Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa
MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA TENDO LA NDOA
Maumivu wakati wa tendo la ndoa hutokea sana na pengine ni kawaida hasa kwa wanawake. Ijapokuwa kwa wanaume sio sana. Maumivu haya yanaweza kuwa ya tumbo, ya kiuno, ama viungo vya siri yaani uume na uke. Pia maumivu haya yanaweza kutokea wakati wa tendo la ndoa ama baada.
Je na wewe ni katika wanaopatwa na maumivu makali wakati wa tendo la ndoa. Na je umepata kujuwa chanzo cha tatizo lako?. makala hii ni kwa ajili yako. Katika makala hii tutakwenda kuona maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.
Sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.
1.Mkao uliotumika. Ipo baadhi ya mikao inaongeza uwezekano wa kupatwa na maumivu ya tumbo wakati wa tendo. Mikao hii ni ile ambayo inaruhusu uume kuingia ndani zaidi. Kama unasumbuliwa na tatizo hili jaribu kutumia mikao ambayo utaweza kudhibiti uingiaji wa uume.
2.Kama tumbo la uzazi (uterus) limeinama kidogo. Hii hutokea pale tumbo la uzazi linapolalia nyuma kidogo kuelekea kwenye shingo ya uzazi. Hali hii huwewa kupelekea maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.
3.Maka una tatizo la kuota tishu zinazopaswa kuota kwenye tumbo la uzazi zikaota sehemu nyingine. Hali hii hutambulika kama endometruisis. Haki hii huweza kupelekea maumivu ya mgongo, nyonga na tumbo wakati wa tendo la ndoa. Dalili za hali hii ni pamoja na:-
A.Maumivu makali zaidi wakati wa tendo la ndoa
B.Kupata hedhi yenye damu nyingi
C.Kutokwa na damu kabla na baada ya kumaiza hedhi
D.Maumivu ya tumbo
4.Kama ovari ina matatizo yaani inajaa maji, hali hii hutambulika kama ovarian cysts. Hii hutokea endapo juu y aovari ama ndani kunkuwa na kama vijifuko vijidogo vinajaa maji. Sasa vikiwa vidogo havinaga maumivu ila vikiwa ni vikubwa vinaweza kupelekea maumivu ya chini ya tumbo. Maumivu haya yanaweza kuwa makali zaidi wakati wa tendola ndoa. Pia mtu anaweza kupata dalili zifuatazo:-
A.Maumivu ya mgongo wa chini ama kwenye mapaja
B.Unahisi tumbo limejaa ama kushiba, ama tumbo linakuwa zito
C.Tumbo kujaa gezi na kucheua gesi kwa mdomoni.
5.Kama kuna mashambulizi kwenye kibofu kitaalamu hali hii huitwa interstial cystitis. Misuli ya kwenye kibofu inashambuliwa na kuvimba na baadaye kutoa dalili kama:-
A.Maumivu ya tumbo na nyonga
B.Kukojoa mara kwa mara
C.Kujihisi kukojoa tena punde baada ya kukojoa
D.Kuvuja kwa mkojo yaani kutoka mkojo bila ya wewe kujuwa.
E.Maumivu kwenye uke na mashavu ya uke (papa)
6.Kuwa na uvimbe kwenye tumbo la mimba kitaalamu huitwa fibroid. Huu ni uvimbe usiosabababishwa na saratani. Uvimbe huuu huweza kuleta dalili kama:-
A.maumivu ya tumbo na mgongo sehemu ya chini
B.Kupata damu nyingi ya hedhi pamoja na maumivu makali
C.Maumivu wakati wa tendo la ndoa
D.Kukosa choo.
7.Kama mtu ana maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Hapa mtu anaweza kuona dalili kama:-
A.Kutokwa na uchafu ukeni
B.Kutoka na harufu mbaya ukeni
C.Maumivu wakati wa kukojoa na kuhisi kama unaunguwa
D.Maumivu ya tumbo kwa chini pamoja na nyonga
E.Maumivu na kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada ya hedi
8.UTI na PID; kwa pamoja haya ni mashambuizi ya bakteria ama fangasi ama virusi. Mashambulizi haya huathiri mfumo wa uzazi hapa itakuwa na PID na endapo yatashambulia mfumo wa mkojo itakuwa ni UTI. ugonjwa wa UTI na PID huweza kusababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Dalili za PID
A.Maumivu makali ya nyonga wakatii wa tendo la ndoa
B.Maumivu wakati wa kukojoa
C.Kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada
Dalili za UTI
A.Maumivu ya tumbo ambayo huongezeka wakati wa tendo la ndoa
B.Maumivu wakati wa kukojoa
C.Kukojoa mra kwa mara
D.Mkojo mchafu na wenye harufu kali.
9.kama kuna uvimbe katika tezi dume.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa Ugonjwa wa fangasi,ni sababu mbalimbali ambazo zinaweza kusababisha fangasi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa s
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, mara nyingi tatizo hili uwakumba akina mama mbalimbali ambapo mtoto uzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dalili za mimba kutoka, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mimba zote ambazo utaka kutoka kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.
Soma Zaidi...dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya uzito kwa mjamzito, hii ni hali ya kubadilika kwa uzito kwa Mama akiwa na Mimba
Soma Zaidi...