Menu



FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI

Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.

 

Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.

 

Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.

 

FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME

  1. Kuvimba kwa kichwa cha uume
  2. Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
  3. Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
  4. Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
  5. Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
  6. Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
  7. Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.

DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE

  1. Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
  2. Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
  3. Uuke kuwaka moto kwa ndani
  4. Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
  5. Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
  6. Kutokwa na majimaji kwenye uke
  7. Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.

 

WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA

  1. Wachafu
  2. Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
  3. Wenye kisukari
  4. Wenye HIV
  5. Wenye saratani
  6. Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
  7. Wajawazito

 

NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA

  1. Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
  2. Kutokuvaa nguo mbichi
  3. Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
  4. Kuwa msafi muda wowote
  5. Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
  6. Kuosha uke mara kwa mara
  7. Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
 


                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 3042


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dalili za sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia)
sukari kupungua mwilini (Hypoglycemia) huhusishwa kwa kawaida na matibabu ya Kisukari. Hata hivyo, hali mbalimbali, nyingi zikiwa nadra, zinaweza kusababisha sukari ya chini ya damu kwa watu wasio na Kisukari. Kama vile Homa, Hy Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili Soma Zaidi...

NINI SABABU YA VIDONDA VYA TUMBO
NENO LA AWALI Hapa utaweza kujifunza mambo mengi kuhusu vidonda vyatumbo. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa upungufu wa maji mwilini.
Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji. Soma Zaidi...

Magonjwa ya kuambukiza.
Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya kuambukiza, ni magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuweza kusababisha madhara yale yale kwa mtu aliyeambukizwa au anayeambukiza kwa hiyo Maambukizi yanaweza kuwa ya moja kwa moja au yasi Soma Zaidi...

Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake
Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni. Soma Zaidi...

Maradhi ya Ini na dalili zake, na vipi utajikinga nayo
MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu. Soma Zaidi...

Dalili za ukosefu wa misuli.
Posti hii inahusu dalili za ukosefu wa misuli. ukosefu wa udhibiti wa misuli wakati wa harakati za hiari, kama vile kutembea au kuokota vitu. Ishara ya hali ya msingi, Ataxia inaweza kuathiri harakati, hotuba, harakati za jicho na kumeza. Soma Zaidi...

Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga
Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali Soma Zaidi...

Kushambuliwa kwa moyo na kupumua
Post hii inahusu zaidi kuhusu kushambuliwa kwa moyo na kupumua, kushambuliwa kwa moyo na kupumua kwa kitaala huitwa (cardiopulmonary Arrest) ni kitendo Cha kusimama ghafla kwa moyo na kupumua. Soma Zaidi...