kwa Ugonjwa huu kumesababisha kuongezeka kwa kiasi cha wagane na wajane kwenye jamii na pia vijana kushambuliwa na Ugonjwa huu na hivyo kupunguza nguvu kazi ya nchi.

 

 

 

6.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Ugonjwa huu na kujiwekea mikakati ili tuweze kupunguza idadi ya Maambukizi kwenye jamii zetu kwa sababu Tanzania bila Ukimwi inawezekana.

 

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 4898


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Njia za kujilinda na kujikinga na UTI
Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujilinda na kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Aina za ajali kwenye kifua,
Post hii inahusu Zaidi aina za ajali kwenye kifua,pamoja na kifua kuwa na sehemu mbalimbali na pia na ajali ambazo utokea Huwa za aina mbalimbali kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

Ufahamu Ugonjwa wa hepatitis B
Hepatitis B Ni maambukizi ya ini ambayo yamekuwa sugu kuanzia mwezi na kuendelea. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Uvimbe kwenye ubongo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe au puto katika mshipa wa damu kwenye ubongo. Uvimbe kwenye Ubongo unaweza kuvuja au kupasuka, na kusababisha kuvuja damu kwenye ubongo. Mara nyingi, kupasuka kwa Uvimbe wa Ubongo hutokea katika nafasi kati Soma Zaidi...

Sababu za maumivu ya viungo na viungo kuwaka moto nini sababu zake
Soma Zaidi...

Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo, matibabu na dawa zake, sababu za kutokea kwake
Utajifunza chanzo cha vidonda vya tumbo, dalili zake, dawa na matibabu yake pamoja na njia za kujilinda na vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

Sababu za maumivu ya tumbo
hapa utajifunza maradhi mbalimbali yanatopelekea kuwepo kwa maumivu ya tumbo Soma Zaidi...

Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)
Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani. Soma Zaidi...

Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo Soma Zaidi...